Trafic jamani punguza kupokea hongo

Trafic jamani punguza kupokea hongo

Calist

Senior Member
Joined
Dec 17, 2010
Posts
130
Reaction score
7
Hapa niko jirani na kituo cha trafic naendelea na shughuli zangu na trafic kama kawaida wanaendelea na kazi yao ya kukusanya hongo. Kila gari linalopita linasimama konda au tingo anatoa kitu kidogo safari inaendelea, magari mengine ni mabovu hata kwa kuyaangalia tu lakini wakishatoa wanaruhusiwa tu. Kwa mtindo huu ajari zitakwisha ? Sijui nichukue video yao kama J. Muro ingawa haisaidii kitu maana inaonekana hata wakubwa hapa wana mgao wao, kuwa wazalendo jamani.
 
Uko wapi?

Yupo barabarani..., Ukweli tutawalaumu bure kwani hali ya maisha ni mbaya kwa kila mtanzania na tumeoza kuanzia kichwa hadi vidoleni, hiyo rushwa ndugu yangu huenda kugawanwa na wakubwa zao na wasipofanya hivyo wako hatarini kupelekwa Mtimbira, kawaulize pale Chalinze walivyokosea tu wote wakapigwa PI ktk barabara maarufu
 
Hapa niko jirani na kituo cha trafic naendelea na shughuli zangu na trafic kama kawaida wanaendelea na kazi yao ya kukusanya hongo. Kila gari linalopita linasimama konda au tingo anatoa kitu kidogo safari inaendelea, magari mengine ni mabovu hata kwa kuyaangalia tu lakini wakishatoa wanaruhusiwa tu. Kwa mtindo huu ajari zitakwisha ? Sijui nichukue video yao kama J. Muro ingawa haisaidii kitu maana inaonekana hata wakubwa hapa wana mgao wao, kuwa wazalendo jamani.

Rushwa kuiondoa siyo jitihada za traffic. Umejiuliza kwa nini mtu anatoka na kushawishi kutoa RUSHWA? kuna tatizo katika mifumo yetu. Kama sumatra wamemupa route, kama TRA wamemupa lesseni ya biashara na gari lake bovu, unadhani polisi ataanzia wapi kukomesha hali hiyo? hizi taasisi zote, ni wehu tu, masaburi @ work every nukta, usitegemee ajali kuisha.

kuna OCD mmoja alisimamia sheria ya kupiga disco kusini mwa tanzania. aliyekuwa anapiga disco, alikuwa ni KOMBA. Mda ulipofika OCD akaeenda kumkumbusha mwisho wa makubaliano yetu 6 usiku, watu wakasema tunataka hadi majogoo, komba akamsihi amruhusu, OCD akagoma, komba akamwambia ukininyima ruhusa ya kukesha, iko sehemu nitaruhusiwa. Komba akapiga simu, akaruhusiwa na yule OCD kuamriwa kumlinda komba mpaka majogoo. Kulipokucha, OCD alifatwa na RPC wake kuwa anaitwa kwa mkuu wa mkoa, alipigwa transfer na kushushwa cheo hadi mshauri wa mgambo wilaya.

walioshikilia system wakiwa waovu, hata wanaoisaidia sysytem kuendelea kuwepo watakuwa waovu, hautapata msafi hata siku moja
 
Rushwa kuiondoa siyo jitihada za traffic. Umejiuliza kwa nini mtu anatoka na kushawishi kutoa RUSHWA? kuna tatizo katika mifumo yetu. Kama sumatra wamemupa route, kama TRA wamemupa lesseni ya biashara na gari lake bovu, unadhani polisi ataanzia wapi kukomesha hali hiyo? hizi taasisi zote, ni wehu tu, masaburi @ work every nukta, usitegemee ajali kuisha.

kuna OCD mmoja alisimamia sheria ya kupiga disco kusini mwa tanzania. aliyekuwa anapiga disco, alikuwa ni KOMBA. Mda ulipofika OCD akaeenda kumkumbusha mwisho wa makubaliano yetu 6 usiku, watu wakasema tunataka hadi majogoo, komba akamsihi amruhusu, OCD akagoma, komba akamwambia ukininyima ruhusa ya kukesha, iko sehemu nitaruhusiwa. Komba akapiga simu, akaruhusiwa na yule OCD kuamriwa kumlinda komba mpaka majogoo. Kulipokucha, OCD alifatwa na RPC wake kuwa anaitwa kwa mkuu wa mkoa, alipigwa transfer na kushushwa cheo hadi mshauri wa mgambo wilaya.

walioshikilia system wakiwa waovu, hata wanaoisaidia sysytem kuendelea kuwepo watakuwa waovu, hautapata msafi hata siku moja

Kwa kweli habari ndiyo hiyo. Mkuu wa kaya ndiyo bosi wa mabosi wanaosimamia hongo hizo. Hao wadogo wanapochukua hongo hupeleka mgawo kwa walioko juu. Angalia ngazi yao ya madaraka na vivyo hivyo hongo hizo huwafikia huko huko. Hii ni Tanzania na lazima ulielewe hilo. Vinginevyo kama una uchungu na nchi hii basi tukiitisha maandamano ya kuwaondoa madarakani hao wanaosimamia hongo/rushwa basi ujitokeze.
 
Yupo barabarani..., Ukweli tutawalaumu bure kwani hali ya maisha ni mbaya kwa kila mtanzania na tumeoza kuanzia kichwa hadi vidoleni, hiyo rushwa ndugu yangu huenda kugawanwa na wakubwa zao na wasipofanya hivyo wako hatarini kupelekwa Mtimbira, kawaulize pale Chalinze walivyokosea tu wote wakapigwa PI ktk barabara maarufu

Hakika, kuna mdau mmoja katoka BOTSWANA kimatembezi, alifanikiwa kuongea na askari wa cheo cha chini kabisa kule, akambiwa pesa anayolipwa askari wa chini kabisa, ambapo pesa zile kwa pesa yetu ni sawa na 1,800,000/- sasa katika mazingira haya, nani atachukua rushwa? halafu kiburi cha botswana ni diamond na gold pekee, ambapo mwekezaji 50% ya mrahaba huku akiwajibika kulipia vitu vingine kama kodi, lesseni na mambo kibao.

Tanzania tuna zaidi yao karibia mara 100. tuna gold, diamond, uranium, coal, tanzanite, rubi, chuma na mengine siyajui jina, lakini mrahaba wetu asilimia 1-5% matokeo yake mishahara kwa watumishi wa umaa 150,000/-300,000/= kwa wale wenye kataaluma ka shahada.

Katika mazingira haya, ukiangalia na mfumuko wa bei, mtu mwenye familia ataishije? akiwa na nafasi ya kupokea mlungula, lazima atapokea.

waliopewa uongozi wakiwa waovu, usitegemee watendaji wa chini kuwa safi, ni rushwa kwenda mbele ili mwezi uishe salama

 
Kwa kweli habari ndiyo hiyo. Mkuu wa kaya ndiyo bosi wa mabosi wanaosimamia hongo hizo. Hao wadogo wanapochukua hongo hupeleka mgawo kwa walioko juu. Angalia ngazi yao ya madaraka na vivyo hivyo hongo hizo huwafikia huko huko. Hii ni Tanzania na lazima ulielewe hilo. Vinginevyo kama una uchungu na nchi hii basi tukiitisha maandamano ya kuwaondoa madarakani hao wanaosimamia hongo/rushwa basi ujitokeze.

inahitaji uelimishaji wa hali ya juu sana. Jana nilikuwa na dereva tax, alikuwa ananipeleka hospitali, wife anaumwa, yeye akaanza kuwaponda waarabu eti wamezidi. Mwisho akasema, mie siwezi kuandamana eti nadai fulani atoke, aingie fulani kwani wote lao moja.

nilimjibu nikamwambia siku ukielewa siasa ni nini na kazi yake ni nini, utaingia mtaani kudai uhuru wako. Babu zetu hawakuwa wajinga kuwatimua wakoloni pamoja na kuwa na risasi za moto, Marekani leo kila mtu anatamani kwenda, kwa kuwa Martin Luther king jr, alikubali kufa kwa kuandaa mazingira ya hawa wanaokimbila leo marekani waende bila kubaguliwa. Ukiwa mbinafsi, huwezi kushiriki, lakini wanao watakuja kukuhoji, umetuachia nini cha maana zaidi ya mikataba mibovu, maisha duni, kusoma kwenyewe shule za kata mwl. mmoja na mtatizo kibao, atakulaumu sana.

Kidogo akaanza kunielewa

 
Uko wapi?

Niko Iringa au unataka kujua Iringa sehemu gani? Sasa hivi ndio anapokea mkwanja kwenye bus moja mkweche unatoka kijijini umeshona abiria kibao. Kama vile walishapangiana kiasi maana wafika wanatoa sent wanaondoka hakuna kuulizana.
 
Cha ajabu wakiona DFP, ST, au gari ya mwarabu wanaangalia pembeni, kama hii kusanya kusanya ingekuwa haiendi hadi kwa wakubwa hawa wadogo wangekuwa wanakamatwa kirahisi muno, we kamanda wa Iringa hebu jaribu kushtukiza sasa hivi halafu wakague hao walioko barabara zinazoingia Iringa mjini uone kila mmoja ana shs ngani na kazipata wapi, saa hizi.
 
Ukitaka utamu wa Askari hawa na wasikupe shida toka Bukoba hadi Songea wee tafuta na nunua pesa bandia za Tsh 10,000/=, kila wakikusimamisha toa aione kidogo halafu ikunjekunje kwa sanaaaa halafu naye ataipokea haraka haraka na kuificha tena walivyo huwa hawapendi wenzie wajue kuwa hapo imetoka u..ten ili baadaye awazime, jioni wee umeshafika safari yako yeye anafunga mahesabu au anaagiza bia basi hapo ndio msala unakuwa wake
 
Cha ajabu wakiona DFP, ST, au gari ya mwarabu wanaangalia pembeni, kama hii kusanya kusanya ingekuwa haiendi hadi kwa wakubwa hawa wadogo wangekuwa wanakamatwa kirahisi muno, we kamanda wa Iringa hebu jaribu kushtukiza sasa hivi halafu wakague hao walioko barabara zinazoingia Iringa mjini uone kila mmoja ana shs ngani na kazipata wapi, saa hizi.

hayo ni magari ya serikali, haywezi kukamatwa labda kuwa na ulazima wa kuyakamta. Halfu mengi hayana makosa kama yalivyo magari ya kiraia
 
Ukitaka utamu wa Askari hawa na wasikupe shida toka Bukoba hadi Songea wee tafuta na nunua pesa bandia za Tsh 10,000/=, kila wakikusimamisha toa aione kidogo halafu ikunjekunje kwa sanaaaa halafu naye ataipokea haraka haraka na kuificha tena walivyo huwa hawapendi wenzie wajue kuwa hapo imetoka u..ten ili baadaye awazime, jioni wee umeshafika safari yako yeye anafunga mahesabu au anaagiza bia basi hapo ndio msala unakuwa wake

kuna wengine wana machale, watakukamata nazo halafu ubaki na kesi ya kumiliki noti bandia. Kuna jamaa alifanya kama ulivyosema, alaikuwa ana noti za 6,000,000/-, kwalambisa askari wengi alipofika mahali fulani akashitukiwa, mpaka sasa yko gerezani. ni mshikaji namfahamu sana
 
Rushwa kuiondoa siyo jitihada za traffic. Umejiuliza kwa nini mtu anatoka na kushawishi kutoa RUSHWA? kuna tatizo katika mifumo yetu. Kama sumatra wamemupa route, kama TRA wamemupa lesseni ya biashara na gari lake bovu, unadhani polisi ataanzia wapi kukomesha hali hiyo? hizi taasisi zote, ni wehu tu, masaburi @ work every nukta, usitegemee ajali kuisha.

kuna OCD mmoja alisimamia sheria ya kupiga disco kusini mwa tanzania. aliyekuwa anapiga disco, alikuwa ni KOMBA. Mda ulipofika OCD akaeenda kumkumbusha mwisho wa makubaliano yetu 6 usiku, watu wakasema tunataka hadi majogoo, komba akamsihi amruhusu, OCD akagoma, komba akamwambia ukininyima ruhusa ya kukesha, iko sehemu nitaruhusiwa. Komba akapiga simu, akaruhusiwa na yule OCD kuamriwa kumlinda komba mpaka majogoo. Kulipokucha, OCD alifatwa na RPC wake kuwa anaitwa kwa mkuu wa mkoa, alipigwa transfer na kushushwa cheo hadi mshauri wa mgambo wilaya.

walioshikilia system wakiwa waovu, hata wanaoisaidia sysytem kuendelea kuwepo watakuwa waovu, hautapata msafi hata siku moja
hatari hatari zaidi ya umeme

 

Similar Discussions

Back
Top Bottom