Trump atashinda Uchaguzi USA

Trump atashinda Uchaguzi USA

Uchaguzi wa Mwaka huu utakuwa mgumu sana
Media itaplay big part na kule Clinton keshajiandalia almost 1bil $ ili kufanyia kampaign
 
Media zinapenda anaependwa zaidi
Mi naufatilia vizuri huu uchaguzi
Wewe unahisi media zitampenda nani kati ya Trump na Hillary?(kumbuka atakaependwa na media lazima atashinda!)
 
Wewe unahisi media zitampenda nani kati ya Trump na Hillary?(kumbuka atakaependwa na media lazima atashinda!)

CNN wameshaenda upande wa trump
Na media nyingi ziko upande wa Trump
Huyu hajawah kuwa mwanasiasa ila ona alivyowashinda wanasiasa
 
CNN wameshaenda upande wa trump
Na media nyingi ziko upande wa Trump
Huyu hajawah kuwa mwanasiasa ila ona alivyowashinda wanasiasa
Wamarekani ni ovyo, wanapenda ule utabe na kiburi cha jamaa hasa kwenye foreign policy!....Jamaa alifananisha trade deficity ya Marekani kwa china kama ubakaji, mambo kama hayo ndo yanampa popularity!!
 
Huu mnyukano nimeupenda na Trump ataibuka kidedea..

Hivi ule ugonjwa wa moyo wa Bi Hilal Clinton uliishia wapi vile?
 
YANAYOENDELEA REPUBLICAN BAADA YA TRUMP KUKOSA WA KUMZUIA.(JAMAA WANADHIHIRISHA DEMOCRACY HAPA TZ WANAKUKATA JUU KWA KWAJU NA KUMUWEKA WAO)
Na:Joseph Mshinga.

1.Wapinzani wa Donald Trump wamejitoa wote baada ya matumaini yao kumzuia kushindikana.

2.Hakuna namna tena ya kumzuia billionea Donald Trump kuwa mgombea urais wa Republican.

3.Chama cha Republican kinashuhudia mgawanyiko na mpasuko mkuwa kabisa kuwahi kutokea kuliko wakati mwingine wowote.

3.Wanachama wa Republican wameonekana kuchoma moto kadi zao za uachama kama hasra zao kwa mgombea ambaye hawamtaki.

4.Wapo wanaosema hawatashiriki kabisa kupiga kura uchaguzi mkuu kwa kuwa Donald Trump hawamtaki na hawawezi kumpigia kura Hillary Clinton.Wapo ambao wanajiondoa katika chama.

5.Wapo wanaosema watalazimika kumchagua Hillary Clinton maana hawako tayari kuona Donald Trump anakuwa Rais wa Marekani.

6.Wapo wanaoona ni bora tu wakubaliane na hali na kumuunga mkono mtu ambaye hawamtaki kwa manufaa ya chama.

7.Aliyekuwa Rais wa 41 wa Marekani George H.W Bush mwenye umri wa miaka 91 amesema atajiweka kando katika uchaguzi huu na hana mpango wa kumuunga mkono Donald Trump.
Hii ni mara ya kwanza kwa George H.W Bush kutomuunga mkono mgombea wa chama chake cha Republican katika chaguzi zote.

8.Aliyekuwa rais wa 43 wa Marekani George W Bush(Junior ) naye amesema atajiweka kando katika uchaguzi huu na hatamuunga mkono Donald Trump.
NB:Marais wastaafu wa Republican walio hai ni hawa Bush wawili kwa maana ya baba na mwana.

9.Aliyekuwa mgombea Urais wa Republican 2012 Mitty Romney amesema hatamuunga mkono Donald Trump na ameenda mbali zaidi kwa kusema kuwa hata kwenye mkutano mkuu wa kumtanganza mgombea pale Cleveland hatashiriki.

10.Aliyekuwa mgombea Urais wa Republican 2008 John McCain naye yupo mbioni kutoa taarifa rasmi.Taarifa za awali zinadokeza kuwa naye atachukua msimamo wa kutomuunga mkono Donald Trump na atajiweka kando katika uchaguzi huu.

11.Matajiri wapenzi wa chama nao wamegawanyika kama ilivyo hapo juu kwa makundi mengine wapo ambao wameonekana tayari kumuunga mkono Hillary Clinton kwa kuandika hadharani kauli mbiu ya Hillary Clinton I AM WITH HER (wakimaanisha wanamuunga mkono Hillary Clinton na si mgombea wa chama chao).

Mbona naona kama unaandika kwa emotions zako zaidi ya kubalance story? Trump alisimamishwa na nani ikiwa republican wote hawamtaki?

Huku unasema Trump atashinda uchaguzi USA, halafu hapo hapo unasema watu wote hawamtaki na wanamuunga mkono Clinton! Nani atampigia kura trump? Mbona kama na wewe ni mwathirika wa sera za trump kwa uandishi wako?

Ninamuunga mkono Trump kwa 100% kwa sababu atawaambia ukweli viongozi wapuuzi wa Africa wasiojali uhai wetu.

WAKATI WASIOPENDA KWELI NA USTAARABU WAKIUMIZA VICHWA ITAKUWAJE JAMAA AKISHINDA, DUNIA YA KWELI NA USTAARABU INAMHITAJI TRUMP! TRUMP ANAHITAJIKA KWA DUNIA NZIMA!. APEWEEEEEEEEEEEEEEEEEEEEEEEEEEEE!
 
Kama wote hawamuungi mkono huyo mtu amefikaje fikaje huko alipo sasa?
 
Hahaha ....bora huko wana akili ....huku kwetu gia zilibadilishiwa angani na watu wakakubali kuzungurusha mikono ...wengine na barabara wakadeki ....kweli elimu, elimu, elimu ....
Ila la kushangaza zaidi huku kwetu mtu anashinda kabisa Urais kwa kupigiwa kura na Wananchi ila hatangazwi yeye anatangazwa mwingine kisha wana dola.

Au mpinzani akishinda urais kwa kura za wananchi basi uchaguzi unafutwa,sasa hapo kuna democracy gani? Hahahaha....

Only in Tanzania.
 
Huwezi kuchukua nchi ikiwa wengi ndani ya chama chako wanakupinga wazi wazi tena hadharani. Hillary akijipanga vizuri kwenye hizi kampeni kuwatumia akina Michelle, Barack, African American, white na Latino celebrities wanaomuunga mkono na kuhakikisha wote wanaomuunga mkono kujitokeza kwa wingi kupiga kura, basi ataichuikua nchi kiulaini na hivyo kuwa mwanamke wa kwanza kuwa Rais USA.
But Hillary HAFAI kuwa rais. Usiniulize kwanini
 
Siwaamini sana wazungu, hayo yote naona kama mazingaumbwa kwa nchi nyingine hasa shamba lao la bibi Africa. Wanalao lengo kwa mavi hii.
 
Raic kaishachaguliwa na freemanson hkuna wa kupinga.

Donald atapita kama obama alivyopita kimuujiza.
Obama alipitaje kimiujiza? Hakufanya kampeni na kupigiwa kura na wananchi wa Marekani?

Freemasons ni imani za hovyo hovyo tu na za kutunga.
 
Hii dhana yako sijui umeitoa wapi maana haina supporting evidence. As per opinion polls taken recently Hillary is the most qualified candidate to become US President in 2016.

But Hillary HAFAI kuwa rais. Usiniulize kwanini
 
Trump namfananisha na Lowasa hapa Tanzania..
 
we all know that Ameraca pretend to hate trump bt they like a kind of president like him.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom