Tujadili kuhusu "VAT"

Tayari raia wanaojua kutetea mifumo ya udhulumishi wamefika kutetea huu ubadhilifu.......kama ninachokisema si sahihi......ni kwanini mabenki yamekatazwa kuwatoza wateja ongezeko la VAT ili wao waikwepe........tumia akili nyepesi tu utapata majibu.......usipende kujiaminisha upo sahihi kwa kutumia ushahidi wa vitu vinavyoendelea kimakosa........

Mfano mdogo ni hata rushwa kuna watu wameklemisha kuwa unapifanya kosa la balabalani basi ni utaratibu kumpatia trafiki kitu kidogo wakati kiuhalisia hilo ni kosa lakufungwa kabisa ila kuna watu huwa wanaona hii ni halali na ni haki kufanya.
 
Mimi nakubaliana na ii kitu kua anaekuuzia ndio anaetakiwa kulipa io kodi
Mfano hai:Mim niliwai kwenda duka moja pale k koo kununua bidhaa mbali mbali ni kama taa flani za mapambo thamani ya zile bidhaa ilikua ni kama elfu 80 yule muuzaji wakati anataka kunipa risit akaniomba anikatie ya njiani MEANs anikatie risit kwa kuandika bei ya chini sana kuliko bei halisi ya bidhaa nilizochukua
 
Neno VAT ni neno la kiuchumi au la kibiashara la lugha ya kiingereza(english) ikiwa ni ufupisho wa maneno "VALUE ADDED TAX yaani kwa kiswahili ni kodi ya ongezeko la thamani.

VAT ni aina ya kodi ambayo hutozwa kwenye mapato yatokanayo na mauzo ya bidhaa ya aina yeyote kubwa kwa ndogo lakini pia kwa malipo ya huduma zozote! Kwa kifupi ni kiasi ambacho hutozwa kwa muamala wowote na hutozwa kwa yule anayepokea tu na si mtoaji.

Kwa muda mrefu serikali yetu imekuwa ikichaji aina hii ya kodi kwenye malipo yanayofanyika katika manunuzi ya bidhaa na huduma hapa nchini(si mauzo yote hufanikiwa kuchajiwa kwasababu ya ukwepaji kodi na mifumo isiyokidhi mahitaji pamoja na biashara nyingi kutokuwa rasmi).
Aina hii ya kodi hukadiriwa kulingana naongezeko la thamani au kushuka kwa thamani ya bidhaa au huduma usika.......tafsiri yake ni kuwa kama bidhaa au huduma itapanda au kushuka bei then kiwango cha kodi inayochajiwa nacho kitapanda au kushuka kulingana na asilimia ambayo hutozwa.....( kwasasa ni asilimia 18).

Kuna kasumba ambayo imejengeka katika akili za watanzania (wasomi na hata wasio wasomi) kuwa tozo la kodi ya V.A.T huwa inatakiwa kulipwa na mnunuaji wa bidhaa pale anapokwenda dukani kwamaana ya kwamba hii kodi tokea bidhaa ina nunuliwa basi kila anayeuza hii bidhaa humtupia mzigo wa kulipa anayeishia wa mwisho kitu ambacho si sahihi. Ntakupa mfano ili unielewe vema.......

Mfano:

Tutachukulia kiwango cha VAT ni asilimia kumi (10%) ili kurahisisha mahesabu........ila kiwango halisi cha VAT kwa sasa ni asilimia kumi na nane (18%).


mfano, bakhresa anazalisha juice ya azam mango
Juice hii hutengenezwa na maembe. Bakhresa anakwenda shambani kwa mkulima ambaye tutachukulia anamiembe ambayo ni ya asili hivyo hakuna gharama yeyote ya uzalishaji hapo ila tu ameisimamia miembe yake imekuwa na imezaa kwahiyo pesa ya kwanza katika hii scenario ni wakati bakhresa analipia maembe kwaajiri ya kupeleka kiwandani kwake kwaajiri ya kukamua juice.

Tuchukulie bakhresa amechukua tani 10 ambazo ni kwa ujumla wake amemlipa mkulima shilingi laki mbili (200,000/=). Sasa hapa ndio habari ya VAT huanza........kwa maana huu ni muamala wa kwanza wa malipo ya kifedha unafanyika kutoka kwa bakhressa kwenda kwa mkulima. Hivyo basi.....mkulima hypothetically anatakiwa kuwa na ile mashine na TRA ili amuandikie risiti bakhresa na kuwapatia serikali kupitia wakala wake (TRA) mapato yao ya asilimia kumi (10%) kodi ya tozo la ongezeko la thamani kutoka sifuri (0) hadi laki mbili (200,000) ambayo itakuwa ni shilingi elfu ishirini (20,000). Hivyo basi bakhresa hatotakiwa kulipa zaidi ya 200,000/= kwa mkulima na hatolipa chochote kwa serikali maana yeye hajapokea chochote ila ametoa. Mkulima atatakiwa kubaki na 180,000/= baada ya kutoa 20,000/= ya VAT.

Bakhressa atasafirisha huu mzigo kwenda kiwandani kwake kwakutumia fuso ya mtu binafsi anaetoa huduma hiyo.......tuchukulie atalipia 30,000 kama gharama ya usafiri. Pia huyu msafirishaji anatakiwa kuwa na Kifaa cha risiti cha tra ili aweze kulipa vat kila wakati mtu anapofanya malipo kwake. Hivyo basi katika hatua hii pia msafirishaji atatakiwa kulipa 10% ya 30,000 kama VAT bakhressa hatalipia zaidi ya 30,000 na VAT haimuhusu maana hajapokea ametoa.
Baada ya mzigo kufika kiwandani bakressa ataanza kutengeneza juice yake.......tuchukulie kwamba maembe yanatoa juice nyingi kiasi kwamba anaweza kupanga bei ya sh.2500/= kwenda kwa muuzaji wa jumla shilingi 2000 /= ni kufidia gharama alizoingiza na 500 ni faida kwaajiri yake.

Tuchukulie Mangi mwenye duka la jumla amekuja kununua boksi 100 za juice ya bakhressa ambazo zitamgharimu sh. 250,000/= .....bakhressa atatakiwa kulipa VAT kwasababu katika muamala huu yeye ndiye anapokea Mangi hatotakiwa kulipa zaidi ya 250,000/= kwa bakhressa ili kupata hizo boksi 100.
Hivyo basi bakhressa atapokea sh. 250,000/= na atakata VAT ambayo ni 10% ya 250,000/= ambayo ni sh.25,000/= iende serikalini na yeye atabaki na 225,000/=.

Mangi atakwenda na mzigo dukani kwake ili akauze reja reja kwa wauzaji wa reja reja. Mangi atalipia usafiri wa bajaji kubeba hizi boksi 100. Tufanye bajaji ni sh.5000/=. Huyu jamaa wa bajaji anatakiwa kuwa na kile kifaa cha TRA pia ili alipe kodi. Hivyo tuchukulie anacho hivyo basi atalipa vat pia 10% ya sh.5000/= ambayo ni shiling 500/= Mangi hatolipia chochote zaidi ya 5000 hapa........
Mzigo utafika dukani kwa Mangi tayari kwaajiri ya mauzo. Mangi atauza kila boksi kumi kwa bei ya sh. 3000 kila boksi hivyo bei yake ya jumla ni sh. 30,000/=.
Muuzaji wa rejareja anayeutwa Faki atakwenda dukani kwa Mangi kununua mzigo wake ili apeleke dukani kwake kuuza reja reja.
Faki atamlipa Mangi shilingi 30,000 kwa boski kumi. Faki hatolipia VAT hapa na hatomlipa Mangi zaidi ya sh. 30,000/= .......Mangi atakiwa anatakiwa ampe Faki risiti ya TRA kutoka katika kifaa cha tra ambayo itaonyesha kuwa amelipia VAT (10% ya sh. 30,000/=) ambayo ni sh. 3000/= kwenda serikilini kupitia TRA.
Faki atakwenda na hii bidhaa dukani kwake ili akauze reja reja kwa boksi moja moja kwa mtumiaji wa mwisho ambaye ni mimi au wewe.
Faki atapanda Boda boda pia atalipia gharama ya sh. 3000/=. Boda boda atatakiwa ampatie risiti ya TRA Faki kwa malipo yaliyofanyika ambapo bodaboda atalipia VAT kwa serikali kupitia kifaa cha TRA(Tanzania bado havijaletwa ila tunatakiwa kuwa navyo) boda boda atalipa sh.300/= kwenda serikalini kupitia TRA.Faki hatolipia VAT hapa na hatolipia zaidi ya sh.3000/= kwaajiri ya gharama za usafiri.

Faki atafika dukani pake na kuweka maboksi ya juice tayari kwa kuuza.
Mimi nitakwenda dukani kwa faki kununua juice boksi moja.
Faki anauza boksi moja ya juice kwa bei ya sh.3500/=. Mimi nitanunua hii box kwa shilingi 3500/= hiyo hiyo. Faki atalipia VAT 10% ya 3500/=ambayo ni 350/= iende serikalini kupitia tra.
Mimi hapa sitotakiwa kulipia zaidi ya sh.3500/= na sitolipia VAT kamwe kwasababu nimelipia na sitauza ninakwenda kuitumia hii juice. Hapa ndipo kodi aina ya Vat hukomea kwa muuzaji wa mwisho.

Kama umefuatilia vizuri huo mtiririko basi utakuwa umejifunza mambo mengi kuhusu VAT. Mojawapo ni kuwa....
(1)VAT hailipwi na anayenunua bidhaa au huduma ila anayeuza ndiye hulipa..

(2)Vat huchajiwa kama tozo ya ongezeko la thamani na hivyo basi huchatozwa pale tu ambapo kuna muamala mpya unafanyika yaani mauziano mapya.

(3)VAT kwa tanzania kiuhalisia tofauti na kwenye mfano hapo juu huwa inarushwa au hukwepwa na wanaouza bidhaa au huduma kwa kuificha ndani ya bei wanayokupa na ukiwahoji wanakwambia vat imepanda ndio maana na bei imepanda .....hili ni kosa kubwa kisheria na wengi huwa wanalifanya wakijua ni haki yao kumbe si halali hata kidogo kwa wao kulipa vat halafu ile vat wanairudisha kijanja kwenye bei ya vitu wanavyouza au huduma
mfano
hapo faki angeniuzia mimi juice kwa bei ya sh. 3,850/= badala ya 3500 ili ndani ya hiyo bei akwepe Kodi ya ongezeko la thamani yaani VAT nimlipie mimi.



Nakaribisha maswali.........uchangiaji........na pia nyongeza kama kuna kitu kimepungua au hakipo sawa.
Yaani mkuu umechanganya madawa ile mbaya!!utaratibu wa VAT hauko hivyo kabisa!!kwanza elewa kuwa kuna sifa maalum kwa mfanyabiashara kuwa mkusanya ji wa kodi ya ongezeko la thamani,si kila mfanyabiashara ana sifa hiyo,na yeye anakusanya hiyo kodi kwa niaba ya serikali kutoka kwa mtumiaji,na baada ya kupeleka returns zake kila mwezi wanaangalia mauzo ghafi na manunuzi yake,ndio wanajua kama unadaiwa au unadai,na sio kila bidhaa mfano maembe hayatozwi vat.ni somo kubwa sana,Ila wewe umechemka sana na hata kwenye kukokotoa VAt ni tofauti kabisa na unavyofanya eti kama vat ni 10% mfano wa 30000 ni elfu 3000???mkuu unachekesha hii ni fani ya watu sio unavyofikiria..Rudi darasni upate mwanga japo kidogo.
 
Mtoa mada mfanyabiashara ni TAX COLLECTOR anakusanya kodi kwa niaba ya TRA , kama umefanya biashara au umejaza tender yoyote au quotation lazima kuna kipengele cha Add 18% VAT so usipotoshe uma.
Na pia mfanyabiashara nae pia analipa VAT anapoenda kununua malighafi so Bakhresa akienda kununua maembe shambani ni bakhresa ndie anaelipa kodi yule mkulima anaipeleka TRA na vivyo hivyo Mangi akienda kununua juice kwa bakhresa ni Mangi anayelipa hiyo VAT na sio bakhresa tena anachofanya mfanyabiashara ni Ku add 18% VAT
Yaaninhuyo jamaa hana analojua juu ya VAT kabisa,hata kukokotoa vat tu hajui anadhani ni suala tu la kuchukua mfano asilimia 10 ya 30,000 ni 3000!!!ndio vat ina kokotolewa hivyo??
 
umenierimisha sana mkuu .kumbe benki wanataka kutuibia kwa kuongeza bei ya kutumia atm kwa mteja wakati ni wajib na jukumu lao .
Jamaa amewalisha matango poli ile mbaya,hajui anachokielezea,mfumo wa VAT hauko hivyo kabisa,bei ya bidhaa au huduma unayonunua inakuwa na kodi ya ongezeko la thamani humo humo,yule muuzaji kama amesajiliwa na VAT yeye anakuwa ni mkusanyaji tu wa kodi hiyo kwa niaba ya serikali na kila mwisho wa mwezi anatakiwa kupeleka returns zake,,ambazo na yeye atatakiwa kuonyesha mauzo yake ghafi,ambayo ndio hayo aliyowauzia nyie na manunuzi yake aliyofanya,ndio wataangalia kama mauzo yake yanazidi manunuzi atapaswa kulipia hiyo tofauti,ila kama manunuzinyake ni makubwa kuliko mauzo ya mwezi husika atarejeshewa pesa iliyozidi,japo sio cash kabisa itabaki huko ila kama return yake ya mwezi unaofuata atadaiwa itapunguzwa kwenye hiyo credit balance yake,kwanza aelewe kuwa kila mfanyabiashara lazima awe na TIN(tax identification number)ila si kila mfanyabiashara lazima awe registered na VAT.
 
Neno VAT ni neno la kiuchumi au la kibiashara la lugha ya kiingereza(english) ikiwa ni ufupisho wa maneno "VALUE ADDED TAX yaani kwa kiswahili ni kodi ya ongezeko la thamani.

VAT ni aina ya kodi ambayo hutozwa kwenye mapato yatokanayo na mauzo ya bidhaa ya aina yeyote kubwa kwa ndogo lakini pia kwa malipo ya huduma zozote! Kwa kifupi ni kiasi ambacho hutozwa kwa muamala wowote na hutozwa kwa yule anayepokea tu na si mtoaji.

Kwa muda mrefu serikali yetu imekuwa ikichaji aina hii ya kodi kwenye malipo yanayofanyika katika manunuzi ya bidhaa na huduma hapa nchini(si mauzo yote hufanikiwa kuchajiwa kwasababu ya ukwepaji kodi na mifumo isiyokidhi mahitaji pamoja na biashara nyingi kutokuwa rasmi).
Aina hii ya kodi hukadiriwa kulingana naongezeko la thamani au kushuka kwa thamani ya bidhaa au huduma usika.......tafsiri yake ni kuwa kama bidhaa au huduma itapanda au kushuka bei then kiwango cha kodi inayochajiwa nacho kitapanda au kushuka kulingana na asilimia ambayo hutozwa.....( kwasasa ni asilimia 18).

Kuna kasumba ambayo imejengeka katika akili za watanzania (wasomi na hata wasio wasomi) kuwa tozo la kodi ya V.A.T huwa inatakiwa kulipwa na mnunuaji wa bidhaa pale anapokwenda dukani kwamaana ya kwamba hii kodi tokea bidhaa ina nunuliwa basi kila anayeuza hii bidhaa humtupia mzigo wa kulipa anayeishia wa mwisho kitu ambacho si sahihi. Ntakupa mfano ili unielewe vema.......

Mfano:

Tutachukulia kiwango cha VAT ni asilimia kumi (10%) ili kurahisisha mahesabu........ila kiwango halisi cha VAT kwa sasa ni asilimia kumi na nane (18%).


mfano, bakhresa anazalisha juice ya azam mango
Juice hii hutengenezwa na maembe. Bakhresa anakwenda shambani kwa mkulima ambaye tutachukulia anamiembe ambayo ni ya asili hivyo hakuna gharama yeyote ya uzalishaji hapo ila tu ameisimamia miembe yake imekuwa na imezaa kwahiyo pesa ya kwanza katika hii scenario ni wakati bakhresa analipia maembe kwaajiri ya kupeleka kiwandani kwake kwaajiri ya kukamua juice.

Tuchukulie bakhresa amechukua tani 10 ambazo ni kwa ujumla wake amemlipa mkulima shilingi laki mbili (200,000/=). Sasa hapa ndio habari ya VAT huanza........kwa maana huu ni muamala wa kwanza wa malipo ya kifedha unafanyika kutoka kwa bakhressa kwenda kwa mkulima. Hivyo basi.....mkulima hypothetically anatakiwa kuwa na ile mashine na TRA ili amuandikie risiti bakhresa na kuwapatia serikali kupitia wakala wake (TRA) mapato yao ya asilimia kumi (10%) kodi ya tozo la ongezeko la thamani kutoka sifuri (0) hadi laki mbili (200,000) ambayo itakuwa ni shilingi elfu ishirini (20,000). Hivyo basi bakhresa hatotakiwa kulipa zaidi ya 200,000/= kwa mkulima na hatolipa chochote kwa serikali maana yeye hajapokea chochote ila ametoa. Mkulima atatakiwa kubaki na 180,000/= baada ya kutoa 20,000/= ya VAT.

Bakhressa atasafirisha huu mzigo kwenda kiwandani kwake kwakutumia fuso ya mtu binafsi anaetoa huduma hiyo.......tuchukulie atalipia 30,000 kama gharama ya usafiri. Pia huyu msafirishaji anatakiwa kuwa na Kifaa cha risiti cha tra ili aweze kulipa vat kila wakati mtu anapofanya malipo kwake. Hivyo basi katika hatua hii pia msafirishaji atatakiwa kulipa 10% ya 30,000 kama VAT bakhressa hatalipia zaidi ya 30,000 na VAT haimuhusu maana hajapokea ametoa.
Baada ya mzigo kufika kiwandani bakressa ataanza kutengeneza juice yake.......tuchukulie kwamba maembe yanatoa juice nyingi kiasi kwamba anaweza kupanga bei ya sh.2500/= kwenda kwa muuzaji wa jumla shilingi 2000 /= ni kufidia gharama alizoingiza na 500 ni faida kwaajiri yake.

Tuchukulie Mangi mwenye duka la jumla amekuja kununua boksi 100 za juice ya bakhressa ambazo zitamgharimu sh. 250,000/= .....bakhressa atatakiwa kulipa VAT kwasababu katika muamala huu yeye ndiye anapokea Mangi hatotakiwa kulipa zaidi ya 250,000/= kwa bakhressa ili kupata hizo boksi 100.
Hivyo basi bakhressa atapokea sh. 250,000/= na atakata VAT ambayo ni 10% ya 250,000/= ambayo ni sh.25,000/= iende serikalini na yeye atabaki na 225,000/=.

Mangi atakwenda na mzigo dukani kwake ili akauze reja reja kwa wauzaji wa reja reja. Mangi atalipia usafiri wa bajaji kubeba hizi boksi 100. Tufanye bajaji ni sh.5000/=. Huyu jamaa wa bajaji anatakiwa kuwa na kile kifaa cha TRA pia ili alipe kodi. Hivyo tuchukulie anacho hivyo basi atalipa vat pia 10% ya sh.5000/= ambayo ni shiling 500/= Mangi hatolipia chochote zaidi ya 5000 hapa........
Mzigo utafika dukani kwa Mangi tayari kwaajiri ya mauzo. Mangi atauza kila boksi kumi kwa bei ya sh. 3000 kila boksi hivyo bei yake ya jumla ni sh. 30,000/=.
Muuzaji wa rejareja anayeutwa Faki atakwenda dukani kwa Mangi kununua mzigo wake ili apeleke dukani kwake kuuza reja reja.
Faki atamlipa Mangi shilingi 30,000 kwa boski kumi. Faki hatolipia VAT hapa na hatomlipa Mangi zaidi ya sh. 30,000/= .......Mangi atakiwa anatakiwa ampe Faki risiti ya TRA kutoka katika kifaa cha tra ambayo itaonyesha kuwa amelipia VAT (10% ya sh. 30,000/=) ambayo ni sh. 3000/= kwenda serikilini kupitia TRA.
Faki atakwenda na hii bidhaa dukani kwake ili akauze reja reja kwa boksi moja moja kwa mtumiaji wa mwisho ambaye ni mimi au wewe.
Faki atapanda Boda boda pia atalipia gharama ya sh. 3000/=. Boda boda atatakiwa ampatie risiti ya TRA Faki kwa malipo yaliyofanyika ambapo bodaboda atalipia VAT kwa serikali kupitia kifaa cha TRA(Tanzania bado havijaletwa ila tunatakiwa kuwa navyo) boda boda atalipa sh.300/= kwenda serikalini kupitia TRA.Faki hatolipia VAT hapa na hatolipia zaidi ya sh.3000/= kwaajiri ya gharama za usafiri.

Faki atafika dukani pake na kuweka maboksi ya juice tayari kwa kuuza.
Mimi nitakwenda dukani kwa faki kununua juice boksi moja.
Faki anauza boksi moja ya juice kwa bei ya sh.3500/=. Mimi nitanunua hii box kwa shilingi 3500/= hiyo hiyo. Faki atalipia VAT 10% ya 3500/=ambayo ni 350/= iende serikalini kupitia tra.
Mimi hapa sitotakiwa kulipia zaidi ya sh.3500/= na sitolipia VAT kamwe kwasababu nimelipia na sitauza ninakwenda kuitumia hii juice. Hapa ndipo kodi aina ya Vat hukomea kwa muuzaji wa mwisho.

Kama umefuatilia vizuri huo mtiririko basi utakuwa umejifunza mambo mengi kuhusu VAT. Mojawapo ni kuwa....
(1)VAT hailipwi na anayenunua bidhaa au huduma ila anayeuza ndiye hulipa..

(2)Vat huchajiwa kama tozo ya ongezeko la thamani na hivyo basi huchatozwa pale tu ambapo kuna muamala mpya unafanyika yaani mauziano mapya.

(3)VAT kwa tanzania kiuhalisia tofauti na kwenye mfano hapo juu huwa inarushwa au hukwepwa na wanaouza bidhaa au huduma kwa kuificha ndani ya bei wanayokupa na ukiwahoji wanakwambia vat imepanda ndio maana na bei imepanda .....hili ni kosa kubwa kisheria na wengi huwa wanalifanya wakijua ni haki yao kumbe si halali hata kidogo kwa wao kulipa vat halafu ile vat wanairudisha kijanja kwenye bei ya vitu wanavyouza au huduma
mfano
hapo faki angeniuzia mimi juice kwa bei ya sh. 3,850/= badala ya 3500 ili ndani ya hiyo bei akwepe Kodi ya ongezeko la thamani yaani VAT nimlipie mimi.



Nakaribisha maswali.........uchangiaji........na pia nyongeza kama kuna kitu kimepungua au hakipo sawa.

Kwakudanganya kwa makusudi au kwakutojuwa jinsi ya VAT inavyofanyakazi nineamua kukupa LIKE.

Yaani katika mfano wako wa maembe unadanganya kwamba VAT ni punguzo la kiasi anachopokea muuzaji kwa asilimia zilizopangwa na serikali. Kwamba kama embe ziliuzwa sh 30,000 mnunuzi hatalipa zaidi ya sh 30,000 bali muuzaji atabakiwa na kiasi pungufu ya sh 30,000. Nikufungue macho; kodi katika bidhaa inaongeza bei ya bidhaa hiyo na ongezeko hilo ndilo linalokwenda serikalini. Hivyo basi, Baresa atauza juice yake kwa sh 30,000 (hiki nikiasi kinachompa yeye faida au aka break even na kamwe hatapunguza 10% iende serikalini), juu ya hapo ndipo atamwongezea mnunuzi kwa 10% na hivyo kumfanya mnunuzi alipe sh30,000 plus ongezeko la 10% ambapo jumla itakuwa sh 33,000. Hapo sasa Baressa atapeleka sh 3,000 serikalini.

Mkuu rudi darasani tena, na kama huna uhakika wa unachokisema tafadhali usichangie mada za kisomi maana kwa kufanya hivyo unapotosha wanafunzi wanaosoma hapa na kujifunza.
 
uzi wa upotoshaji huuu.

What is your aim mtoa mada, kuwafanya watanzania wajinga zaidi badala ya kuwaelimisha.

Au kwasbabu unajua ni wavivu wa kusoma na kujitafutia ukweli ndo maana unawaambia vitu vya upotoshaji namna hii??

Bila kukuchosha kuleta reference hapa, embu nenda kwenye google type neno V. A. T halafu ndo ujue maana yake nini na burden ya kulipa mwisho wa siku inaangukia kwa nani.

Kwa definition ndogo ya kukusaidia, angalia definition ya V. A. T kutoka mamlaka ya kodiView attachment 362597
Mkuu... huyu jamaa nadhani ana lengo la kuwafanya watu wawe wajinga zaidi... sijui ana lengo gani. .. au labda naye hajui maana ya VAT...
 
Walioko TRA au wachumi

Please explain VAT on Tourism

And Tourists are consumers and pays VAT

Sasa marejesho yanakuwaje kwa Tourists? TRA na Wizara ya Fedha mmejipanga?

Why Do Government charges VAT on its own money/revenue? - (Park entry fees) What is aim?
 
Maelezo ni mazuri sana na huenda yakashabihiana na mipango mizuri pamoja na taarifa zilizomo kwenye makabati ya wizara na taasisi zetu. Lakini alichoambatanisha mpiga domo kinaendana tofauti na uhalisia huu.
Ngoja nifuatilie katika nchi zingine kujua utofauti na ukweli lakini Tanzania kila kitu huenda kinyume nyume na dio maana RPC 'anavunja tamko la polisi' la kuzuia mikutano na mikusanyiko ya kisiasa!
 
Mtu aliyepata maendeleo kuliko wewe ni vizuri kuiga mfano wake.....

Japan imefanya mapinduzi ya Viwanda na kutengeneza magari miaka ya 70s/80s......Japan waliiga UK, Italy, France, German....
Hata USA waliiga Europe na Israel kutengeneza Cardilac na Hummer

So Japan ni koloni la Europe?????

Kenya wametuzidi kiuchumi na viwanda.... Bidhaa za Kenya ni bora sana....Tujilinganishe

South Africa, Botswana, Mauritious, Namibia.....

Is Tanzania only wildlife safari destination?

Au Mlima Kilimanjaro?

Who know Table Mountain

Drakensberg?
 
Pengine asilimia 18 kwa bidhaa na huduma ni kubwa mno kwa ujumla wake kutokana na utafaouti wa bidhaa na huduma, na umuhimu wake kwa jamii.

TRA wangeweka unafuu wa asilimia kwa mahitaji muhimu kama vile madawa na huduma za hospitalini, na kwenye usafiri wa mabasi, hali kadhalika katika vyakula.
 
kwa wale wenye kujitoa fahamu (sisi.....) na viongozi wake sijui kama watakuelewa labda
upload_2016-7-4_12-25-54.png
amuunge mkono mtoa mada
 
swali...mbona ukienda nunua UMEME au MAJI. tunalipa na VAT wakati kwa elim yako hiyo aliepaswa kulipa vat ni tanesco au idara ya maji...lakin nakuta kwenye risiti nalipia na VAT?
 
Sasa hapa ndio watanzania mjue kuwa wanaotufilisi hii nchi ni wasomi na masomo yao kuklemisha na si mataifa ya nje.............mimi hapo nimeonyesha mfumo ambao VAT inatakiwa kuwa na serikali iweze kupata mapato yake inavyotakiwa......na nikaandika kabisa kuwa huo ni mfano........na hata hivyo namna serikali wanavyokokotoa VAT si kama hapo juu maana hata ningekuwa sijui chochote ningeenda online halafu ningekuja kupaste tu vitu nilivyosoma...........lakini nilichofanya hapo ni kutoa namna ambayo ingekuwa nzuri ya kukusanya kodi ya serikali........

Ila tatizo ni kuwa wasomi wengi tanzania wapo vizuri kwenye kumeza vitu kama vilivyo bila kuvitoa dosari...........iwe ni mambo ya benki upande wa riba na makato au inshu za kodi kama hivi........hili taifa linahitaji wasomi ambao wanahoji mifumo na sio watu wanaokwenda shule wanajua tu kumeza hesabu halafu wanakuja kutumia walichojifunza kurudusha taifa nyuma kwa kuwanyonya wananchi kupitia mifumo ambayo sio rafiki kwa maendeleo ya wananchi achilia mbali ya taifa.............

So kwa wale ambao mnasema nilichosema sio kitu cha kueleweka wekeni mfumo halisi wa VAT halafu mtaona kama kuna mjumbe atawaelewa au ataona tija ya huo mfumo halisi.........



Ifike wakati wasomi tuwe watu wa kuhoji mifumo ambayo haitusaidii kuleta maendeleo.......leo hii raia wa kawaida kwanza hata haelewi nini maana ya kodi maana hajui inamaana gani zaidi anahofia itamzulumu........


WITH MY SOCIETY I STAND.
 
mtoa mada maneno mengi na mifano mingi yako ipo kimtizamo ila uhalisia vat analipa mtumiaji wa mwisho na ndyo maana kwenye hyo vat mzigo wote anabeba mtumiaji wa mwisho.japo ipo kwa kila hatua ila mfanyabiashara anaisaidia serikali kukusanya toka kwa mlaji wa mwisho na yeye ndye most affected.hvyo hizi taasisi za fedha zinaisaidia tu serikali kupata kodi yake kutoka kwa maskini mtumiaji wa mwisho.hyo ya mtoa mada ni mfumo wake ambao naona anaishauri serikali.bt kwa tz na jinsi vat ilivyo mzigo upo huku kwetu na c kwa mfanyabiashara wa taasisi za fedha.mtoa mada yupo kinadharia zaidi.
 
T
Kwakudanganya kwa makusudi au kwakutojuwa jinsi ya VAT inavyofanyakazi nineamua kukupa LIKE.

Yaani katika mfano wako wa maembe unadanganya kwamba VAT ni punguzo la kiasi anachopokea muuzaji kwa asilimia zilizopangwa na serikali. Kwamba kama embe ziliuzwa sh 30,000 mnunuzi hatalipa zaidi ya sh 30,000 bali muuzaji atabakiwa na kiasi pungufu ya sh 30,000. Nikufungue macho; kodi katika bidhaa inaongeza bei ya bidhaa hiyo na ongezeko hilo ndilo linalokwenda serikalini. Hivyo basi, Baresa atauza juice yake kwa sh 30,000 (hiki nikiasi kinachompa yeye faida au aka break even na kamwe hatapunguza 10% iende serikalini), juu ya hapo ndipo atamwongezea mnunuzi kwa 10% na hivyo kumfanya mnunuzi alipe sh30,000 plus ongezeko la 10% ambapo jumla itakuwa sh 33,000. Hapo sasa Baressa atapeleka sh 3,000 serikalini.

Mkuu rudi darasani tena, na kama huna uhakika wa unachokisema tafadhali usichangie mada za kisomi maana kwa kufanya hivyo unapotosha wanafunzi wanaosoma hapa na kujifunza.
Tofauti yako na mtoa mada ni ipi hapo. Kabla haujakosoa soma ukaelewa. Muuzaji si lazima amwambie mnunuaji kwamba laki mbili na vat, maana ya mtoa mada ni kwamba wewe piga faida zako then ongeza vat kisha ndio muuzie mnunuzi.
 
Hii ndio maana ya vat sijui huyo jamaa kaitoa wapi maana yake. Vat ni value added tax kwa maana kuwa ni kodi juu ya thamani ya kitu au huduma.
Huyu Killaza wetu kaja kudanganya watu humu! sasa mamuma wengine wako wanasema et wameelewa somo! hawaendi hata kwenye supermarket zetu waone kwenye receipt wajue ni nani kalipa VAT kati ya muuzaji na mnunuaji!!!!!
Anayenunua ndo anayelipa VAT!!!! Toa mifano yako lukuki lkn ukweli ni huo, na kama sivyo hatuna serikal maana raia watakuwa walishaibiwa tangu Vat imeanzishwa!!!!!!
 
Back
Top Bottom