TUCTA: Mishahara kutoongezwa kumepunguza ari ya kazi

beth

JF-Expert Member
Aug 19, 2012
3,877
6,326
Kaimu Katibu Mkuu wa TUCTA, Said Wamba amesema Wafanyakazi hapa Nchini hawajaongezewa Mishahara kwa miaka 8 kwa upande wa Sekta isiyo rasmi na miaka 6 kwa Sekta ya Umma

Amesema, "Hali hii imesababisha kupungua kwa ari ya kazi na hivyo kupunguza ufanisi ya uwajibikaji mahali pa kazi. Gharama za maisha zimezidi kupanda ilihali stahiki na ujira zimeendelea kuwa duni"

Ameeleza hayo katika Uwanja wa CCM Kirumba Mkoani Mwanza kwenye maadhimisho ya Siku ya Wafanyakazi. Kaulimbiu ya mwaka 2021 ni "Maslahi Bora, Mishahara Juu, Kazi Iendelee"
 
Inabidi wafanyakazi mpewe na fidio la miaka sita yote au naongopa ndugu zangu?
 
  • Thanks
Reactions: Lee
MBONA walikua hawathubutu kusema??? Tucta Hamna kitu pale..Hovyo Kabisa...
 
Kuongezewa mshahara ni jambo zuri ila sio chachu ya ufanisi, utapata mshahara mpya leo utafurahi ila na uhakika baada ya mwezi tu utasahau na utataka zaidi ila yako mambo mengi kazini yanaoweza kuleta furaha na ufanisi. Mishahara mizuri, madaraja lakini kubwa mazingira ya kazini na kuridhika na mtu kuona kuwa kuna nafasi kesho akafika pale.
 
Acheni uongo, baada ya mishahara kutokupanda na nidhamu kwa watumishi wa umma imeongezeka maradufu...tuenzi mazuri ya aliyetangulia...kujenga madaraja, SGR na kununua ndege ni muhimu kuliko kulipana mishahara minono, nasema uongo ndugu zangu ?🤸🤣🐒
 
Kumbe hata kikwete hakuongeza mishahara mwaka mmoja wa mwisho


Ila nidhamu haiwez kurud kisa kuongeza mishahara, marais walopita walkua wanafanya hlo ila uwajbikaji ulikua hafifu sana. Watumish walilidhika sana maana walikua hawwajibishwi, kamat za waajir znajua kuajir ila kupanish kwa wale wazembe hawajui hata utendaji wao unaposhuka wao kuajir na kupandsha madaraja tu ndo kitu wanajua
 
Back
Top Bottom