"Traffic" Nunua gari yako upande

"Traffic" Nunua gari yako upande

Haaa nyie hamjui traffic police walivyo washenzi, mimi simpi lift labda aniombe, kuna siku nilikuwa natoka bagamoyo Polisi aliomba lift nikampa lakin mle ndani tulikuwa na jamaa yangu tunakula samaki na mazagazaga mengine tukamnyima shenzi

Hahahahahahahaaa, mmenichekesha balaa, eti ..."tukamnyima", mna umri gani we na jamaa zako? Kwa hiyo alivyoingia kwenye gari aliomba na samaki au ilikuwaje mpaka "mkamnyima'...lol!
 
Sio jibu zuri hasa kwa tamaduni zetu za kiafrica, wenzetu wa ulaya hilo jibu ni la kawaida sana kwao maana hawana umoja kama sisi.
 
Lala tu ila kesho uje kujibu tuhuma za kumpa hongo mtumishi wa uma, kitendo kinachotafsiriwa kama kumziba mdomo ili siku ukicommit crime barabarani akuoffend!

Akicommit crime amuoffend?!!!! Au am defend??!!
 
Hahahahahahahaaa, mmenichekesha balaa, eti ..."tukamnyima", mna umri gani we na jamaa zako? Kwa hiyo alivyoingia kwenye gari aliomba na samaki au ilikuwaje mpaka "mkamnyima'...lol!

Jamaa kanikumbusha shule ya msingi ukinyimwa mihogo na rafiki yako, inaumaa!
 
Jamaa kanikumbusha shule ya msingi ukinyimwa mihogo na rafiki yako, inaumaa!

Kuna mwanafunzi mwenzetu mama yake alikuwa mama lishe karibu na shule yetu....basi dogo daily alikuwa anafungashiwa njugu mawe ili apate staftahi mapumziko ya saa nne...tulimwoneaje gere!
 
Sio jibu zuri hasa kwa tamaduni zetu za kiafrica, wenzetu wa ulaya hilo jibu ni la kawaida sana kwao maana hawana umoja kama sisi.

Nani kakwambia ulaya hawapeani lift? Nchi zilizoendelea gari ni kitu cha kawaida sana, ukikuta mfanyakazi anaenda kazini kwa mguu ujue ameamua, wengi wanatumia usafiri wa umma na baiskeli kuepuka foleni na kupunguza matumizi yasiyo ya msingi. Sisi gari ni kama ng'ombe kwa mmasai, ni alama ya wealth, mtu akiwa na funguo ya gari hataki hata kuitia mfukoni, full time mkononi na masimu yake mawilimawili kama hana mifuko!
 
Kuna mwanafunzi mwenzetu mama yake alikuwa mama lishe karibu na shule yetu....basi dogo daily alikuwa anafungashiwa njugu mawe ili apate staftahi mapumziko ya saa nne...tulimwoneaje gere!

Duh, kwa njugumawe mbichi za kuchemsha hata mimi ningebembeleza urafiki!
 
Na urafiki wenyewe unakufa sku hiyohiyo...."we mchoyo sana", shuleni mpaka barafu tunang'atiana!

Utoto raha sana! Anang'ata ashkrimu halafu anakutemea mkononi na wewe unaila tu bila wasiwasi!
 
Nani kakwambia ulaya hawapeani lift? Nchi zilizoendelea gari ni kitu cha kawaida sana, ukikuta mfanyakazi anaenda kazini kwa mguu ujue ameamua, wengi wanatumia usafiri wa umma na baiskeli kuepuka foleni na kupunguza matumizi yasiyo ya msingi. Sisi gari ni kama ng'ombe kwa mmasai, ni alama ya wealth, mtu akiwa na funguo ya gari hataki hata kuitia mfukoni, full time mkononi na masimu yake mawilimawili kama hana mifuko!


Lifti watu wanapeana ulimwenguni kote ila kwa ulaya nitofauti sana na africa, mtu hawezi akawa anategemea lifti yako wakati miundo mbinu ya mabasi ya umma iko vizuri, nilikua nalenga hasa hasa upande wa kitu kinaitwa "selfishness" hiki kitu kibaya sana na kimeanza kuingia kwetu pia. Wazungu wanacho mda mrefu ndio maana stress level zao na zetu hazifanani, sie waafrica tunapendana sana na kusaidiana.
 
Back
Top Bottom