Tujadili: Dunia ya machale!!!!!!!!

Kaunga

JF-Expert Member
Joined
Nov 28, 2010
Posts
12,529
Reaction score
13,501
Kuishi kwa machale
Kuongea kwa machale
Kupenda kwa machale
Urafiki wa machale
Ushirika (biashara) wa machale
Undugu wa machale
Kanisani machale
Misikitini machale
Kazini machale
Kwenye familia machale
Kwenye ndoa machale​
Najua ni ngumu kumuamini kila mtu, lakini naona maisha ni magumu sana kwa kutomuamini mtu yoyote. Katika ndoa kila mtu anamtegea mwenzie, yaani hata kuufungua moyo wako kwa mpenzio unaogopa kwa kuhisi tu mwenzio atauexploit na kukuumiza. Where is the trust?

Kwenye masuala ya mali ndio kabisa, kila mtu anatoa ukweli nusu au hata pengine robo hii ni hatari sana kwa maoni yangu. Matokeo yake tunakuwa wapweke sana kwa kuwa tuna siri nyingi sana ambazo hatuzishei; licha ya upotevu wa mali unaotokea pindi mmiliki wa siri anapotangulia.

Labda swali la kujiuliza hapa, chanzo cha kuishi kimachale au kuangalia kila kitu kwa jicho la tatu if you may ni nini? Ni kujifunza kutoka kwa makosa ya wengine? je mazingira ya kutokea kwa hayo makosa ya wengine ni the same? Au waliokosea wanafanana na hawa wenzi wetu kwa kila kitu?

Wana jamvi kuna shida gani ukimuamini mtu?

Karibuni tujadili.
 
Nafikiri chanzo cha kuishi kimachale ni hii dhana ambayo leo watu wengi wanayo,yaani dhana ya mimi,dhana hii imesababisha watu kuwa wanaojifikiria na kujiwazia wao tu hivi kwamba kufanya uhujuma au usaliti hata kuelekea watu wanaominiana nao sana limekuwa jambo la kawaida sana ili tu kutimiza dhana hiyo ya mimi nikale wapi?mimi nitafaidi lini?kwa nini yeye tu na sio mimi?na linapotokea jambo la usaliti kati ya watu wanaoamniana sana na watu katika jamii kushuhudia,wengi wao wenye kuweza kujifunza hujifunza kitu kuwa kama yule kafanyiwa hivyo mimi ni nani nisiweze kuja kufanyiwa hivyo na mtu nimwaminiye na kisha kuanza kuishi maisha ya machale pia.
 

Aisee, hivyo ubinafsi huchangia sana kushindwa kuwaamini wengine eeh.
Nafikiri pia watu hutafsiri udhaifu au upungufu wao kwa watu wengine; mfano, kama mimi sio mwaminifu basi inakuwa ngumu kuamini kuwa kuna watu waaminifu. Unaionaje hii?
 
KUJIAMINI!
KUAMINI!
KUMUAMINI!
...
Kujiamini ndio kitu cha msingi! Coz you have a TOTAL CONTROL upon this!
...
Kuamini: ni muhimu sana! Hapa as a reasonable man/person, You ought to foresee the possibility of something due to the facts and evidence!
...
Kumuamini: inatakiwa umuamini kwa sababu na mifano! All in all hutakiwi kumuamini mtu YOYOTE kwa asilimia 100! Yap! Huna control ya kutosha kwa yeyote! When it comes to love, hata mtu aweje hakuna kumuamini kwa asilimia zote but kumuonesha kama humuamini haitakiwi ikiwa huna sababu na direct examples to him/her!
Human being are SELFISH IN NATURE!
...
Nadhani nimesoumeka hapo!
 
Aisee, hivyo ubinafsi huchangia sana kushindwa kuwaamini wengine eeh.
Nafikiri pia watu hutafsiri udhaifu au upungufu wao kwa watu wengine; mfano, kama mimi sio mwaminifu basi inakuwa ngumu kuamini kuwa kuna watu waaminifu. Unaionaje hii?
Ndiyo hiyo pia ni sababu mojawapo na ndio maana hata imezoeleka kuwa ukikuta mume au mke ana wivu kupita basi ujue kuwa hata yeye si mwaminifu kwani atahisi anavyoiba nje ya ndoa mwenzie pia anafanya hivyo hivyo,the same to asiye mwaminifu kwa kila jambo ye pia ataona watu wote kuwa matraitors na hivyo kuishi kwa machale hata zaidi.
 
Wakati mwingine kuishi kwa "machale" husababishwa na tabia ya ubinafsi...

lakini vipi kuhusu madhara ya too much machale; yaani mimi naona unakosa amini hivi kwa muda wote kuhisi kila kitu kina motive behind au conspiracy fulani hivi.
 

waoh, nimependa sana ulivyonyambulisha vizuri. Thanks buddy!

Sasa kuhusu kutomuamini mtu 100%, je kwa mwenzi wako wa ndoa ni % ngapi za kumuamini zinazotakiwa? Na kuna shida gani nikimuamini 100% hata kama akinidisappoint si ni tatizo lake na sio langu. Tunapokuwa na reservation na wapenzi wetu huoni kama inatufanya tuzidi kuwa far apart?
 
i think selfishness,,, ila dont trust any body usijal may be that is better life.....
 
….umeniwahi na 'sredi' ya mawazo haya,
machale yanaweza kukuepusha na ile siku ya #40!

Siku ya Arobaini, au Arobaini yako ikifika, #Machale yatakucheza
tu kwamba mnh…leo!!!...

Hapana dharau #Machale aisee…ile ni 6th Sense!

 
lakini vipi kuhusu madhara ya too much machale; yaani mimi naona unakosa amini hivi kwa muda wote kuhisi kila kitu kina motive behind au conspiracy fulani hivi.
Kuwa na machale saa zote zinachangiwa na experience alizopitia mhusika mfano kusalitiwa mara tofauti na watu anaowaamini na kuwategemea na halii hujenga negativity na kumfanya mtu awe sceptical na kudoubt kila kitu...yaani mtu wa aina hio anakuwa hata mgumu kufunguka kwa watu ni mtu msiri ambaye ni watu wachache mno anaweza kuwaamini!Naweza kusema pia ni makuzi aliyopitia mfano kama kulikuwa hakuna uaminifu nyumbani usitegemee mtu huyo atamuamini mtu mwengine kirahisi ukubwani..
 
….umeniwahi na 'sredi' ya mawazo haya,
machale yanaweza kukuepusha na ile siku ya #40!

Siku ya Arobaini, au Arobaini yako ikifika, #Machale yatakucheza
tu kwamba mnh…leo!!!...

Hapana dharau #Machale aisee…ile ni 6th Sense!

Aisee, mimi naona ni kama kuwa paranoia fulani hivi when you live around too much machale. Usiniulize what is too much and what is too little; yaani kuna watu muda wote wanahisi kutendwa tu hawana amani kabisa, nilikuwa na jirani yangu yeye kila mtu au anamuhisi mchawi au kama ni mwanamke basi anamzengea mumewe. Honestly nilikuwa namuhurumia.
 
wanasema "i dont trust anybody thats why i can survive" but in practice a you must have someone where you can put all your faith(lean on) hapo ndipo tunapoumia na watu wengi wanapalalamikia
 

asante kwa mchango wako, it makes a lot of sense; lakini bado naona sio kitu kizuri sana kwa afya ya huyo mtu na pengine sio fair kwa wale watu ambao anapaswa kuwaamini. Is there anything which can be done ili aweze kuamini watu tena? au labda ni mimi tu ndio naona kama ni tatizo kutomuamini mtu hasa yule ambaye unapaswa kumuamini kama spouse vile.
 

Duu hii umenikumbusha kitu, kuna shemeji yangu (Mke wa kakaangu) ana kesi mahakamani lakini mmewe alikuwa hajui mpaka siku moja ilipotoka habari gazetini zile wanaziita 'kutoka mahakamani kwa ufupi', ishu ni kwamba alikuwa ananunua kiwanja kwa siri na ametapeliwa Tshs M26, wakati huo huo wanaishi kwenye nyumba ambayo haijafanyiwa finishing kutokana na familia kutokuwa na pesa.
 
wanasema "i dont trust anybody thats why i can survive"

mimi nasema, "the reason you are miserable is because you don't have anyone to trust"

(simaanishi wewe ofcourse)
 
lakini vipi kuhusu madhara ya too much machale; yaani mimi naona unakosa amini hivi kwa muda wote kuhisi kila kitu kina motive behind au conspiracy fulani hivi.

Ni kweli kuwa kila jambo likifanywa pasipo kiasi huwa na madhara ikiwemo hili la "machale"...machale yakizidi sana unakuwa kama mtumwa wa wasiwasi au hofu.

Wakati mwingine watu ambao muda wote hukosa imani kwa kudhani kuna hidden agenda au conspiracy fulani sio wa kuwashangaa, ukiacha walw wabinafsi baadhi huwa ni wahanga wa jambo walikwepalo na hufanya hivyo kujihami tu...

Kwani aliyeng'atwa na nyoka na akabahatika kupona, hukimbiza wake mguu hata akiguswa na unyasi wa kondeni...
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…