Ta Kamugisha
JF-Expert Member
- May 17, 2011
- 3,536
- 2,187
Wakati uleeee tukisoma, kulikuwa na Tuition moja ipo pale Mwenge nyuma ya Nakiete Phamacy (MAPAMBANO TUITION CENTRE) Nakumbuka kipindi kile wanafundisha wakina Selemani matipa, Magnus kibonde a.k.a P Didy, Mussa Detebha na wengine wengi nimewasahau, kwanza tulianzia pale karibia na Magorofa ya jeshi Mwenge kwa Mzee mmoja alikuwa anaitwa Mzee Chilumba ndo tukahamia nyuma ya Nakiete Phamacy. Enzi hizo vijana tulikuwa tunasoma si mchezo, kwanza palikuwa na ushindani wa shule kwa shule ili shule yako iwe ya kwanza lazima ushike No. 1. Palikuwa hapatoshi jamani siku ya pepa. Kipindi hiko Makongo ipo chini ya Kipingu, ilikuwa makongo ya ukweli si kama ilivyo sasa Palikuwepo na vijana kama Kamna Shomari, Alex mavika, Daudi Bupilipili, Pale Forodhani nawakumbuka wakina Shabani kingazi kwa sasa ni dr, Big Noise, Jangwani namkumbuka Nanzoke Mvungi sijui yuko wapi, Mzumbe namkumbuka Benjamini kamala kwasasa ni dr, Loyola namkumbuka Mtabazi, Azania nimewasahau, kibasila nimeawsahau ila walikuwepo sana tu pamoja na zanaki, Watu walikuwa wanajituma kichizi, Tegeta namkumbuka Datius Mshala kwasasa ni pirot! Azania ilikuwa si mchezo, Pugu nao walikuwepo, Kibasila. Forodhani, Kisutu, Jangwani, Royola, Tegeta na Jitegemee kwa mbali ingawa walikuwa wanakimbia pepa kwa sana. Namkumbuka mdada mmoja wa jangwani alikuwa anaitwa Nanzoke alikuwa ni noma kwa Mathematics! Makongo ilikuwa inabebwa na vijana wa pure mathematics. Kimbembe kilikuwa wakati wa likizo, wakija wale waliobalikiwa kiakili yaani Mzumbe, Ilboru na Kibaha + Tabora Boyz. Hawa jamaa tulikuwa tunashindana nao mpaka kinaeleweka ingawa kiukweli walikuwa juu sana. Kwa sasa nashangaa vijana hawajitumi wanafeli kila kukicha, hakuna ushindani tena baina ya shule na shule! Enzi zetu tulikuwa tunasoma si mchezo jamani ndo maana tupo hapa tulipo au wewe ulipo au nakosea?
Ebu na wewe tukumbushe Tuition yako, bila kusahau zile za ubungo, Mchikichini nk.
Naomba kuwasilisha.
Ebu na wewe tukumbushe Tuition yako, bila kusahau zile za ubungo, Mchikichini nk.
Naomba kuwasilisha.