Mshana Jr
Platinum Member
- Aug 19, 2012
- 371,548
- 860,668
- Thread starter
- #41
VMstari upi? Au ndo nikasome agano lote?
Mit 31
Mafundisho ya Mama wa Mfalme Lemueli
1Maneno ya mfalme Lemueli; mausia aliyofundishwa na mama yake.
2Ni nini, mwanangu? Tena ni nini, mwana wa tumbo langu?
Tena, ni nini mwana wa nadhiri zangu?
3 Usiwape wanawake nguvu zako;
Wala moyo wako usiwape wale wawaharibuo wafalme.
4 Ee Lemueli, kunywa mvinyo hakuwafai wafalme, hakuwafai wafalme;
Wala haifai wakuu waseme, Ki wapi kileo?
5 Wasije wakanywa na kuisahau sheria,
Na kuipotosha hukumu ya mtu aliye taabuni.
6 Mpe kileo yeye aliye karibu na kupotea;
Kampe divai yeye aliye na uchungu nafsini.
7Anywe akausahau umaskini wake;
Asiikumbuke tena taabu yake.
8Fumbua kinywa chako kwa ajili yake aliye bubu;
Uwatetee watu wote walioachwa peke yao;
9 Fumbua kinywa chako, uhukumu kwa haki;
Uwapatie maskini na wahitaji haki yao.