Yapo mambo mengi yamekuwa yakiendelea katika kipindi hiki, ambapo mengi katika mambo hayo ni ya hovyo, machafu na yasiyofaa katika jamii lakini yanahalalishwa kwa jina SIASA. Mambo yenye kushusha heshima ya mtu, kudhalilisha utu wake na kufedhehesha jamii yake siku hizi hayakemewi tena, sio na watu wenyewe ama taasisi bali hata Serikali yenyewe imekalia kimya mambo hayo na jamii wameyapa jina jipya, hauitwi tena UDHALILISHAJI bali inaitwa SIASA CHAFU.
Kwa muda mrefu, binafsi nimekuwa nikitukanwa sana hapa jamvini, tena na watu wenye heshima zao na wengine nawajua kwa sura na majina halisi lakini hata hawashtuki, nao huingia kwenye mkumbo huu wa matusi, kunidhalilisha na kunishushia heshima..wakati mwingine tunalazimika kuvumilia kwa sababu ndivyo ilivyo jamii yetu lakini hakika ni lazima tukemee tabia hizi zinazoimarika ndani ya jamii yetu...Watanzania walikuwa ni watu wenye kutolewa mfano kwa kuheshimiana, kupendana na kuishi kijamaa lakini hali ya sasa ni ya mazungumzo ya chuki, uhasama, kudhalilishana na kuvunjiana heshima.
Nimeiona VIDEO inayozunguka kwenye mitandao ya kijamii, ikimdhalilisha Mama Regina, huyu ni Mwanamke mwenzangu lakini pia ni kama Mama yangu mzazi kwa umri wake na mtu mwenye heshima ya kipekee katika jamii yetu, si jambo jema hata kidogo, Mimi nalipinga jambo hili kwa namna yeyote ile itakavyotafsiriwa.
Hii sio siasa, na nawaonya Vijana wenzangu wa CHAMA CHA MAPINDUZI (CCM) ikiwa wao ndio wanaozisambaza video hizi, wajue wanafanya makosa kisheria na ni kukosa adabu na heshima kwa wazazi wetu. Nimewataja Vijana wenzangu wa CCM kwa sababu VIDEO hiyo nimeiona kwenye simu ya mmoja wao akidai ametumiwa na kijana anayeitwa Peter Kasera (ambaye nae ni kijana wa UVCCM) hizi sio tabia za wanachama ama Vijana wa CCM, MNATUDHALILISHA. Na nimeamua kukutaja kwa jina halisi ili uone haya kokote ulipo na ujutie kitendo chako, ikiwezekana uombe radhi kwa kitendo hicho.
Lakini pia hawa wapiga picha wanaokuwepo kwenye shughuli za CHADEMA na UKAWA hivi mnaishi nao vipi..? maana event ile ni ya "wanamabadiliko" imekuwaje VIDEO ile imevuja..? It's obviously kuwa mpigaji picha deliberately ameamua kuitoa kwa maslahi yake na ya wale anaowajua yeye.
Maoni yangu:
Watu hawa wote wachukuliwe hatua, kuanzia yule aliyefanya kitendo kile, aliyevujisha VIDEO pamoja na hawa wanaoendelea kusambaza..kwani ni hatua ya juu kabisa ya UDHALILISHAJI aliyofanyiwa Mama Regina.
NB:
Sitoiweka VIDEO hiyo hapa, na siitaji mtu yeyote katika uzi huu ama mwingine aweke VIDEO hiyo ama yenye mfano wa hiyo, Mods stay alerted...hata kama ni SIASA jamani kuna maisha baadae..TUACHE UDHALILISHAJI, imetosha sasa.
Mkuu umesema ukweli kabisa tabia hii ni bora watu wa pande zote mbili tungezingatia utu
kwanza.iwe ccm au upinzani, tungethaminiana. Tumezidi mipaka sana!
Lakini mkuu naona umesema vijana wa CCM ndo wanatukana, mimi katika hilo siwezi kusema ni kweli au hapana. Kwa mtazamo wangu naona wanao ongoza na kufundisha kutukana ni Mkurugenzi wa TCRA na wafanyakazi wake kwa kushindwa kukemea kashfa hizo au kuzichukulia hatua.
Sasa kama upinzani wanatukana na hata ccm wanatukana na kusambaza picha za kashfa mfano kama picha tajwa hapo juu, TCRA haitakiwi kulifumbia macho kamwe kwasababu ndo wame anzisha sheria za mtandaoni.
Katika maelekezo ya mwanzo ya TCRA, walisema mtu ukitoa taharifa ya kudharirisha, au uongo, au picha kutuma na kupokea picha za kudharirisha, muhusika atakuwa amevunja sheria na pia na faini za sheria hizo walizitaja.
Katika hali ya kusikitisha ten asana, huyu mkurugenzi wa TCRA na watu wake, wamekuwa wakifumbia macho Video za kashifa zinasambaa hovyo na ku-dharirisha au kushusha utu wa mtu. Lakini akisemwa kiongozi tu wa selikari, utasikia wanajitokeza kuwa mtu kakamatwa!!!
Nachukua hatua hii kukuaonya wewe mkurugenzi wa TCRA, Tafadhari simamia sheria hii kwa ku-balance na kutenda haki. Siyo watu humu kipindi hiki wanadharirishwa sana, mtu anaibua kashfa za aibu anatuma na nyie mko kimia, mnasubiria asemwe Mkuu wa majeshi ndo tunakuja kuwaona kwenye TV. Picha tajwa ya huyu mwanamke kiukweli ni udharirishaji kabisa, TCRA haikutakiwa kuifumbia macho hata kwa kumuonya muhusika.
JESHI LA POLICE
Mchungaji Gwajima, akiwa kanisani kwakwe, alisema maneno juu ya Askofu wa kanisa katoliki, ambayo maneno hayo, mimi siwezi kusema alikosea au hakukosea , ila nyie Jeshi la police mlitafisili amekosea na mim si walahum kwa hilo na hivyo kumkamata na kumhoji. Wakati huo huo Askofu wa kanisa katoliki yeye alitoa msamaha akamuachia Mungu nyie police mkakomaa, Gwajima. Gwajima mkidai ametukana!!
Sasa niwahulize nyie police, Je maneno aliyo yasema Bwn Mwigulu Nchemba kule tarime kuhusu Lowassa, maneno makali, matusi ya aibu tena ya nguoni, mbona mme kaa kimia?
Kiukweli na nyie mnachangia kupotosha na kuharibu mahadili ya nchi yetu kwa ku-tobalance kazi zenu. Naomba niwakumbushe. Tafadhari tendeni haki msije mkafikili siku ya kihama haipo. Hipo vizuri na Kila mtu atahukumiwa kwa kazi zake.
Mwisho: ombi langu sisi wenyewe wananchi,kama mtoa mada alivyo sema ni bora hata bila sheria tukaheshim utu wa mtu awe CCM au ukawa au asiye kuwa na chama. Mwenye hati miliki ya maisha ya mwanadam ni Mungu tu.