Transfer Window updates 2013/2014 season - Europe

Transfer Window updates 2013/2014 season - Europe

Edgar Davids anaelekea mjini Milan kuwa kocha msaidizi wa AC Milan ambayo sasa inafundishwa na Mdachi mwenzake Clarence Seedorf.
 
Kocha David Moyes amepewa kitita cha £150m kwa ajili ya usajili katika dirisha dogo. Tayari mshambuliaji wa Monaco Edinson Cavani anatarajiwa kutua Old Trafford Januari hii.
pia, Adam Lallana, Ross Barkley na engine kibao watamwagiwa 'mtama' ndani ya wiki mbili zilizobaki.
Monaco ni radamel falcao....sidhani kama moyes anamweza
 
Juan Mata kutua ManUtd kwa ada ya £37m.
 
Arsenal inakamilisha usajili wa kiungo mkongwe mswedish Kim Kallstrom (31) kutoka Spartak Moscow kwa mkopo hadi mwisho wa msimu.
 
Mario Balotelli anatazamiwa kutua Arsenal msimu ujao baada ya agent wa Mario kukutana na kocha Arsene Wenger jana. Mario hafurahii ubaguzi wa rangi uliopo nchini Italia.
 
David Luiz (26) anakamilisha mipango ya kuhamia Barcelona msimu ujao. Bei yake kwa sasa ni £22million.
 
Kapteni na beki wa kutisha wa ManUtd Nemanja Vidic (32) atajiunga na InterMilan msimu ujao kama mchezaji huru.
 
Kocha mzoefu wa Uholanzi Van Gaal (62) ndiye atakayeinoa Tottenham kuanzia msimu ujao.
Van Gaal ameshawahi kuzifundisha Ajax, Barcelona, AZ Alkmaar na Bayern Munich kwa mafanikio makubwa na ameahidi kuinogesha zaidi EPL.
 
Van Gaal sasa yupo kwenye mazungumzo ya kuifundisha ManUtd, ni baada ya kuitolea nje Tottenham. Moyes kupigwa panga mwisho wa msimu.
 
Kocha David Moyes ametimuliwa ManUtd baada ya kuifundisha kwa miezi 10.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom