TRA 'wambana' Dk Slaa

Dkt Willbrod Slaa huwa hakurupuki bila ushahidi wa uhakika lazima hapo pana ufisadi ndani yake pengine ktk hizo bilioni 80 huyu Luoga anazo zake 40.Pili ktk habari hii mwandishi kakurupuka maana kichwa cha habari hakiendani na habari sambamba maana sioni mahali TRA wamembana Dkt wa ukweli Willbrod Slaa.
Nimelipa kodi TRA kwa miaka 4 ktk biashara yangu na cha kushangaza mwaka wa tano wameniambia nilikuwa nnaiibia Serikali pesa sbb ikiwa aliekuwa akikadiria alikosea.Sasa Kama ni kweli nilikuwa nikiibia Serikali mapato nnahusika vp hapo kwani kodi zote nimezilipa ktk ofisi zao?
 
Issue ya uplifting ukiagiza kijigari chako japan is disgusting. I used to respect tra but since such horrible thing happened to me naona km genge tu la wakusanya ushuru tena unfairly. Hata ukiwapa documents za email how u negotiated with the vendor na invoice hawakuelewi. sanasana wakishaup lift wanakaa kimya na documents hazi move tena utajijua kwenye storage/demurrage charges. Since then najiuliza hawa ma assessors/ valuers wa tra wamesoma vyuo gani au ndo wale wanagraduate na gentlemen gpas. Next time nikipata vijisent napitishia gari yangu Mombasa and am not being unpatriotic!
 

Ha ha ha haaaa mzee wa watu Slaa amelishwa kasa tena na wajanja wa mjini , sijui lini ataacha kujiabisha namna hii
 

Naunga mkono.
 
wapenda anasa wametajwa kinawauma sana,matanuzi mtaani hatunywi maji,watu hawana amani na ndoa zao kisa wafanyakazi wa TRA,maana hawa jamaa kama mke wa mtu ni mzuri wanakunyang'anya,dhambi ilioje

Kwa hilo mie sina tatizo nalo kwani popote pale nikisikia tu huyu au yule ni mke wa mfanyakazi wa TRA basi kwishney, kwa gharama zozote zile na alhamdulilah wengi wao si wabaya kama waume zao wanavyotufanyia pale long room
 
hilo tamko limetolewa na nani? na ni vyombo vingapi vya habari vilihusishwa?
I mean hii habari inaelea elea tuu!!
huu ni usanii mtupu toka kwa taasisi nyeti kama tra..
binafsi nawaelewa sana hawa: ni mafisadi waliokubuhu!!
 
Eti 'kuchafua heshima ya mamlaka ya mapata'.
Hii imenichekesha sana, heshima ipi? Misamaha holela ya kodi kwa wageni au heshima ipi- chukua chako mapema au heshima ipi?
Najisikia kuweweseka na hii heshima ambayo inadaiwa kuchafuliwa.
 
akitoa ushahidi wao watawajibika vipi? watajiudhuru na kukubali kufilisiwa?
kwa nini wao hawataki kujisafisha kwa kusema nini hasa kilitokea,
hii nayo ni aina ya upuuzi hapa TANZANIA ndio kichaka chao cha kujificha siku hizi
sisi wananchi Dr Slaa tunamsoma
MIMI NINA HAKIKA SIKU DR SLAA akiongopa kama wao wanavyodai na wakajua kadanganya kesi itafunguliwa haraka sana
na hivi vyombo vya serikali, maana mtu wanayetaka kumuona JELA kwa sasa ni Dr Slaa (most wanted )



 
hilo tamko limetolewa na nani? na ni vyombo vingapi vya habari vilihusishwa?
I mean hii habari inaelea elea tuu!!
huu ni usanii mtupu toka kwa taasisi nyeti kama tra..
binafsi nawaelewa sana hawa: ni mafisadi waliokubuhu!!

ndo maana asubui nkasema sasa TRA imekuwa chama kipya cha siasa,uksoma wananchi utaona upeo mdogo wa mleta habari!
 
TRA Ni waongo na wazushi wakubwa tena kutumia kodi za watanzania kuandika uongo ni ufisadi mwingine.

N a wana JF hebu tujenge utamaduni wa kusoma ripoti mbalimbali zinazowekwa hapa , kuhusu ufisadi wa Luoga na TRA CAG ALISEMA HIVI;

RIPOTI YA MDHIBITI NA MKAGUZI MKUU WA
HESABU ZA SERIKALI KUHUSU TAARIFA ZA
FEDHA ZA SERIKALI KUU KWA MWAKA​
ULIOISHIA TAREHE 30 JUNI, 2010

•​
Malipo ya fidia isiyostahili kwa kampuni ya TANGO
Limited Sh.554,464,133

Kiasi cha Shs.554,464,133.60 kililipwa kwa M/S Tango
Transport Limited (Verani Tango) kama fidia kwa
mujibu wa hati za Magari yake zilizodaiwa
kuchukuliwa na maafisa wa TRA mwaka 1997 kwa
muda wa siku tisini (90). Hata hivyo, mapungufu
yafuatayo yalibainishwa:
i. Mrejesho ya Shs.53,650,151 yaliambatanishwa na
hati ya kukiri mapokezi ambayo uhalisi wake
haukuthibitishwa. Aidha, kiasi hiki kililipwa mara
mbili, wakati awamu ya kwanza malipo yalifanywa
kwa amri ya mahakama.
ii. Malipo ya Sh.6,788,840 hayakuhusiana na madai ya
msingi
iii. Malipo ya riba ya Shs.554,464,133.60 yalifanyika​
kwa ‘compound interest” badala “simple interest”.

SASA WANAPOSEMA HAWAJAWAHI KULIPA KIASI HICHO NA HAWANA KUMBUKUMBU KAMA KUNA KESI YA TANGO TRANSPOTERS WANAMAANISHA NINI?

NTAREJEA.
 
Ha ha ha haaaa mzee wa watu Slaa amelishwa kasa tena na wajanja wa mjini , sijui lini ataacha kujiabisha namna hii

Degraded you by 150%....i thought ur a gentleman. Hebu tupe ushahidi wako....!!!!
 
Kifupi nawaambia kuwa hii itakuwa aibu kubwa sana kwa TRA kwani wameingia kwenye mtego wenyewe, nalifahamu hili suala niliwahi kushirikishwa na Dr.Slaa.

Ni aibu ya mwaka na nawaambia kuna hukumu inaonyesha kuwa Veran alipwe fidia ya 800 bilioni ,na hata malipo yaliyofanywa najua effort za Dr.Slaa akiwa mbunge aliandika barua nyingi sana na nyingi zilijibiwa na Luoga mwenyewe na hata mwanasheria mkuu wa serikali wakati huo Mwanyika amewahi kujibu na hata waziri mkuu pinda amejibu kwa maandishi sasa TRA wamenasa, wait u shall see.
 
Imefafanua kuwa kumbukumbu zilizoko TRA zinaonyesha kuwa kampuni ya Tango Transport ni ya Arusha na kusisitiza kwamba hakuna taarifa zinazoeleza kuwa TRA imewahi kukamata magari ya kampuni hiyo kwa miaka 10.

Nawaambia magari yalikamatwa , kama hawajakamata waseme milioni 554 zilizohojiwa na CAG ni za kazi gani?

wanapaswa kujipanga upya na hapa nafikiri kuna kesi ya Dr.Slaa kukashifiwa na TRA na kwa sababu hawa wana pesa za kumlipa fidia sio vibaya akafa nao kwa mara ya kwanza mahakamani.
 

mimi binafsi sioni kazi zenu zinaendaje watoza ushuru nyie mnashibisha matumbo yenu
 
TRA ni taasisi kubwa nchini na ina wanasheria wazuri. Kama inaona imechafuliwa, kwa nini wasifungue mashitaka dhidi ya Dr. Slaa?
Jamani yaani siku hizi Bongo ukikashifiwa suluhu ni kumuomba aliyekuchafua aweke mambo wazi kwa wananchi na si kwenda mahakamani. Sasa aeleze umma mara ngapi kuwa kuna ufisadi?

Kwa mtazamo wangu: Kama umechafuliwa na ukashindwa kwenda mahakamani wakati una haki ya kwenda mahakamani kutoa malalamiko yako, basi nina-assume kuwa uko GUILTY.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…