Transfer Window updates 2013/2014 season - Europe

Transfer Window updates 2013/2014 season - Europe

Attachments

  • db97cdf19e957ff91dc81c7b17934750.jpg
    db97cdf19e957ff91dc81c7b17934750.jpg
    107.3 KB · Views: 234
Everton and Manchester United agree £27.5m deal for Marouane Fellaini The window has closed but Sportsmail understands Everton and Manchester United have agreed a £27.5m deal for the transfer of Marouane Fellaini to Old Trafford




How do you feel now you’re a Manchester United player?

I’m very, very happy. It’s a big moment for me. I waited for a long time, I’ve worked hard for this and I’m very happy to join this big club, this great club. I hope to do everything for this club.
 

Attachments

  • cf7d18226b2ca4d431dc25dbed590efa.jpg
    cf7d18226b2ca4d431dc25dbed590efa.jpg
    16.6 KB · Views: 192
DONE DEALS (BIG NAME TRANSFERS):

REAL MADRID
- Gareth Bale (24) ametua Real Madrid kwa uhamisho wa £85.3m (REKODI YA DUNIA) kwa mkataba wa miaka 6. Atalipwa mshahara wa £300,000 kwa wiki. Kumbuka Christiano Ronaldo alisajiliwa na Real Madrid kwa dau la £80m.

ARSENAL

- Kiungo mchezeshaji anayeteleza Mesut Ozil (24) ametua Arsenal kwa mkatabawa miaka 5, kwa dau la £42.4m na mshahara wa £150,000 kwa wiki.
- Kipa Emiliano Viviano (27) ametua Arsenal kwa mkopo kutoka Palermo. Viviano anadakia pia timu ya taifa ya Italia.
- Kiungo Mathieu Flamini (29) amerejea Arsenal kutoka AC Milan kwa uhamisho huru. Flamini aliichezea Arsenal mwaka 2004 - 2008.
- Mshambuliaji Gervinho (26) ameuzwa AS Roma ya Italia kwa bei ya £8m.

CHELSEA
- Mshambuliaji kinda Romelu Lukaku (20) ameondoka tena, amehamia Everton kwa mkopo.
- Mshambuliaji Samuel Eto'o (32) ametua Chelsea kwa uhamisho huru kutoka Anzhi Makhachkala, kwa mkataba wa mwaka 1.
- Kiungo mshambuliaji Willian (25) ametua kwa uhamisho wa £30m kutoka Anzhi Makhachkala ya Urusi. Mkataba miaka 5.
- Kiungo Florent Malouda (33) ameondoka Chelsea kwenda Trabzonspor ya Uturuki kwa mkataba wa miaka 2.
- Mshambuliaji André Schürrle (22) kutoka Bayer Leverkusen ametua kwa dau £18m.
- Kiungo kinda Marco van Ginkel (20) ametua kutoka Vitesse Arnhem kwa dau la £8m.

LIVERPOOL
- Mshambuliaji wa Chelsea Victor Moses (22) amehamia Liverpool kwa mkopo wa msimu mmoja.
- Beki wa kati na kushoto Mamadou Sakho (23) ametua Liverpool kwa dau la £18m kutoka PSG.
- Beki wa kati Tiago Ilori (20) ametua Liverpool kutoka Sporting Lisbon kwa dau la £7m.
- mshambuliaji Iago Aspas (26) ametua kutoka Celta Vigo kwa dau la £7m.
- Golikipa Simon Mignolet (25) ametua kutoka Sunderland kwa dau la £9m.
- Beki Kolo Toure (32) ametua Liverpool kutoka ManCity.
- Kipa Pepe Reina (31) ameondoka Liverpool na kutua Napoli kwa mkopo. Anaungana tena na kocha Rafa Benitez.
- Mshambuliaji kinda Jonjo Shelvey (21) ameondoka Liverpool kwenda Swansea kwa dau la £5m.
- Mshambulaji Andy Carroll (24) amehamia West Ham kwa dau la £15.5m
- Mshambuliaji Fabio Borini (22) amehamia Sunderland kwa mkopo.

MANCHESTER CITY
- Beki Martin Demichelis (32) ametua ManCity kwa dau la £3.5m kutoka Atletico Madrid.
- Mshambuliaji Stevan Jovetic (23) ametua kwa dau la £22m kutoka Fiorentina.
- Mshambuliaji Alvaro Negredo (27) ametua kutoka Sevilla kwa dau £20m.
- Beki Maicon Douglas Sisenando (31) ameondoka ManCity kwenda AS Roma, baada ya kucheza mechi 13 tu tangu ajiunge na City.
- Kiungo mkabaji Fernandinho Luiz Roza (26) ametua kutoka Shakhtar Donetsk kwa dau la £30m.
- Kiungo Jesús Navas (27) ametua kutoka Sevilla kwa dau la £16m.

MANCHESTER UNITED
- Kiungo mshambuliaji Marouane Fellaini (25) ametua ManUtd kutoka Everton kwa dau la £27.5m.
 
- Wesley Sneijder(29) anayeichezea Galatasaray anawaniwa na Chelsea kwenye dirisha dogo. Anasema kocha wa Uholanzi Louis van Gaal.
- Mlinzi wa Chelsea David Luiz (26) atapigwa panga na kocha Jose Mourinho mwezi Januari kufuatia kiwango kisichoridhisha.
 
Javier Hernandez - Chicharito (25) huenda akatua Arsenal kwenye dirisha dogo kufuatia kukosa nafasi kwenye kikosi cha kwanza ndani ya ManUtd ingawa amekua akifanya kweli kila anapopewa nafasi.
 
Javier Hernandez - Chicharito (25) huenda akatua Arsenal kwenye dirisha dogo kufuatia kukosa nafasi kwenye kikosi cha kwanza ndani ya ManUtd ingawa amekua akifanya kweli kila anapopewa nafasi.

Chicharito ni mchezaji wa sub....inabidi atumike ivyo yani
 
Diego Costa: Kocha Arsene Wenger atatuma scouts kwenda kufuatilia kiwango cha Diego Costa wa Atletico Madrid katika mechi mbili zijazo ili kumsajili katika dirisha dogo kwa dau la £32m ambalo limeshapata baraka zote.
Kama kawaida tayari makocha wengine nao wameshaanza kumwania. Mara nyingi makocha husubiri Professor of Football aoneshe njia (... kama fisi vile).
Diego Costa ameshafunga mabao 22 katika mechi 21 alizocheza msimu huu, ikiwemo mabao 17 katika mechi 16 za La Liga.
Costa.jpg
 
- Wesley Sneijder(29) anayeichezea Galatasaray anawaniwa na Chelsea kwenye dirisha dogo. Anasema kocha wa Uholanzi Louis van Gaal.
- Mlinzi wa Chelsea David Luiz (26) atapigwa panga na kocha Jose Mourinho mwezi Januari kufuatia kiwango kisichoridhisha.

Karibu Barcelona David Luiz.
 
Mshambuliaji namba 1 duniani kwa sasa, Luis Suarez wa Liverpool amesaini mkataba mpya wa miaka minne na nusu kwa mshahara wa £200,000 kwa wiki. Hii itaongeza ugumu wa kumn'goa Anfield.
 
hatimaye DIRISHA DOGO la usajili linafunguliwa ambapo vilabu vinapata fursa ya kuweka sawa vikosi vyao kwa ajili ya kumalizia msimu wa 2013/14.
 
Mshambuliaji anayetisha duniani kwa sasa Diego Costa (25) wa Atletico Madrid anawaniwa na Arsenal, Chelsea na Borussia Dortmund. bei yake kwa sasa ni £35m. Diego Costa amefunga mabao 22 katika mechi 21 alizocheza msimu huu, ikiwemo mabao 17 katika mechi 16 za La Liga.
 
Beki wa kushoto anayepanda Leighton Baines (29) bado yumo kwenye rada ya kocha Davidd Moyes wa ManUtd ambaye ametenga dau la £16m kung'oa Everton Januari hii.
 
Mshambuliaji wa zamani wa ManUtd Ole Gunnar Solskjaer anakaribia kuukwaa ukocha wa Cardiff City ...
 
Mshambuliaji kinda wa Real Madrid Alvaro Morata (21) ameomba kuondoka Real ili akapate nafasi ya kucheza na kuonesha kipaji chake elsewhere. Anategemewa kutua Arsenal au Tottenham.
 
Real Madrid wamesema sasa wapo tayari kupokea ofa kutoka kwa timu zinazomtaka Morata KWA MKOPO TU. Mzee Wenger kwa sasa anaongoza mashambulizi ya kumchukua kinda huyo. Morata anategemewa kutua Emirates mwisho wa mwezi huu.
 
Diego Costa: Kocha Arsene Wenger atatuma scouts kwenda kufuatilia kiwango cha Diego Costa wa Atletico Madrid katika mechi mbili zijazo ili kumsajili katika dirisha dogo kwa dau la £32m ambalo limeshapata baraka zote.
Kama kawaida tayari makocha wengine nao wameshaanza kumwania. Mara nyingi makocha husubiri Professor of Football aoneshe njia (... kama fisi vile).
Diego Costa ameshafunga mabao 22 katika mechi 21 alizocheza msimu huu, ikiwemo mabao 17 katika mechi 16 za La Liga.
View attachment 127532

Akitua emirates mambo yatakuwa poa sana na nafas ya ubingwa itakuwa nyeupeeeee
 
Mshambuliaji kinda wa Schalke 04 Julian Draxler nae yumo kwenye rada ya Arsenal. Anaweza kung'olewa kwa dau lisilopungua £40m.
 
Kocha David Moyes amepewa kitita cha £150m kwa ajili ya usajili katika dirisha dogo. Tayari mshambuliaji wa PSG Edinson Cavani anatarajiwa kutua Old Trafford Januari hii. Pia, Adam Lallana, Ross Barkley na engine kibao watamwagiwa 'mtama' ndani ya wiki mbili zilizobaki.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom