jojipoji koromije
JF-Expert Member
- Mar 22, 2017
- 991
- 1,412
Soko la mwanjelwa mkoani Mbeya ni kama Soko la Kariakoo kwa Dar es Salaam!! Ni kama Business District. Biashara ya mabilioni ya Shilingi inafanyika hapa kilasiku! Lakini kwa uchunguzi wangu wafanyabiashara hawa hawatoi kabisa risiti za EFD!
Nimeingia sokoni hapo zaidi ya Mara tatu kufanya manunuzi hawa jamaa utadhani hawajawahi kuambiwa wanapaswa kutoa risiti hizi. Ni aibu kwa TRA na Serikali kushindwa Kukusanya kodi kwenye biashara za mabilioni hapa MWANJELWA na kung’ang’ania kuwawekea TOZO kali kwenye Miamala ya simu wananchi wa kawaida kabisa wasio na kipato!
Serikali na bunge mmekosa ubunifu kabisa wa kukusanya kodi halali kabisa na mmebaki kumkaba kabali ya MBAO mwananchi Masikini.
Acheni hizo, futeni hayo matozo fuatilieni kodi halali zinazopotea bure hapa MWANJELWA Mbeya, Tunduma na Kariakoo.
Nimeingia sokoni hapo zaidi ya Mara tatu kufanya manunuzi hawa jamaa utadhani hawajawahi kuambiwa wanapaswa kutoa risiti hizi. Ni aibu kwa TRA na Serikali kushindwa Kukusanya kodi kwenye biashara za mabilioni hapa MWANJELWA na kung’ang’ania kuwawekea TOZO kali kwenye Miamala ya simu wananchi wa kawaida kabisa wasio na kipato!
Serikali na bunge mmekosa ubunifu kabisa wa kukusanya kodi halali kabisa na mmebaki kumkaba kabali ya MBAO mwananchi Masikini.
Acheni hizo, futeni hayo matozo fuatilieni kodi halali zinazopotea bure hapa MWANJELWA Mbeya, Tunduma na Kariakoo.