Bususwa
JF-Expert Member
- Sep 30, 2021
- 429
- 1,011
Nimekuwa mfanyakazi wa kampuni moja kubwa sana hapa Dsm kwa zaidi ya miaka Saba sasa, baadae nilipelekwa mkoani kwaajili ya kazi yangu hiyo hiyo,hapa sitataja Mkoa kwa sababu ya kuficha uhusika wangu kamili.
Hii kampuni imekuwa na mambo ya ajabu sana, tumeajiriwa kwa jina la kampuni x, lakini pesa zote zinapelekwa na kuwekwa kwenye kampuni, hii kitu niliwahi kuhoji kwenye vikao vya management, nikaishia kutishiwa kufutwa kazi! Hii Kampuni inafanya kazi ya kuuza bidhaa jamii ya chakula, Mkurugenzi wetu kwa kusaidiana na Mkuu wa fedha, wamekuwa wakisema tusitoe list ya EFD, hii itasaidia wao kukwepa kodi!
Niliwahi kuuliza iweje niwe na Mauzo ya Tshs 200,000,000 lakini EFD machine yangu inasoma Tshs 30,000,000 nilijibiwa kama hutaki kazi endelea kuwa unaingia kila Mauzo kwenye EFD machine, sababu na Mimi nina familia niliamua kukaa kimya!
Pia hii kampuni imeajiri watu kutoka jamii ya Asia, wakati hizi kazi wanazofanya wao hata sisi wazawa tunaweza kuzifanya bila shida yoyote kabisa! Watu wa UHAMIAJI mko WAPI?? Watu wa idara ya kazi mko WAPI?? Hawa wahindi wanatudharau sana sisi wazawa na baadhi ya wazawa wapo pamoja na hawa wahindi
Mhindi anafanya kazi analipwa Tshs 30,000,000,mzawa ambaye ndizo mzalishaji Mkubwa analipwa Tshs 500,000!
Mmiliki wa hii Kampuni kuna wakati hua anatuita sisi mbwa! Yaani anasema kabisa wewe Mbwa hebu njoo hapa.
Tatu hii Kampuni ilikuwa inaitwa kampuni x zamani,lakini wakaja wakauza kihuni na kuipa jina la kampuni y,hapo wataalum wa kodi mnaweza kujua kabisa kwamba,walikwepa hapa,ili waweze kupiga pesa!
Watu wa TAKUKURU hii Kampuni mkifanya kazi kwa undani kabisa, mtakuta kuna madudu mengi sana hapa, niliwahi report hili suala kwa moja ya wafanyakazi wa TAKUKURU sijui hili jambo liliishia wapi,hadi leo ni kimya kweli na watu wanazidi kufukuzwa kazi kwa sababu zisiso na misingi!
Mhindi anasema kabisa kama, watanzania wenzeni wanashindwa kuwasaidia sisi tutawasaidia vipi? Nenda kwetu kama utakuta Bwana Fedha wa kampuni ya India ni mtanzania, sana sana atakua anapiga deki kwenye vyoo tu huko!
Watu wa UHAMIAJI, TAKUKURU na TRA nipo tayari kutoa ushahidi wa kila kitu,kama tu mtakuwa tayari kunihitaji popote pale nitakuja.
Asanteni sana
Hii kampuni imekuwa na mambo ya ajabu sana, tumeajiriwa kwa jina la kampuni x, lakini pesa zote zinapelekwa na kuwekwa kwenye kampuni, hii kitu niliwahi kuhoji kwenye vikao vya management, nikaishia kutishiwa kufutwa kazi! Hii Kampuni inafanya kazi ya kuuza bidhaa jamii ya chakula, Mkurugenzi wetu kwa kusaidiana na Mkuu wa fedha, wamekuwa wakisema tusitoe list ya EFD, hii itasaidia wao kukwepa kodi!
Niliwahi kuuliza iweje niwe na Mauzo ya Tshs 200,000,000 lakini EFD machine yangu inasoma Tshs 30,000,000 nilijibiwa kama hutaki kazi endelea kuwa unaingia kila Mauzo kwenye EFD machine, sababu na Mimi nina familia niliamua kukaa kimya!
Pia hii kampuni imeajiri watu kutoka jamii ya Asia, wakati hizi kazi wanazofanya wao hata sisi wazawa tunaweza kuzifanya bila shida yoyote kabisa! Watu wa UHAMIAJI mko WAPI?? Watu wa idara ya kazi mko WAPI?? Hawa wahindi wanatudharau sana sisi wazawa na baadhi ya wazawa wapo pamoja na hawa wahindi
Mhindi anafanya kazi analipwa Tshs 30,000,000,mzawa ambaye ndizo mzalishaji Mkubwa analipwa Tshs 500,000!
Mmiliki wa hii Kampuni kuna wakati hua anatuita sisi mbwa! Yaani anasema kabisa wewe Mbwa hebu njoo hapa.
Tatu hii Kampuni ilikuwa inaitwa kampuni x zamani,lakini wakaja wakauza kihuni na kuipa jina la kampuni y,hapo wataalum wa kodi mnaweza kujua kabisa kwamba,walikwepa hapa,ili waweze kupiga pesa!
Watu wa TAKUKURU hii Kampuni mkifanya kazi kwa undani kabisa, mtakuta kuna madudu mengi sana hapa, niliwahi report hili suala kwa moja ya wafanyakazi wa TAKUKURU sijui hili jambo liliishia wapi,hadi leo ni kimya kweli na watu wanazidi kufukuzwa kazi kwa sababu zisiso na misingi!
Mhindi anasema kabisa kama, watanzania wenzeni wanashindwa kuwasaidia sisi tutawasaidia vipi? Nenda kwetu kama utakuta Bwana Fedha wa kampuni ya India ni mtanzania, sana sana atakua anapiga deki kwenye vyoo tu huko!
Watu wa UHAMIAJI, TAKUKURU na TRA nipo tayari kutoa ushahidi wa kila kitu,kama tu mtakuwa tayari kunihitaji popote pale nitakuja.
Asanteni sana