Picha halisi ni hivi: (1) Kuna wapiga wa kura Republican walioonesha kumtaka Trump awe mgombea wa chama hicho. Huko ndiko kwenye kelele nyingi kiasi kwamba kwa wale wasiofuatilia habari kwa makini ndiyo wanafikiri basi kashinda kwa majority ya Wamarekani. Sivyo kabisa. (2) Kuna wapiga kura wa Democratic party ambao wanaelekea kumpendelea Hillary Clinton awe mgombea wa Democratic party. Kumbuka kwamba Trump na Clinton hawajapambanishwa kwa kura bado. (3) Kuna wapiga kura wasiofungamana na chama chochote kati ya hivyo viwili.
Unaposema hamung'unyi maneno, kwa kiasi fulani ni ukweli. The problem ni maneno mabaya. Ukiona mtu anagombea nafasi ya juu ya nchi halafu hamung'unyi maneno na kumwaga matusi ya nguoni kwa sababu hajampenda mtu fulani, huyo ni bozo hafai kwa ofisi hiyo. Msikilize vizuri, usirukie tu kwa sababu mtu mwingine kamsifia kwenye kijiwe. Soma habari zake. Sidhani kama ukipata habari zake zaidi kama utamshabikia hivyo.
Fact nyingine: Wapiga kura wa primaries kwa kawaida ni wachache zaidi ya wapiga kura wa general election.
Narudia utabiri wangu: Kwa mujibu wa mambo niyaonavyo hapa, Trump hawezi kushinda labda utokee muujiza. Hata kwa watu wa kawaida, Trump hakubaliki. Anakubalika miongoni mwa wapenda ubaguzi. Hao ndiyo walihamasika sana katika primaries. Come November, it's going to be a whole new story.