Tuache uwongo Genocide ya Rwanda haikusababishwa na Media bali ni Utawala wa Kibabe na wa Kikabila.

Wewe unayejua weka basi hapa hayo unayoyajua na acha kupaparika kama Kuku Jike aliyetoka kupandwa na Jogoo muda mfupi uliopita.


Achana nae huyo poyoyo, wenye akili tumekuelewa vizuri, kulaumu vyombo Vya habari ni sawa na kuhangaika na ulipoangukia badala ya pale ulipojikwaa! Tanzania tukikosa a calming voice, a voice of reason, a unifying voice, a consoler in chief tukakakamaza shingo kwa vitisho na ubabe na kauli za kuwagawa watu, Mungu atunusuru, taifa litaangamia, tunahitaji sauti inayopooza cheche na wala sio kuzitia petroli! Wako wapi wababe wa dunia hii kina Bokassa, Mobutu, Samuel Doe, Gadafi, Mussolini, Hitler, Stalin nk; wako wapi
 
Hao wapinzani unaosema welipania kuutoa utawala madarakani walitumia njia zipi kuunganisha watu??? Vyombo vya habari havikutumika???
Ukija hapa nchini kwetu je kuna ukabila wa kiwango unachokisema hapo???.
Na kama upo ukabila wa hivyo je unaweza ukanambia hasa ukijikita katika mfano ulio utoa ukitumia wasukuma, je unaweza kunitajia ni angalau wasukuma 10 walio Fanya makosa wazi kabsa na wakaachwa bila adhabu yoyote??? (taja na makosa angalau mawili kwa kila mmoja).

Mwisho ni nini unataka kutuaminisha hapo kuhusu tasnia ya habari hapa kwetu??
 
Mkuu Ulikuwa Wapi? Ni kitambo Sasa Umepotea Comrei.

Nakupongeza kwa kuja na kabandiko kako ka kutoa Angalizo kwa Viongozi wetu.

Lakini napenda ni kukumbushe kwamba sisi tulio ona Mbali tuliwambia tulipokuwa tanaelekea kwenye Uchaguzi 2015

kwamba Tanzania inamwitaji Kiongozi Mwenye Vision.

Sasa nadhani mmeanza kupata Akili, tatizo la maendeleo ya Tanzania halikuwa Ufisadi Bali ni Mipango Mizuri ya Uongozi na Utendaji.

Japo wengi tuliaminishwa kwamba tatizo la tanzania kutokuendelea ni Ufisadi lakini sasa tunagundua kwamba tatizo ni Mipango na Utekelezaji wa Serikali usiokuwa na Dira au Mipango Madhubuti.

Niaibu kuona kanchi kadogo kama Rwanda kalichotoka kwenye Vita juzitu 94 kameshatuacha kwa mbali sana kwa maendeleo!!!!!

Halafu sisi tunabaki kutimuana timuana visasi gilba na maneno mengi badala ya kuweka mipango mizuri ya maendeleo tunabaki kutumbuana!

Mtashtukia 2020 imefika tunakwenda kwenye Majukwaa na kuanza kutoa sababu lukuki kwa wananchi na kupiga pushap jukwaani ili kutafuta huruma za wananchi?

Sikweli kwamba Rais Aliyepo madarakani sasa hivi hajafanya mazuri.

Amefanya tena Mengitu. Ila wananchi tunataka tuone Maendeleo kwa wananchi na siyo kama mwalimu nyerere alivyotuambia kwamba maendeleo siyo Vitu bali maendeleo yanatakiwa yaonekene kwa watu.

Ikiwa mtanzania kwa sasa hata mlo 1 haupati tena! Ukija kumwambia umejenga Mabarabara, umepunguza wafanyakazi hewa na kutumbua Majipu, hunakushanya matrilioni ya kodi, huku yeye haoni unafuu wa maisha hawezi kukuelewa kabisa.

Tujifunze katika utawala wa mzee mkapa yeye aliwezaje kupandisha uchumi wa nchi na kudhibiti mifumuko ya Bei?

Sote tunakumbuka kulikua na urahisi wa bidhaa muhimu kama vyakula, usafiri, ujenzi na Nk.

Sasa wananchi wanajiuliza Awamu hii vp? Kama imeweza Kudhibiti mianya yote na kukusanya matrilioni kwa mwezi mbona hawaoni unafuu wa maisha?

Nahapa wananchi wakihoji viongozi wasiwaone wananchi siyo wazalendo kwa kuhoji kulikoni?

Uzalendo ni pamoja na kuhoji hasa pale tunapoona mambo hayaendi sawa.

Nimalizie kwa kusema, kuchagua ni uchaguzi wa kila mwananchi ila maumivu ya kuchagua vibaya Au Vizuri yanatugusa Wote.

Nipo Mkuu ila nashangaa sana umenitupa siku hizi sijui labda unahisi nimekubandulia Shemeji yetu ( Mkeo ) kwani siku hizi hunipi ushirikiano wako kama zamani wakati ni ukweli usiopingika kuwa Mimi na Wewe ni kama Kikwete na Lowassa ( namaanisha ni marafiki na tumetoka mbali ). Nimekubaliana kwa 100% yote uliyoyaandika Mkuu ila kuna msemo wa Wahenga usemao na nitaunukuu kwa faida yako na kwa wengineo " mjinga wakati wa kwenda wakati wa kurudi ni mwerevu ". Yawezekana miaka hii mitani sisi ni wajinga tumekubali kwenda ila sasa hiyo 2020 ikifika tutakuwa werevu na tutarudi vizuri sana na tutaheshimiana tu.
 
Nipo Mkuu ila nashangaa sana umenitupa siku hizi sijui labda unahisi nimekubandulia Shemeji yetu ( Mkeo ) kwani siku hizi hunipi ushirikiano wako kama zamani wakati ni ukweli usiopingika kuwa Mimi na Wewe ni kama Kikwete na Lowassa ( namaanisha ni marafiki na tumetoka mbali ). Nimekubaliana kwa 100% yote uliyoyaandika Mkuu ila kuna msemo wa Wahenga usemao na nitaunukuu kwa faida yako na kwa wengineo " mjinga wakati wa kwenda wakati wa kurudi ni mwerevu ". Yawezekana miaka hii mitani sisi ni wajinga tumekubali kwenda ila sasa hiyo 2020 ikifika tutakuwa werevu na tutarudi vizuri sana na tutaheshimiana tu.
Teh Teh teh teh Komredi wangu Tupo Pamoja Sana Mkuu wangu.

Iyo Mithali yako Imenifikirisha Mbali Sana Komredi.

BG UP
komredi wangu Pamoja Sana Usipotee Sana Unajua Unatoaga Nondo Nzito sana Humu Jukwaani.
 
Vyombo vya habari ndivyo vilivyopiga mwangwi mkuu wa chuki za ukabila na kusababisha kufumuka hiyo unayoiita genocide.
Itafute na uiangalie documentary ama tuseme clip huko you tube inaitwa Hotel Rwanda.
Hapo utaona jinsi vyombo vya habari, hasa radio zilivyotumika kuhamasisha mauaji hayo.

Narudia tena kusema na kusisitiza kwa jeuri zote huku nikijiamini 100% kuwa ni ONLY 2% Media ilihusika na yale mauaji ya Kimbari ila 98% ni Uongozi wa Kibabe, Chuki, Ukabila na wa Kiupendeleo ndiyo ulisababisha yale yote. Acheni kupotosha humu Watu wa interests zenu. Ya nchini Rwanda yanajulikana na hata Wahusika wenyewe wengi wao ambao walikuwepo Arusha wakihukumiwa na sasa wengine wanahukumiwa katika Mahakama zao za Jadi ziitwazo GACHACHA wanasema huo ukweli nyie ni nani leo mtake kutudanganya kuwa mchochezi mkuu wa yote yale ilikuwa ni Media? Kawadanganyeni wengine tafadhali na siyo GENTAMYCINE.
 
Achana nae huyo poyoyo, wenye akili tumekuelewa vizuri, kulaumu vyombo Vya habari ni sawa na kuhangaika na ulipoangukia badala ya pale ulipojikwaa! Tanzania tukikosa a calming voice, a voice of reason, a unifying voice, a consoler in chief tukakakamaza shingo kwa vitisho na ubabe na kauli za kuwagawa watu, Mungu atunusuru, taifa litaangamia, tunahitaji sauti inayopooza cheche na wala sio kuzitia petroli! Wako wapi wababe wa dunia hii kina Bokassa, Mobutu, Samuel Doe, Gadafi, Mussolini, Hitler, Stalin nk; wako wapi

Safi sana Mkuu, akhsante na umemaliza kila kitu. Sishangai ndiyo maana hata ripoti ya Furaha duniani Tanzania ni wa pili. Hivi kwa mwendo huu wa mateka mikono juu plus bastola hadharani hiyo furaha itapatikana wapi? Sasa hadi tukiwa na Wake zetu Vitandani tunaogopa Kugegeda vizuri kwa hofu huenda muda wowote ukainuliwa Bastola.
 
Teh Teh teh teh Komredi wangu Tupo Pamoja Sana Mkuu wangu.

Iyo Mithali yako Imenifikirisha Mbali Sana Komredi.

BG UP
komredi wangu Pamoja Sana Usipotee Sana Unajua Unatoaga Nondo Nzito sana Humu Jukwaani.

Akhsante sana Mkuu na maneno yako ama hakika yamezidi kunitia moyo ili nizidi kusaka maarifa zaidi kusudi nikija humu JF niwe kamili gado. Kuhusu kuwepo humu nadhani labda Wewe ndiyo umepotea kwani Mimi huwa sibanduki humu JF kama vile ambavyo Shiza Kichuya wa Simba SC a.k.a Mnyama Mnyamani huwa habanduki katika goli la Yanga FC a.k.a Chura Churani.
 
Hao wapinzani unaosema welipania kuutoa utawala madarakani walitumia njia zipi kuunganisha watu??? Vyombo vya habari havikutumika???
Ukija hapa nchini kwetu je kuna ukabila wa kiwango unachokisema hapo???.
Na kama upo ukabila wa hivyo je unaweza ukanambia hasa ukijikita katika mfano ulio utoa ukitumia wasukuma, je unaweza kunitajia ni angalau wasukuma 10 walio Fanya makosa wazi kabsa na wakaachwa bila adhabu yoyote??? (taja na makosa angalau mawili kwa kila mmoja).

Mwisho ni nini unataka kutuaminisha hapo kuhusu tasnia ya habari hapa kwetu??

Mkuu kwani kuna sehemu yoyote katika UZI wangu nimewaongelea Wasukuma? au unajihisi sasa na unataka kunichokoza nami nianze kutiririka juu ya Usukuma na Utawala wetu kisha ujione ulivyo mtupu upstairs? Siku nyingine nakuomba ukiona UZI umeanzishwa basi jikite mno katika kujibu Hoja na siyo kukurupuka kama ulivyofanya na kutuletea Ngonjera zako sawa?
 
Mkuu kwani kuna sehemu yoyote katika UZI wangu nimewaongelea Wasukuma? au unajihisi sasa na unataka kunichokoza nami nianze kutiririka juu ya Usukuma na Utawala wetu kisha ujione ulivyo mtupu upstairs? Siku nyingine nakuomba ukiona UZI umeanzishwa basi jikite mno katika kujibu Hoja na siyo kukurupuka kama ulivyofanya na kutuletea Ngonjera zako sawa?
Mkuu huu uzi umeunganishwa hapo. Kuna mtu alianzisha uzi hapo. Ndiye mimi nilimhoji hayo sijui umenielewa hapo.
Hebu soma post namba 2 ya Tinde nsalala utaona alichokiandika, hapo.
 
mm sijasoma story ya mauaji ya kimbali ya rwanda lakini nayafahamu chanzo cha mauaji hayo,kikubwa ni ukabila wahutu na watusi mabila makubwa rwanda,wakati huo rais wa nchi hiyo alikuwa anaitwa Haibyalimana ambaye alikuwa ni mhutu wskati huo palikuwa na uasi wa kundi la RPF ambalo lilikuwa likiongozwa na rais wa sasa bwana kagame,uasi huo ambao ulichangiwa sana na majeshi ya uganda kumsaidia kagame hadi ikapelekea mazungumzo ya amani amvayo yakusimamiwa na serikali ya tanzania arusha,mauaji yalikuja kupamba moto wakati marais wa rwanda na burundi wakitoka kwenye mazungumzo ya amani arusha ndege yao ambayo iliwabeba marais wote wawili ilipigwa kombora la kivita na kupelekea marais wote wawili kupoteza maisha yaani rais wa rwanda haibyalimana na cypirian ntayamila wa burudi,baada ya taarifa kuenea kuwa rais wao amepiteza maisha kwa ndege yake kunduliwa na kombora wakajua wazi wsliohusika ni kundi la waasi wa kitusi ndo lililofanya mauaji hayo ndo ikaanza vita ya kulipizana kisasi hapo ndo wahutu kwa sababu walukuwa serikalini wakaanza kugawa silaha kwa wahutu na kufanya mauaji makubwa sana ya kikabila ambapo ikabidi serikali ya uganda ikaongeza nguvu kusaidia kundi la RPF hadi serikali ya kuhutu ikaangushwa na kiongizi mpya wa rwanda akapatikana,msaada ukiotolewa na uganda ulikuwa wa kundugu zaidi kama mnavyojua kagame na mseveni wote ni watusi kwa uganda wanaishi maeneo ya mbarara wanajiita wanyankole,hivyo mauaji ya kimbali siyo vyombo vya habari ila ni ukabila na bahati nzuri tanzania ya nyerere aliliona hilo akajenga msingi imara ya kuondoa ukabila lakini tukilewa na amani tukaanza ukabila tumeumia na tujitahidi kama watanzania kupinga kwa nguvu zote kulipinga hilo!kwa mfano makabila yenye watu wengi msije mkaleta ukabila ni kwa kutumia wingi wenu mkanyanyasa makabila madogo taifa litawahukumu!
 
Safi sana Mkuu nataka aseme hicho anachokijua halafu nimwelekeze kama ana hicho Kitabu hapo alipo sasa hivi afungue page ipi ili nimuumbue vizuri kusudi siku nyingine asiwe anakurupuka pindi Wanamume tunapoweka uzi humu JF? Ukiona hadi natiririka na uzi humu jua nimejikoki vizuri hasa Kidata. Kwanza sidhani hata kama Kitabu chenye ameshakisoma pages zake 5 tu achilia mbali pages zake jumla 355.
Popoma,pamoja na kuwa wewe ni mnyarwanda,Nina uhakika hata hicho kitabu hukijui kinafananaje ila mkwara tu!.Unachokihadithia umekisikia kama wengine.

Nilitegemea kutokana na kuandamwa hapa,ungeleta story kwa Urefu kutokana na kuwa umekisoma.Na Mimi namsaidia huyo jamaa,nenda kajipanga upya then rudi
 
Popoma,pamoja na kuwa wewe ni mnyarwanda,Nina uhakika hata hicho kitabu hukijui kinafananaje ila mkwara tu!.Unachokihadithia umekisikia kama wengine.

Nilitegemea kutokana na kuandamwa hapa,ungeleta story kwa Urefu kutokana na kuwa umekisoma.Na Mimi namsaidia huyo jamaa,nenda kajipanga upya then rudi

Popoma Shangazi yako! Siku humu kutaka kushindana kama nimesoma hicho Kitabu au hapana kwani sidhani kama hiyo itasaidia ila nilichokifanya ni kuleta hoja mbele kusudi kupinga upuuzi fulani ulioenezwa hivi majuzi na Mbabe wa Kivita wa Magogoni kuhusu Media na mauaji ya Kimbari. Nimejipanga na ndiyo maana umeona nimeweza kuanzisha Uzi ambao hata Wewe umekuvutia na umekurupuka huko ulikotoka utadhani Chura katoka shimoni na kuja kuuangalia na sasa umeshapata maarifa ambayo ulikuwa huna kuhusu Rwanda Genocide ndiyo unaanza kupovuka tu humu jamvini.
 
Popoma Shangazi yako! Siku humu kutaka kushindana kama nimesoma hicho Kitabu au hapana kwani sidhani kama hiyo itasaidia ila nilichokifanya ni kuleta hoja mbele kusudi kupinga upuuzi fulani ulioenezwa hivi majuzi na Mbabe wa Kivita wa Magogoni kuhusu Media na mauaji ya Kimbari. Nimejipanga na ndiyo maana umeona nimeweza kuanzisha Uzi ambao hata Wewe umekuvutia na umekurupuka huko ulikotoka utadhani Chura katoka shimoni na kuja kuuangalia na sasa umeshapata maarifa ambayo ulikuwa huna kuhusu Rwanda Genocide ndiyo unaanza kupovuka tu humu jamvini.
Popoma,hakuna kipya ulicholeta tusichokijua kuhusu Rwanda Gynocide.Mi nakubaliana na wewe kwamba si Media za Rwanda ndiyo zilikuwa chanzo,ila ni ukweli zilifanya kazi kubwa kuchochea,Kumbuka Biashara ni matangazo,bila media huenda mauaji yale yasingefikia kiwango kule

Ukiwa kama raia wa Kagame hebu funguka tuambie mapya tofauti na tunachokijua,ukizangatia ulisoma hicho kitabu na huenda ulikuwepo kule kipindi cha Mauaji hayo ya kimbari.Twende kazi Popoma
 
Back
Top Bottom