Mushi92 na
MBEBA MAONO KAJA Meljons
Nitaelezea hapa kidogo lakini msimeze tu navyovitoa bila nanyi kujishughulisha kidogo. Nitakuwa nawaelezea huku nikiwapa link za kudadavua zaidi wenyewe pale nitakapoweza. (Japo nasengenywa na data za google, hehehe)
Nianze hivi:
1. Mnajua kwa sasa China imeipita USA na kuwa nchi yenye uchumi kubwa zaidi duniani. Hizi data zinatoka IMF na sio propaganda. Fwata habari hii hapa chini upate link zaidi
China Just Overtook The US As The World's Largest Economy | Business Insider India
Sababu kubwa ya China kuweza kuipiku USA kiuchumi ni walivyoweza kutumia mishahara yao midogo (low wages) kuweza kuwa kiwanda cha dunia. Western Countries bila kujitambua walishangaa waChina wamekua na akili na technical know how kubwa sana na mishahara yao midogo sana, hivyo cost zakitengeneza mfano kijiko zinakua ndogo sana China ukiringanisha na kutengeneza kijiko hicho Marekani hata kama unakuja kuuza Marekani hio hio.
Muda si mrefu makampuni karibia yote ya ulaya na marekani yakalazimika kufanya uzalishaji China, ili yaweze ku survive in the business market.
Capitalism ilirudi kuwaumiza waanzilishi wenyewe wa Capitalism. Wanajuta!
Sasa kwa kufupisha ni hivi, Marekani haiwezi kushusha minimum pay yao ili iweze kupambana na uzalishaji wa China, HAWAWEZI!
Vichwa vikakaaa na kutafakari watafanyeje?
Source kubwa ya energy kwa ajili ya kuendesha viwanda na uzalishaji ni nishati ya MAFUTA, na hali ilivyokuwa Marekani hawezi shindana na CHINA kununua mafuta, Mchina ana hela zaidi!! Na Mchina alikua tayari kununa mafuta Iraq na Libya kwa bei kubwa sana, sababu hela anayo.
Sasa imagine wewe ndio Marekani, kuna factors kubwa 2 za uzalishaji 1 ni wafanyakazi 2. source of energy au chanzo cha nishati
Sasa basi wafanyakazi unao lakini huwezi shusha mishahara sababu maisha tayari yako juu, wafanyakazi wako wamezoea mishara mikubwa na maisha mazuri, pili huna uwezo wa kununua mafuta kwa bei ya soko huria, na nchi yako inazidi kudidimia kiuchumi kila kukicha, viwanda vinafungwa uzalishaji unadidimia. Ungefanya nini??
Fikiri kidogo.
...
...
...
...
...
Ni hivi..
Mmarekani akaamua kutumia kitu kimoja tu alichobaki nacho kama namba 1 duniani, nacho ni JESHI! Hivyo basi, tuanzishe vugu vugu la mapinduzi arabuni kote, kwa uongo wa kuleta Demokrasia, Kutokomesha Terrorism nakadhalika machafuko yakiendelea sisi tunaendelea kuwauzia hao waarabu silaha huku tukiiba mafuta na yale tutakayo shindwa iba tutawaambia watulipe silaha tunazowapa kwa mafuta. HICHO NDICHO KINACHOTOKEA UARABUNI!!
Waliingia Iraq kwa kisingizio cha WMD, hatujaziona. Wakamuua Saddam wa watu bila huruma eti kisa aliua kurds na wakasema wanaleta demokrasia. Iko wapi hio demokrasia sasa Iraq. Mbona Saudia hakuna hio demokrasia ila hawajaingia?
Wameingia Libya, wakamuua na Ghaddafi. Sababu ni nini? Embu jiulize, Gadaffi aliuliwa kwanini? Mnajua Libya ilikua nchi isiyo na deni lolote, umeme walikua hawalipi na wala kodi hakuna? Angalieni link hizi: (Msije lia tu)
LiveLeak.com - Facts About Libya Under Gaddafi That You Probably Did Not Know!
Ingieni hata wikipedia muone.
Haya basi hio Demokrasia wanayoileta iko wapi?
Jiulizi hizo silaha na risasi zisizoisha mpaka leo zinatoka wapi wakati hakuna viwanda vya silaha uarabuni?
Sasa wakati wao wanapiga, jamaa wanaiba mafuta, na vita ikiisha tu, kama basi itaisha hivi karibuni Mmarekani anakuja na deni la ma trillioni na kukwambia hili ni deni lako kwa vifaa tulivyotoa wakati wa vita. Mtatulipa kwa mafuta ambayo kampuni zetu za USA zitawasaidia kuchimba, tunawasaidia sababu ndio mmetoka kwenye vita tu jamani!
Anyways niachie hapo ila tambueni kuwa machafuko ya huko arabuni na afrika kaskazini mwa sahara ni kwa ajili ya wizi wa mafuta wa Marekani.
TURUDI HAPA KARIBU NA KWETU KWA WABANTU HAPO WEST AFRICA.
West Africa ina visima vya mafuta na hazina ya mafuta nyingi mnooo. Imekua ni nia ya USA kutaka ku control vyanzo hivi vya mafuta na rasilimali zetu kwa mda mrefu sana kuanzia enzi za ukoloni.
http://www.markswatson.com/afrioil.html
Ila wataingieje sasa? Maana kwa uarabuni wanatumia kete ya
TERRORISM ili kuhamasisha na kushawishi wananchi wao wakubali nchi yao kwenda vitani Uarabuni. Terrorism imetengenezwa na CIA kwa faida ya Marekani, wale watu unaona wanachinjwa eti na kurushwa mitandaoni ile nitaongelea siku ingine.
Sasa basi, wataingieje West Africa na kui control, wanaume wakaanza kuumiza vichwa tena.
Mnakumbuka hii kampeni iliyozuka ghafla April nafikir:
Tuliona
#BringBackOurGirls kila kona na dunia nzima utadhani hao BokoHaram wanashinda twitter na FB kuangalia comment zenu.
Ukweli ni kwamba ile kampeni ilikua feki tupu na propaganda kujaribu kutengeneza ushawishi duniani na hasa Marekani kuwa Boko Haram ni hatari, na jeshi la marekani linahitajika kusaidia kule WA!!
Hehehe hii mbinu ikagoma. Bahati mbaya, wamarekani wengi hawakuwajali sana wasichana mia 2 kiasi cha kuwa tayari kuruhusu Jeshi lao liende.
Basi ndio vichwa vikaja na
EBOLA!!!!!!!!!
Sasa isingetosha tu kuwa na EBOLA huko mbali West Africa wananchi bado wasingekua na support kwa serikali yao kutuma Jeshi, kwahio chakufanya ni kuonyesha ya kwamba EBOLA INAWEZA KUJA MPAKA MAREKANI, SI MNAONA WATU WETU MPAKA HUKU MAREKANI WNAKUFAAA!!!!!
Obama mara moja akaagiza watumwe wanajeshi elfu 3 mia 9 kwenda kusaidia mlipuko!! NANI AIUNUE MDOMO KUBISHA, HUYO ATAKUA ENEMY OF THE STATE (ADUI WA NCHI!!!!)
Hao askari ni wakulinda maslahi ya mafuta ya Marekani yanayotoka WA, kiukweli mnaweza kufa kama inzi tu Mmareakni asijali sana, ila ni pale tu ambapo na yeye yuko hatarini. Koffi anan alisema hili juzi.
SASA MAREKANI ITAKUA INA UWEZO WA KUSHINDANA NA CHINA SABABU INAPATA NISHATI YAKE KWA GHARAMA NDOGO SANA IKITUMIA MABAVU NA STRATEGIC THINKING YA JUU!! MCHINA ATABAKI NA SILAHA YAKE YA PESA, LAKINI FOR HOW LONG?
Basi ndugu zangu hivyo ndio ambavyo mnaona jeshi la marekani limetua West Africa, na haliondoki leo wala kesho. Inawezekana kweli EBOLA ipo lakini sio tishio, tena hasahasa huko marekani kama tunavyolishwa kwenye vyombo vya habari!!!
Wenzetu wanafikira mbali sana kuhusu mistakabili ya nchi zao, achana na sisi tunaowaza kujishibisha matumbo wenyewe na kukata mauno jioni. Hawa jamaa wanapanga mikakati leo kwa vizazi vya miaka 200 mbele.
Kama una swali uliza natumaini kuna wakuu wengine hapa wako fiti kuelezea. Hivi vyote vinapatikana mtandaoni ukiwa mdadisi kidogo sana.
cc
Elli BAK MziziMkavu Riwa Eiyer The hammer King Kong III Deception maziku Masunga Jr
D 007
Na wengine.