Beatrice Kamugisha
JF-Expert Member
- May 18, 2019
- 761
- 6,985
Kutumbuliwa kwa Mkurugenzi wa Geita kumeibua mjadala kuhusu kiongozi gani anapaswa kumiliki au kutembelea gani.
Hoja kuu inatokana na kile kinachoelezwa kuwa V8 si anasa kwa wakurugenzi na wamekuwa wakitumia gari hizi kwa miaka kadhaa sasa.
Hi hoja ilipowasilishwa Bungeni wakati wa Spika Makinda ilizua mjadala mkali sana na Serikali ikaazimia kutafuta magari ya bei ya chini lakini baadhi ya mabeberu weusi wakakataa wakidai Mkurugenzi lazima awe na gari la hadhi yake.
Maisha yameenda kasi na karibia viongozi wote waandamizi wa nchi hii wanatumia v8 na mashangingi mengine ya kifahari. Hivyo Mkurugenzi wa Geita amefuata nyayo tu.
Jambo linalozua mtafaruku ni kuhusu utaratibu wa ununuzi wa magari ya Serikali yakiwemo ya wakurugenzi. Je, kwa mfumo wa Sasa ambao fedha zote zipo hazina na huduma nyingi zinalipwa kwa control number, Mkurugenzi alinunua gari bila Hazina kushirikishwa? Je, kama walishirikishwa walipitisha vipi Kibali ambacho kipo kinyume na circula ya serikali? Kwanini wote waliokula mchongo wakuingizia Serikali hasara wasitumbuliwe?
Nadhani Mhe. Jafo tume yako ipe adidu za rejea, moja ya adidu za rejea iwe "kupitia mchakato mzima wa ununuzi wa gari ilo" then wakikuletea ripoti isome public tujifunze mchakato wa manunuzi tujue kama tatizo lipo kwa Mkurugenzi au lipo kwenye mfumo wa manunuzi ili marekebisho yafanyike.
Hoja kuu inatokana na kile kinachoelezwa kuwa V8 si anasa kwa wakurugenzi na wamekuwa wakitumia gari hizi kwa miaka kadhaa sasa.
Hi hoja ilipowasilishwa Bungeni wakati wa Spika Makinda ilizua mjadala mkali sana na Serikali ikaazimia kutafuta magari ya bei ya chini lakini baadhi ya mabeberu weusi wakakataa wakidai Mkurugenzi lazima awe na gari la hadhi yake.
Maisha yameenda kasi na karibia viongozi wote waandamizi wa nchi hii wanatumia v8 na mashangingi mengine ya kifahari. Hivyo Mkurugenzi wa Geita amefuata nyayo tu.
Jambo linalozua mtafaruku ni kuhusu utaratibu wa ununuzi wa magari ya Serikali yakiwemo ya wakurugenzi. Je, kwa mfumo wa Sasa ambao fedha zote zipo hazina na huduma nyingi zinalipwa kwa control number, Mkurugenzi alinunua gari bila Hazina kushirikishwa? Je, kama walishirikishwa walipitisha vipi Kibali ambacho kipo kinyume na circula ya serikali? Kwanini wote waliokula mchongo wakuingizia Serikali hasara wasitumbuliwe?
Nadhani Mhe. Jafo tume yako ipe adidu za rejea, moja ya adidu za rejea iwe "kupitia mchakato mzima wa ununuzi wa gari ilo" then wakikuletea ripoti isome public tujifunze mchakato wa manunuzi tujue kama tatizo lipo kwa Mkurugenzi au lipo kwenye mfumo wa manunuzi ili marekebisho yafanyike.