Tuendelee na historia ya chama cha (A.A)

Magical power

JF-Expert Member
Sep 27, 2022
356
1,605
1686764217743.jpg
1686764220868.jpg

TUENDELEE NA HISTORIA YA CHAMA CHA (A.A).

Picha namba (1) inaonyesha jengo la ghorofa mbili lenye mistali ya rangi ya kijani na nyeupe, jengo hilo lilikuwa ni la chama cha African Association (A.A) alafu likatumiwa na TAA, alafu baadae TANU. Na pembeni yake kidogo kuna jengo la CCM.

Miaka ilivyozidi kusonga jengo la CCM likaunganishwa na jengo la A.A, baadae TAA, alafu TANU. Jengo hili lipo mtaa wa Lumumba na kariakoo Kama linavyoonekana hivi sasa katika muonekano mpya kwenye picha namba (2).

Kwanza tujiulize! Kleist Sykes haliupata wapi ujasili na moyo wa uzalendo wa kuwaamasisha marafiki zake kuunda chama cha African Association?

Ngoja nikuibie siri kidogo, ilikuwa mwanzoni mwaka miaka ya 1924, DR JAMES KWEGYIR AGGREY mwafrika kutoka GHANA kama anavyoonekana katika picha namba 3, ndiye aliye muamasisha Kleist Sykes kuingia kwenye siasa.

Ilikuaje? Ilikuwa hivi, Dr Aggrey alikuja Tanganyika mwaka 1924, kipindi icho alikua katika Phelps_Stokes Commissions iliyokuwa imeundwa kwa ajili ya kuchunguza elimu ya waafrika.

Wakati anafika Tanganyika akiwa ndani ya kamisheni yake hiyo, Dr Aggrey alikataliwa kupanga New Afrika Hotel kwa kuwa alikua mtu mweusi. Ndipo Gavana Cameron ilim'bidi amtafutie chumba Government House ajistiri kwa malazi

Wakati alipokuwa Dar es salaam ndipo Dr Aggrey, akakutana na Kleist Sykes. Baada ya mazungumzo wa muda mrefu baina yake na mgeni wake huyo, Dr Aggrey alimtunukia Kleist moja ya vitabu vyake vya siasa na akakitia sahihi yake.

Kwa kitendo icho alichofanyiwa na Dr Aggrey, Kleist Sykes alipata hamasa na mwaka 1929 Kleist na marafiki zake wa karibu wakaanzisha African Association (A.A). Kwa mchango aliohutowa Dr Aggrey katika nchi yetu, nasi bila hiyana tukamtunukia mtaa wenye jina lake.

Wahenga wenzangu hii ndio historia ya kweli kabisa ambayo imefichwa na watu wasiopenda Mimi, wewe na vizazi vyetu tuijue historia hii adhimu ya wapigania uhuru wa nchi yetu. Na vilevile historia hii, huwezi kuipata katika vitabu vya kufundishia mashuleni.

ASANTENI:
 

Attachments

  • 1686764223452.jpg
    1686764223452.jpg
    76 KB · Views: 13
Asante sana Mohamed Said kwa majibu yako mazuri, Rais muasisi ni Cecil Matola. Swali la pili, je huyu Cecil Matola hakuwa na mchango wowote katika uanzishwaji wa AA?
Mag3,
Mkutano wa kuasisi AA ulifanyika nyumbani kwa Cecil Matola Mission Quarter.

Waasisi wengine walikuwa Kleist Sykes (Secretary), Mzee bin Sudi, Ibrahim Hamisi, Suleiman Majisu, Zibe Kidasi, Ali Said Mpima, Raikes Kusi na Rawson Watts.

Lakini katika kundi hili mchango mkubwa na uongozi khasa wa mambo katika AA alikuwanao Kleist Sykes kwani yeye alikuwa na hali nzuri ya fedha.

Isitoshe mwaka wa 1933 Kleist, Mzee bin Sudi na Ali Jumbe Kiro wakaunda chama kingene pembeni ya AA Al Jamiatul Islamiyya fi Tanganyika (Umoja wa Waislam wa Tanganyika).

Katika chama hiki kipya Mzee bin Sudi akawa President na Kleist Secretary.

Cecil Matola akafariki 1934 Mzee bin Sudi akawa President wa AA.

Ikawa sasa viongozi wa juu wa AA ndiyo pia viongozi wa Al Jamiatul Islamiyya fi Tanganyika.
 
Asante sana Mohamed Said kwa majibu yako mazuri, Rais muasisi ni Cecil Matola. Swali la pili, je huyu Cecil Matola hakuwa na mchango wowote katika uanzishwaji wa AA?
Cecil matola hahusika hata kidogo AA , mhusika mkuu wa Aa alikuw ni mashanto plantains mwanajeshi mzuru kutoka afrika kusini.AA kiliundwa ili kutetea haki za waafrika waliopigana vita ya kwanza ya dunia 1914-1918,mashanto plantans ndie baba mzazi wa Abdul seksi na klest siksi.
 
Cecil matola hahusika hata kidogo AA , mhusika mkuu wa Aa alikuw ni mashanto plantains mwanajeshi mzuru kutoka afrika kusini.AA kiliundwa ili kutetea haki za waafrika waliopigana vita ya kwanza ya dunia 1914-1918,mashanto plantans ndie baba mzazi wa Abdul seksi na klest siksi.
Yve...
Taarifa yako haiko sawa.

Cecil Matola ndiye alikuwa President.

Mashado Plantan hakutoka Afrika Kusini yeye kazaliwa Mozambique na baba yake ni Affande Plantan Mkuu wa Germany Constabulary.

Mashado aliingia Tanganyika 1905 akiwa mtoto mdogo kuja kwa baba yake.

Baba yao Abdul, Ally na Abbas ni Kleist Sykes.

Ujamaa wa Affande Plantan na Sykes Mbuwane babu yake Abdul Sykes ni kuwa Affande Plantan alimuoa dada yake Sykes Mbuwane.

Haya yote aliandika Kleist Sykes na yapo kwenye kitabu, "Modern Tanzanians," kitabu alichohariri John Iliffe (1973).
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom