Vyote viwili ROAD LICENCE NA
FIRE INSPECTION sio kodi bali ni adhabu ya kumiliki gari TANZANIA.
Lakini kwa vile tumelogwa na mlogaji wetu alikufa hatuna mtu wa
kutuzindua tutaendelea kuumizwa hivi hivi,bunge letu tukufu lililidhia
wizi huu.
kama kila litre ya mafuta niwekayo kwenye gari langu ina tozo rasmi kwa
wenye gari kwa ajili ya road fund,the road licence ni ya nini ? Fire
inspection ili kiwe nini ? fire wameamua kujitafutia kipato toka kwa
wenye gari, kwa nini nilazimishwe kukata bima ya gari na nilizamishwe
kununu fire extinguisher ? kama bima ni pamoja na gari ikiungua kwa nini
iwe lazima kwa mimi kuweka kifaa cha kuzimia moto na si kwamba hicho
kifaa kitolewe na kampuni ya bima ambayo inataka kupunguza risk kwa
ajili ya moto ?
Kwa kweli wigo wa rushwa kwa trafiki wetu unapanuliwa kila iitwapo
leo.
Huu ni wizi mwingine, mchana kweupe,kuna hitajika juhudi, wabunge wetu wasaidie katika kupinga hili, kwani insurance tunayokata ina cover moto pia.
Hiyo ndiyo Tanzania ndugu yangu, Kila sehemu watu wanajitafutia ulaji; hizo hela zinaishia kunenepesha wakubwa hapo Wizara ya Mambo ya Ndani ambayo imeanzisha kitengo kinachojitegemea cha jeshi la zimamoto na hela zote zinachukuliwa na hilo jeshi.
TRA Mwanakula kamisheni ya ukusanyaji lakini kimsingi huo ni wizi ama unyang'anyi wa wazi kwani hakuna huduma yoyote inayotolewa na jeshi hilo kutokana na malipo. Wakati Masha akiwa waziri wa wizara hiyo alikataa kuidhinisha ukusanyaji wa malipo hayo kwani kimsingi madhara ama hasara inayotokana na ajali ya moto kwa chombo cha moto kama gari yanalipwa na bima.
Kama una bahati mbaya basi ni wewe! Mkuu huna mbunge wewe! Hawa jamaa wakiingia tu bungeni kitu ya kwanza wanahongwa gari! Watakukumbuka wewe? 40,000 kwao issue ndogo sana! Kikao kimoja tu wanalipa kila kitu! Why worry about Eeka Mangi with his/her Volkswagen beetle inherited from his grandfather? Walisema MWENYE KUSHIBA HAMJUI MWENYE NJAA.
We need a very serious government. Mtanisamehe sana ila what I believe its totally different. Niliwahi kuwinda na wale jamaa Wahadzabe kule Mang'ola! Wale jamaa wanatoka kwenda kuwinda amini usiamini wakipata tu hupekecha moto na kuchoma kile walichokipata then huwapelekea mabaki kama sio ngozi! Viongozi wenu wana utapia mlo mpaka washibe ndo wawakumbuke. Tunahitaji viongozi wasio na utapia mlo!
Nilipokumbana na hilo nikalilia taifa langu kwanza ndo nikalipa?Wangekuwa wanatoa hata mtungi ingekuwa sio wizi mbaya lakini kwakuchukua elfu 30 na ukienda fire wanataka kumi yakukagua mtungi nchi imeelaaniwa.
hili swala ni kama la NSSF tu.......ni Tanzania tu inayo,Kenya hakuna,Uganda hakuna,Rwanda na Burundi hakuna,kwa wenzetu ukilipia road licence ndo umemaliza kila kitu.
Mimi ni mtanzania mwenye ki tipa cha mchanga.
Kwa kifupi kwenye kioo cha mbele panatakiwa pawe na stika zifuatazo kwa mwaka:
1.Road Licence 240,000.00
2.Bima 120,000.00
3.Manispaa 10,000.00
5.Sumatra 10,000,00
6.TRA Mapato 520,000.00 (hii wanaruhusu kulipa hata kwa instalment)
7.Wiki ya Nenda kwa Usalama 7,000.00
Yaani kioo changu kejaa vistika hadi nashidwa kuona mbele sawasawa!
Wadau,
Wiki iliyopita nilikwenda pale TRA Mwenge kulipia road licence. Nilipokewa vizuri na mabinti pale reception na baada ya kuwaeleza shida yangu, walinisaidia kujaza form zinazotakiwa na kunielekeza wapi niende kwa ajili ya kukadiriwa ni kiasi gani nilipashwa kulipia. Kulingana na CC ya gari nililokwenda kulipia road licence, gharama yake ni Tshs. 150,000. Cha ajabu yule binti aliniandikia nikalipie Tshs. 180,000 na nilipomuuliza kwa nini kiasi hicho akaniambia Tshs. 30,000 zilizoongezeka hapo ni kwa ajili ya fire inspection. Nikamuuliza hiyo fire inspection ni kitu gani na nani anafanya hiyo inspection. Akaniambia inspection inafanywa na watu wa fire ambao ofisi zao ziko pale Lumumba na akasisitiza kwamba nikija kuchukua hiyo road licence nitaona na kupewa maelekezo zaidi.
Bahati mbaya sikuwa na kiasi chote hicho hivyo nililazimika kuondoka kwenda kutafuta pesa zaidi ili niweze kulipia. Pamoja na usumbufu nilioupata kuipata hiyo road licence, bado sikupewa kitu chochote kinachoonyesha kwamba nimelipia hiyo fire inspection.
Kama kuna mwana JF anayejua hii kitu ya fire inspection inafanyaje kazi, naomba atufumbue macho.
Natanguliza shukrani.
Tiba
Siyo kwenye magari tu,saivi wamehamia kwenye maduka na pikipiki ambapo wameanzisha kulipia fire extungisher yan ni wizi mtupu
Wadau,
Wiki iliyopita nilikwenda pale TRA Mwenge kulipia road licence. Nilipokewa vizuri na mabinti pale reception na baada ya kuwaeleza shida yangu, walinisaidia kujaza form zinazotakiwa na kunielekeza wapi niende kwa ajili ya kukadiriwa ni kiasi gani nilipashwa kulipia. Kulingana na CC ya gari nililokwenda kulipia road licence, gharama yake ni Tshs. 150,000. Cha ajabu yule binti aliniandikia nikalipie Tshs. 180,000 na nilipomuuliza kwa nini kiasi hicho akaniambia Tshs. 30,000 zilizoongezeka hapo ni kwa ajili ya fire inspection. Nikamuuliza hiyo fire inspection ni kitu gani na nani anafanya hiyo inspection. Akaniambia inspection inafanywa na watu wa fire ambao ofisi zao ziko pale Lumumba na akasisitiza kwamba nikija kuchukua hiyo road licence nitaona na kupewa maelekezo zaidi.
Bahati mbaya sikuwa na kiasi chote hicho hivyo nililazimika kuondoka kwenda kutafuta pesa zaidi ili niweze kulipia. Pamoja na usumbufu nilioupata kuipata hiyo road licence, bado sikupewa kitu chochote kinachoonyesha kwamba nimelipia hiyo fire inspection.
Kama kuna mwana JF anayejua hii kitu ya fire inspection inafanyaje kazi, naomba atufumbue macho.
Natanguliza shukrani.
Tiba