Ni muda mrefu sasa uwakilishi wa wananchi hasa bungeni hauna mwongozo (uregulated). Raia mmoja anaweza kuwa mbunge kwa zaidi ya miongo minne. Ni ukweli usiopingika kuwa mwakilishi wa wananchi bungeni anachaguliwa na wananchi. Iwe kwa rushwa, kihalali, kwa huruma (wananchi wanamhurumia kwani analia sana wakati anaomba kura), kwa vitisho nk.
Imefika wakati uwakilishi wa wananchi bungeni uwe na mwongozo (sheria). Kikomo cha ubunge kiwekwe. Hii itasaidia kuongeza uwajibikaji na heshima kwa wananchi.
Pia iwekwe sheria ambayo haitalazimu mbunge kuwakilisha wananchi wake kwa kipindi cha miaka mitano. Kwa mfano, ikatokea kuwa baada ya miaka miwili au mitatu mwananchi wameona kuwa mbunge wao hawawakilishi ipasavyo kama alivyoahidi, wananchi wawe na nguvu ya kumhoji. Pale atakaposhindwa kujibu maswali ya wananchi anaowawakilisha bungeni ipasavyo au anapowadharau, basi wananchi wapewe nguvu ya kisheria kupiga kura ya kusitisha uwakilishi wa mbunge wao na kuchagua mbunge mwingine (ikishindikana kufanya uchaguzi basi ateuliwe na wananchi) kwa namna ambayo sheria itaona ni muafaka.
Nawasilisha hoja.
Imefika wakati uwakilishi wa wananchi bungeni uwe na mwongozo (sheria). Kikomo cha ubunge kiwekwe. Hii itasaidia kuongeza uwajibikaji na heshima kwa wananchi.
Pia iwekwe sheria ambayo haitalazimu mbunge kuwakilisha wananchi wake kwa kipindi cha miaka mitano. Kwa mfano, ikatokea kuwa baada ya miaka miwili au mitatu mwananchi wameona kuwa mbunge wao hawawakilishi ipasavyo kama alivyoahidi, wananchi wawe na nguvu ya kumhoji. Pale atakaposhindwa kujibu maswali ya wananchi anaowawakilisha bungeni ipasavyo au anapowadharau, basi wananchi wapewe nguvu ya kisheria kupiga kura ya kusitisha uwakilishi wa mbunge wao na kuchagua mbunge mwingine (ikishindikana kufanya uchaguzi basi ateuliwe na wananchi) kwa namna ambayo sheria itaona ni muafaka.
Nawasilisha hoja.