Kizazi Cha Sasa sio wanawake Wala wanaume tuko obsessed na kuwa weupe,wengine tunajidanganya Kwa jina la kuglow.
Kuglow uglow na rangi yako halisia huku unawaka na kumeremeta,rangi yako halisi,ngozi yako safi
kwani nani kasema weusi ni mbaya?
Weusi ni rangi adimu yenye thamani sana hata wazungu wanatamani wawe nao ila ndo hivo,wanatudharau tunavyojibabua.
Watu wenye ualbino (albinism) wanatamani wawe na hii rangi tunayoichezea lakini wapi..hawawezi.
Ndani ya mwili Kuna seli zinazalishwa tuziite melanocytes,hizi zinaachia kitu inaitwa melanin..hii ndo huchochea rangi ya ngozi nywele na macho yako.sasa unapopaka mikorogo ama kipodozi chenye kubleach huwa kinapenya na kuingia ndani ya mfumo wako wa damu,zile kemikali toka kwenye mafuta ulopaka zinaenda na kuingilia uzalishaji wa melanin, ni kama kinabock na huku Kuna nyingine inabrighten ngozi yako,utaanza kuwa wa njano au mweupe.
Lakini umewahi kujiuliza utakapoacha kutumia mkorogo utabaki hivohivo? hapana
Ukikosa pesa ya mikorogo tu utaanza kuwa kituko kama kuku aliebanikwa unajua kwanini? Sababu umeua uzalishaji wa melanin,inakulinda dhidi mionzi ya jua,so Kwa ngozi iliyochubuliwa haiwezi kupambana na mionzi ya jua na ikizidiwa kinachofuata ni kansa.
Ukioverdose matumizi ya mkorogozile kemikali Zina uwezo wa kuua kabisa seli zako mwilini.hutarudi awali tena.jua litakuwa adui yako,mionzi ikikuzidia kifuatacho ni kansa. Huoni kwanini wenye albinism wanapata tabu juani Hadi wajilinde Kwa kupaka mafuta maalum ya kuwalinda dhid ya mionzi ya jua. Sababu hawana melanin..kinyume na hapo wakikosa hayo mafuta wakipigwa na jua sana wanatoka vidonda na kansa za ngozi ndio tishio lao kuu.
Hata wazungu wanapaka sunblocks,jua sio rafiki kwao.
Kama melanin inasaidia macho tarajia macho yako kufa au uoni hafifu.huoni wenye albinism wanavyopata shida ya macho
Mkorogo unaua macho yako!
Tuthamini tulichopewa.sisi ni wazuri!
Tujikubali.
View attachment 3333527