Trump atashinda Uchaguzi USA

Trump atashinda Uchaguzi USA

ImageUploadedByJamiiForums1462652443.213165.jpg
ATAKAEKATA JINA LA TRUMP TU TUNAE. MSIFIKIRI HAPA TZ, MLIKATA LA JAMAA TUKAKOSA NDEGE YA FASTA KUTUA HUKO. KATA JINA LA DONALD UONE NAVYOMALIZA KAZI
 
Huwezi kutegemea kushinda Urais wa Marekani bila support kubwa ya Watu weusi na Latino ambao Trump kishawatukana vya kutosha na hii kupingwa na vingunge mbali mbali ndani chama chake ikiwemo Bush 41 na Bush 43, Laura Bush na wengineo wengi ndani ya chama chao ni kizingiti kingine ambacho kitamkosesha kura nyingi sana na pia baadhi ya Republicans wameshasema hadharani kwamba ni heri wampigie kura Hillary kuliko Trump, kutusua kwake mwisho kwenye primary race Urais ni vigumu sana kuupata.

Nyani Ngabu yeye alishajisemea ukweli kuwa kila alichofikiri au alichotaka kiwe kwa Trump imekua tofauti yaani anatusua tu, so ameamua kukubaliana na hali halisi.
 
Naona bado una mawazo ya mwaka 47, hakuna aliyempa nafasi Obama kuchukua nchi hata watu weusi pia na political pundits hawakuona shida kutamka hadharani, "United States of America is not ready for a Black President" lakini mwanaume akafanya vitu vyake na kuchaguliwa kama mgombea wa democrats kwa kumpiga chini Hillary ambaye hakuna aliyetegemea kwamba njemba ambaye hana jina anaweza kumshinda Hillary na kisha kumpiga chini Senator McCain 2008 na 2012 kumpiga chini Governor Romney.

itachukua miaka 1000 USA kuja kuongozwa na mwanamke.mwanamke kuaongoza USA ni ndoto za alinacha
 
kama wanachama hawamtaki hizo kura anazopata zinatoka wapi?!
Anapata sapoti ya watu ila kuna kundi ninajiita establishment kwa bongo ndio kama wakina Makamba, Msekwa, JK, wale wanaojifanya chama cha kwao ndio ambao wanampinga na sababu ni kuwa jamaa akiingia watakosa nguvu ya kimaamuzi katika chama!
 
You are dreaming. Winning the Republican nomination and winning the general election are two totally different things.

Trump is not going to win the general election.
 
Hahaha ....bora huko wana akili ....huku kwetu gia zilibadilishiwa angani na watu wakakubali kuzungurusha mikono ...wengine na barabara wakadeki ....kweli elimu, elimu, elimu ....
Wengine wanaiba wake za watu wanaenda kufunga nao ndoa canada kweli elimu elimu elimu
 
Dah ...kuna watu wanaweza kuandika mizaha kama hii nisiwajibu ...ila anapoandika mtu unayefikiri si "wale" ...inafikirisha kidogo ...
Jibu swali uliloulizwa la mumeo hajambo? Sio kujifanya kuwa watu hawajui ndoa yako pale canada
 
Donald Trumph anakubalika Marekani na ndio maana kawabwaga vigogo wenzake! Marekani sio bongo yetu mtu hutakiwi na viongozi wako lkn wananchi wanakukubali wanakukatia juu kwa juu. Pale ndo kitovu cha demokrasia ilipo. Yetu macho na masikio ngoja tusubiri tuone je Trumph ataingia white house!!
Correction: Anakubalika katika Republican Party si kwa majority ya Wamarekani. Usichukulie kupita kwake katika Republican party kuwa ndiyo anakubalika na majority ya Wamarekani. Kumbuka atapambana na Democrats ambao wana mgombea wao. Hawa wa Democtratic party hawakuhusika na kumchagua Trump. Halafu kuna Independents ambao hawako katika makundi hayo mawili. Establishment ya Republican party inajua kabisa kwamba katika hayo makundi mawili hakubaliki kabisa.
Kuna historia pia miaka ya sitini walipowapitisha watu waliokubalika kwa misingi ya ubaguzi, lakini nje ya kusini mwa nchi hiyo wagombea wao hawakukubalika kabisa. Google upate habari za Barry Goldwater.
Narudia tena: Trump hataingia White House. Nakiri huu ni utabiri wangu tu.
Na wengi wa Wabongo wanaomshabikia ni kwamba hawajapata habari za Trump na sana sana wanafuata habari za vijiweni vinavyopendwa sana. Kuwa makini, soma sources za kueleweka juu ya wahusika hao.
 
Vyote ulivyoandika hapa vinaashiria kwamba hatashinda. I don't know how you twist the logic na kusema atashinda..

YANAYOENDELEA REPUBLICAN BAADA YA TRUMP KUKOSA WA KUMZUIA.(JAMAA WANADHIHIRISHA DEMOCRACY HAPA TZ WANAKUKATA JUU KWA KWAJU NA KUMUWEKA WAO)
Na:Joseph Mshinga.
1.Wapinzani wa Donald Trump wamejitoa wote baada ya matumaini yao kumzuia kushindikana.
2.Hakuna namna tena ya kumzuia billionea Donald Trump kuwa mgombea urais wa Republican.
3.Chama cha Republican kinashuhudia mgawanyiko na mpasuko mkuwa kabisa kuwahi kutokea kuliko wakati mwingine wowote.
3.Wanachama wa Republican wameonekana kuchoma moto kadi zao za uachama kama hasra zao kwa mgombea ambaye hawamtaki.
4.Wapo wanaosema hawatashiriki kabisa kupiga kura uchaguzi mkuu kwa kuwa Donald Trump hawamtaki na hawawezi kumpigia kura Hillary Clinton.Wapo ambao wanajiondoa katika chama.
5.Wapo wanaosema watalazimika kumchagua Hillary Clinton maana hawako tayari kuona Donald Trump anakuwa Rais wa Marekani.
6.Wapo wanaoona ni bora tu wakubaliane na hali na kumuunga mkono mtu ambaye hawamtaki kwa manufaa ya chama.
7.Aliyekuwa Rais wa 41 wa Marekani George H.W Bush mwenye umri wa miaka 91 amesema atajiweka kando katika uchaguzi huu na hana mpango wa kumuunga mkono Donald Trump.
hii ni mara ya kwanza kwa George H.W Bush kutomuunga mkono mgombea wa chama chake cha Republican katika chaguzi zote.
8.Aliyekuwa rais wa 43 wa Marekani George W Bush(Junior ) naye amesema atajiweka kando katika uchaguzi huu na hatamuunga mkono Donald Trump.
NB:Marais wastaafu wa Republican walio hai ni hawa Bush wawili kwa maana ya baba na mwana.
9.Aliyekuwa mgombea Urais wa Republican 2012 Mitty Romney amesema hatamuunga mkono Donald Trump na ameenda mbali zaidi kwa kusema kuwa hata kwenye mkutano mkuu wa kumtanganza mgombea pale Cleveland hatashiriki.
10.Aliyekuwa mgombea Urais wa Republican 2008 John McCain naye yupo mbioni kutoa taarifa rasmi.Taarifa za awali zinadokeza kuwa naye atachukua msimamo wa kutomuunga mkono Donald Trump na atajiweka kando katika uchaguzi huu.
11.Matajiri wapenzi wa chama nao wamegawanyika kama ilivyo hapo juu kwa makundi mengine wapo ambao wameonekana tayari kumuunga mkono Hillary Clinton kwa kuandika hadharani kauli mbiu ya Hillary Clinton I AM WITH HER (wakimaanisha wanamuunga mkono Hillary Clinton na si mgombea wa chama chao).
Joseph Mshinga.
 
kama wanachama hawamtaki hizo kura anazopata zinatoka wapi?!
Wapiga kura za primaries ndio wapiga kura wakati wa Uchaguzi, hivyo Trump anaweza kushinda hata bila ya back up ya akina Bush.
Jeb Bush alikuwa mgombea na alishindwa vibaya, ni wazi kuwa Bush family haina influence ya kuamua nani awe mgombea wa Republican.
Raia wengi wanamkubali jamaa kwa sababu hana muda wa kumung'unya maneno.
 
You are dreaming. Winning the Republican nomination and winning the general election are two totally different things.

Trump is not going to win the general election.

kama haya maneno yako ndo kura sawa
 
Ingawa maneno yangu hayawezi kuchagua POTUS, ila nitafurahi sana kama D. Trump atachukua nchi. Ila Crooked Hilary na Goofy Elizabeth Warren, mmmhn. Wakichukua hawa nitahuzunika sana!!!
Itakuwa double defeat kwangu in 2 years consequently.
 
YANAYOENDELEA REPUBLICAN BAADA YA TRUMP KUKOSA WA KUMZUIA.(JAMAA WANADHIHIRISHA DEMOCRACY HAPA TZ WANAKUKATA JUU KWA KWAJU NA KUMUWEKA WAO)
Na:Joseph Mshinga.
1.Wapinzani wa Donald Trump wamejitoa wote baada ya matumaini yao kumzuia kushindikana.
2.Hakuna namna tena ya kumzuia billionea Donald Trump kuwa mgombea urais wa Republican.
3.Chama cha Republican kinashuhudia mgawanyiko na mpasuko mkuwa kabisa kuwahi kutokea kuliko wakati mwingine wowote.
3.Wanachama wa Republican wameonekana kuchoma moto kadi zao za uachama kama hasra zao kwa mgombea ambaye hawamtaki.
4.Wapo wanaosema hawatashiriki kabisa kupiga kura uchaguzi mkuu kwa kuwa Donald Trump hawamtaki na hawawezi kumpigia kura Hillary Clinton.Wapo ambao wanajiondoa katika chama.
5.Wapo wanaosema watalazimika kumchagua Hillary Clinton maana hawako tayari kuona Donald Trump anakuwa Rais wa Marekani.
6.Wapo wanaoona ni bora tu wakubaliane na hali na kumuunga mkono mtu ambaye hawamtaki kwa manufaa ya chama.
7.Aliyekuwa Rais wa 41 wa Marekani George H.W Bush mwenye umri wa miaka 91 amesema atajiweka kando katika uchaguzi huu na hana mpango wa kumuunga mkono Donald Trump.
hii ni mara ya kwanza kwa George H.W Bush kutomuunga mkono mgombea wa chama chake cha Republican katika chaguzi zote.
8.Aliyekuwa rais wa 43 wa Marekani George W Bush(Junior ) naye amesema atajiweka kando katika uchaguzi huu na hatamuunga mkono Donald Trump.
NB:Marais wastaafu wa Republican walio hai ni hawa Bush wawili kwa maana ya baba na mwana.
9.Aliyekuwa mgombea Urais wa Republican 2012 Mitty Romney amesema hatamuunga mkono Donald Trump na ameenda mbali zaidi kwa kusema kuwa hata kwenye mkutano mkuu wa kumtanganza mgombea pale Cleveland hatashiriki.
10.Aliyekuwa mgombea Urais wa Republican 2008 John McCain naye yupo mbioni kutoa taarifa rasmi.Taarifa za awali zinadokeza kuwa naye atachukua msimamo wa kutomuunga mkono Donald Trump na atajiweka kando katika uchaguzi huu.
11.Matajiri wapenzi wa chama nao wamegawanyika kama ilivyo hapo juu kwa makundi mengine wapo ambao wameonekana tayari kumuunga mkono Hillary Clinton kwa kuandika hadharani kauli mbiu ya Hillary Clinton I AM WITH HER (wakimaanisha wanamuunga mkono Hillary Clinton na si mgombea wa chama chao).
Joseph Mshinga.
Usifikiri Wamarekani wana akili za kupandikiza kama unavyofikiri. Hao uliowataja hawafiki hata 20 na waliomchagua wengi wana hekima kuliko hata huo ukoo wa Bush.
 
Najiuliza hiv akiwa rais ataendelea kutumia ndege yake binafsi Boeng yakifahari au atatumia air force 1.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom