Pascal Mayalla
Platinum Member
- Sep 22, 2008
- 50,467
- 113,555
Wanabodi
Mzee David Wakati, amezikwa leo jioni katika makaburi ya Kinondoni.
Mazishi hayo yamehudhuriwa na umati wa watu, wakiwemo mawaziri, wanasiasa, viongozi wakuu wa dini, waandishi wa habari, na umati mkubwa wa ndugu jamaa na marafiki.
Ingawa Mzee David Wakati ametutoka, ametuachia legacy ambayo itaishi na sisi milele.
Nikianzia na kwangu mimi mwenyewe, enzi za primary, nilitokea kusoma darasa moja na mtoto wa David Wakati, Mandela hivyo kumfahamu Mzee David Wakati kupitia kwake.
Nilipomaliza shule nilijiunga na Chuo cha Uandishi wa Habari (TSJ) na kuajiriwa RTD Mzee David Wakati akiwa ni Mkurugenzi, hivyo Mzee Wakati ndie alinifungulia milango ya fani ya utangazaji ambayo niko nayo mpaka sasa.
Baada ya kuajiriwa, batch yetu ikiwa na vijana 12. Mimi Pascal Mayalla, Aboubakar Liongo, Swedy Mwinyi, Kassim Mikongolo, Bakari Msulwa, Abdalah Majula, Nswima Ernest, Rukia Machumu, Shida Waziri (Masamba), Rose Japhet, Nyambona Masamba na Jane Lutaserwa.
Wote tulipigwa kozi ya miezi mitatu ya Radio Induction Course, Mzee Wakati alikuwa ni mmoja wa walimu wetu. Alikuwa ni mwalimu wa somo la Habari na OB. Wakati huo mimi nikiwa nimepania kuwa msomaji wa habari na mtangazaji wa mpira.
Wakati wa somo la habari, Mzee Wakati alikuja na scrpts za habari na kumpa kila mmoja wetu kusoma. Wakati unasoma yeye amekaa kwenye kiti anakusikiliza huku amefunga macho na kuinua sikio moja juu.
Baada ya kutusikia sisi wote 12, alitoa majibu kuwa kati yetu wote wasoma habari ni wawili tuu, Swedy Mwinyi na Aboubakar Liongo!. Sio siri nilikata tamaa kutimiza ndoto yangu ya kuwa mtangazaji.
Mzee Wakati alitutia moyo kuwa kushindwa kusoma habari sio mwisho wa utangazaji, sio kila mtangazaji lazima asome habari, kuna vipindi vingi tuu. Kila mwanafunzi alijaribiwa kila idara, hatimaye mimi nikapangwa External Service, idhaa ya Kiingereza, hivyo huo ndio ukawa mwanzo wangu wa utangazaji. Thanks to David Wakati!.
Tulio fanya nae kazi, japo alikuwa bosi lakini alikuwa humble na down to earth!. Mzee David Wakati alikuwa ni bosi easy to talk too, yaani unajisikia huru kuingia ofisini kwake kumweleza shida yoyote, alikuwa very reachable.
Mzee huyu aliipenda radio kwa moyo wake wote!. Alikuwa na anatembea na kijiredio chake kidogo, portable cha Sony akisikiliza redio 24/7 hivyo mtangazaji ukiboronga hewani, kesho yake unapata habari yako!. Kitendo tuu cha kutangaza huku ukijua Mkurugenzi anasikiliza kuliwafanya watangazaji waliopitia RTD kuwa very resiponsible kwa wasikilizaji wao, kulikuwa hakuna upuuzi upuuzi mnaousikia kwa hawa watangazaji wa siku hizi kuna wengine utadhani wako sokoni, na wengine wanazungumza mambo ya vyumbani mchana kweupe!.
Thanks David Wakati kwa kulea kizazi cha watangazaji wenye nidhamu wa enzi zile, Thanks!.
Japo baadae nililazimika kuacha kazi ya utangazaji due to family pressure ya kutafuta maisha bora, nikajaribu maisha ya ughaibuni nchini Uingereza, Marekani, Uswisi, Italia na Sweden, kote nilishindwa nikarejea Tanzania, nikaenda Mlimani kusoma sheria na kuhitimu ili niwe wakili.
Wakati wote nikisoma nilikuwa nikifanya part time za utangazaji, baada ya kumaliza sheria, nimejikuta napenda zaidi utangazaji kuliko kusimama mahakamani. Hivyo ni ushahidi tosha kazi ya utangazaji ni kazi ya wito bila kujali ina maslahi gani, you just do what you love no matter what you get!. Thanks Mzee DavidvWakati!.
Ile batch yake ya mwisho ya watangazaji 12 aliyewaajiri wote 12 bado ni Watangazaji mpaka leo na 9 kati ya hao 12 bado TBC. Watatu tulioandoka ni mimi Pascal Mayalla, Aboubar Liongo aliyeenda Ujerumani na Abdalah Majura aliyejoin BBC. Msishangae mkisikia ninerudi TBC!. Aboubakar Liongo amerejea nchini na kwenye mazishi alikuwepo hivyo msishangae kama ataibukia TBC!. Majula nae alimaliza mkataba wake BBC na sasa anamiliki Redio yake mwenyewe ila pia msishangae kama mtamsikia nae amerejea TBC!, ili litimie lile neno, " Sikumpoteza hata mmoja kati ya wake thenashara David Wakati, aliyowachagua kabla ya kustaafu rasmi!".
Leo kwenye mazishi, nimemfanyia kipindi chake cha mwisho kwa kuzungumza na baadhi ya watu wakinipa kumbukumbu zao Mzee David Wakati amewaachia nini.
Posts zitakazofuatia nitaweka tribute hizo,
Wengine ambao unazo baadhi ya kumbukumbu za Mzee David Wakati, unaweza ukazitaja humu ili na wengine tuweze kufaidika na alichotuachia Mzee wetu, Baba yetu, Mwalimu wetu, Boss wetu, Mtangazaji wetu, Shujaa wetu, Mshauri wetu, Rafiki yetu, Mtanzania mwenzetu David Wakati,
Thank You for All This!.
Pascal Mayalla
+255 784 270403
pascomayalla@yahoo.co.uk
Update 1.
Kipindi maalum cha David Wakati Legacy kitarushwa hewani na TBC-1 Saa 5:00 usiku huu!.
Mzee David Wakati, amezikwa leo jioni katika makaburi ya Kinondoni.
Mazishi hayo yamehudhuriwa na umati wa watu, wakiwemo mawaziri, wanasiasa, viongozi wakuu wa dini, waandishi wa habari, na umati mkubwa wa ndugu jamaa na marafiki.
Ingawa Mzee David Wakati ametutoka, ametuachia legacy ambayo itaishi na sisi milele.
Nikianzia na kwangu mimi mwenyewe, enzi za primary, nilitokea kusoma darasa moja na mtoto wa David Wakati, Mandela hivyo kumfahamu Mzee David Wakati kupitia kwake.
Nilipomaliza shule nilijiunga na Chuo cha Uandishi wa Habari (TSJ) na kuajiriwa RTD Mzee David Wakati akiwa ni Mkurugenzi, hivyo Mzee Wakati ndie alinifungulia milango ya fani ya utangazaji ambayo niko nayo mpaka sasa.
Baada ya kuajiriwa, batch yetu ikiwa na vijana 12. Mimi Pascal Mayalla, Aboubakar Liongo, Swedy Mwinyi, Kassim Mikongolo, Bakari Msulwa, Abdalah Majula, Nswima Ernest, Rukia Machumu, Shida Waziri (Masamba), Rose Japhet, Nyambona Masamba na Jane Lutaserwa.
Wote tulipigwa kozi ya miezi mitatu ya Radio Induction Course, Mzee Wakati alikuwa ni mmoja wa walimu wetu. Alikuwa ni mwalimu wa somo la Habari na OB. Wakati huo mimi nikiwa nimepania kuwa msomaji wa habari na mtangazaji wa mpira.
Wakati wa somo la habari, Mzee Wakati alikuja na scrpts za habari na kumpa kila mmoja wetu kusoma. Wakati unasoma yeye amekaa kwenye kiti anakusikiliza huku amefunga macho na kuinua sikio moja juu.
Baada ya kutusikia sisi wote 12, alitoa majibu kuwa kati yetu wote wasoma habari ni wawili tuu, Swedy Mwinyi na Aboubakar Liongo!. Sio siri nilikata tamaa kutimiza ndoto yangu ya kuwa mtangazaji.
Mzee Wakati alitutia moyo kuwa kushindwa kusoma habari sio mwisho wa utangazaji, sio kila mtangazaji lazima asome habari, kuna vipindi vingi tuu. Kila mwanafunzi alijaribiwa kila idara, hatimaye mimi nikapangwa External Service, idhaa ya Kiingereza, hivyo huo ndio ukawa mwanzo wangu wa utangazaji. Thanks to David Wakati!.
Tulio fanya nae kazi, japo alikuwa bosi lakini alikuwa humble na down to earth!. Mzee David Wakati alikuwa ni bosi easy to talk too, yaani unajisikia huru kuingia ofisini kwake kumweleza shida yoyote, alikuwa very reachable.
Mzee huyu aliipenda radio kwa moyo wake wote!. Alikuwa na anatembea na kijiredio chake kidogo, portable cha Sony akisikiliza redio 24/7 hivyo mtangazaji ukiboronga hewani, kesho yake unapata habari yako!. Kitendo tuu cha kutangaza huku ukijua Mkurugenzi anasikiliza kuliwafanya watangazaji waliopitia RTD kuwa very resiponsible kwa wasikilizaji wao, kulikuwa hakuna upuuzi upuuzi mnaousikia kwa hawa watangazaji wa siku hizi kuna wengine utadhani wako sokoni, na wengine wanazungumza mambo ya vyumbani mchana kweupe!.
Thanks David Wakati kwa kulea kizazi cha watangazaji wenye nidhamu wa enzi zile, Thanks!.
Japo baadae nililazimika kuacha kazi ya utangazaji due to family pressure ya kutafuta maisha bora, nikajaribu maisha ya ughaibuni nchini Uingereza, Marekani, Uswisi, Italia na Sweden, kote nilishindwa nikarejea Tanzania, nikaenda Mlimani kusoma sheria na kuhitimu ili niwe wakili.
Wakati wote nikisoma nilikuwa nikifanya part time za utangazaji, baada ya kumaliza sheria, nimejikuta napenda zaidi utangazaji kuliko kusimama mahakamani. Hivyo ni ushahidi tosha kazi ya utangazaji ni kazi ya wito bila kujali ina maslahi gani, you just do what you love no matter what you get!. Thanks Mzee DavidvWakati!.
Ile batch yake ya mwisho ya watangazaji 12 aliyewaajiri wote 12 bado ni Watangazaji mpaka leo na 9 kati ya hao 12 bado TBC. Watatu tulioandoka ni mimi Pascal Mayalla, Aboubar Liongo aliyeenda Ujerumani na Abdalah Majura aliyejoin BBC. Msishangae mkisikia ninerudi TBC!. Aboubakar Liongo amerejea nchini na kwenye mazishi alikuwepo hivyo msishangae kama ataibukia TBC!. Majula nae alimaliza mkataba wake BBC na sasa anamiliki Redio yake mwenyewe ila pia msishangae kama mtamsikia nae amerejea TBC!, ili litimie lile neno, " Sikumpoteza hata mmoja kati ya wake thenashara David Wakati, aliyowachagua kabla ya kustaafu rasmi!".
Leo kwenye mazishi, nimemfanyia kipindi chake cha mwisho kwa kuzungumza na baadhi ya watu wakinipa kumbukumbu zao Mzee David Wakati amewaachia nini.
Posts zitakazofuatia nitaweka tribute hizo,
Wengine ambao unazo baadhi ya kumbukumbu za Mzee David Wakati, unaweza ukazitaja humu ili na wengine tuweze kufaidika na alichotuachia Mzee wetu, Baba yetu, Mwalimu wetu, Boss wetu, Mtangazaji wetu, Shujaa wetu, Mshauri wetu, Rafiki yetu, Mtanzania mwenzetu David Wakati,
Thank You for All This!.
Pascal Mayalla
+255 784 270403
pascomayalla@yahoo.co.uk
Update 1.
Kipindi maalum cha David Wakati Legacy kitarushwa hewani na TBC-1 Saa 5:00 usiku huu!.