TRA, kwanini ni wagumu sana kuwatoa Walipakodi kwenye VAT & E-filling?

INSIDER MAN

JF-Expert Member
Nov 7, 2018
1,736
15,856
Leo nitabase na walipakodi binafsi/ Individual taxpayers (Presumptive ). Kuna jambo ambalo nafikiri ni kilio kwa wengi ila wanakosa mahali pakusemea. Ukweli hili jambo TRA mliangalie ni namna gani mtaweza kulitatua.

Mlipakodi akifikisha mauzo ya milion 100 mnamsajili na VAT na pia mnamwambia afanye self assessment. Nashindwa kutambua ni sheria ipi ambayo inamlazimisha mlipakodi kufanya online self assessment (e-filling)?. Point yenu ni kwamba mteja akifika hayo mauzo anatakiwa kusajiliwa na VAT na kuanza kutuma return za VAT hivyo anakua account case, na pia afanye self assessment online. Kumbuka unavofanya self assessment kwenye huu mfumo itabdi uandae hesabu yaani financial statements.

Tunatambua TRA mnania njema na Taifa hasa katika makusanyo ya kodi na pia mnafata sheria Vat Act, 2014 (S.28). Hii sheria naona bado inahitaji maboresho zaidi (Amendement).
Tanzania tuna aina tatu (3) za walipa kodi
1. Walipakodi wadogo ( Presumptive)
2. Walipa kodi wa kati (Normal flow)
3. Walipakodi wakubwa ( Large taxpayers)
Lakini kundi kubwa hapo la walipakodi kwa Tanzania linaangukia kwenye namba moja (1). Asilimia kubwa ni wale ambao tunafanya biashara ili tuweze kujikwamua kimaisha tupate chakula, tusomeshe watoto na mahitaji mengine.

Mitaji pia ni ya kuunga unga na asilimia kubwa ya bidhaa tunapata kwa mali kauli, huko bank tunamikopo ya kutosha. Sasa Mlipakodi kama huyu unakuta kwa mwezi kauza 10million (mfano). Unakuta hapo million 9 inakwenda kulipa deni la watu anabaki na million moja hapo hujalipa kodi ya pango, gharama za umeme, maji, chakula, taka nknk.

Mlipakodi kama huyu unakuja kumtandika na VAT juu, hapo unamtoa kutoka presumptive kwenda kuwa mlipaji kodi wa kati (Normal flow). Mlipakodi atakiwa atafute mtu (mhasibu) wa kumsaidia kutuma ritani za VAT kila mwezi na bado atahitajika kuandaa hesabu zake Financial statements tayari gharama zimeongezeka kwenye biashara.

Ushauri wangu kwa TRA msikimbilie kusajili VAT embu fanyeni kwanza evaluation ya kutosha kwa Mlipakodi. Msikimbilie kusajili, lengo ni kupata Walipakodi bora lasivyo mnazalisha wakwepaji ( Non fillers). Fanyeni tathmini ya kutosha hata zaidi ya miaka 2 mjiridhishe na Mlipakodi. Kumuingiza mteja kwenye VAT mnampa gharama za kila mwezi za kutuma ritani pamoja na gharama za kuandaa hesabu kwa wahasibu biashara ndo inaanza kuyumba, sababu ni ndogo anategemea mali kauli. TRA mnaua biashara nyingi sana huku mitaani kama hamjui leo nawaambia.

Tuje upande wapili

Tatizo ni kwamba unakuta uyo mlipakodi mwaka jana 2022 mauzo yalishuka mpaka 50million kutokana na kuyumba kwa biashara. Mwaka huu Ukienda ofisini TRA kuomba kuondolewa na VAT na pia kuondolewa kwenye mfumo wa e-filling ni kipengele sana utapigwa danadana mpaka ukome. Na mnajua fika mteja akitumia E-filling lazima atatakiwa kuandaa hesabu za mwaka husika.

Sasa kama mteja alifika 100m akasajiliwa na VAT pindi mauzo yanaposhuka na kua chini ya hapo kwanini asitolewe kwenye VAT??. Inamaana hiyo mifumo yenu inashindwa kutambua??. Utaandika barua utazungushwa mpaka unakata tamaa , hapohapo ofisa anakwambia wewe mauzo yameshuka sababu hutoi risiti. Moja ya sababu ya kipumbavu ukimwuliza unaushahidi na unachosema atabaki anajiuma.

Biashara zinabadilika unakuta mtu alipata mauzo makubwa sababu alibahatika kupata tenda ndo ikaboost mauzo. Baada ya kumaliza mkataba mauzo yakashuka yakarudi kama zamani japo kuna ambao hawatoi risiti kweli. TRA hili suala mlitizame maana asilimia kubwa return za VAT ni repayment sababu ya masuala kama haya.

Na hili suala la e-filling kama mlipakodi aliambiwa afanye self assessment online akafanya kwanini kwenye kutoka inakuwa ngumu?. Kwanini kwenye system msiweke option ya kujiondoa?. Ofisa anakwambia mpaka makao makuu kutolewa, mbona tunavoingia kwenye mfumo hatukwenda makao makuu??. Mlipakodi akishakuwa chini ya 100m kwa individual huyu sio account case tena anatakiwa kuondolewa kwenye VAT arudi kuwa presumptive case, kama sheria inavyosema.

Kuna mambo mnafanya mazuri mnastahili pongezi ila kwa hili lina discourage sana walipa kodi. Nakutana na case kama hizi nyingi sana watu wanaumia maana inauwaumiza sana wafanyabiashara wadogo.

Unaweza kuwasiliana na mimi kwa mahitaji ya:
-Makadirio ya kodi (binafsi na kampuni)
-kufungua/kusajili TIN (binafsi na kampuni)
-kufungua business name na kusajili kampuni. BRELA
-Kutuma/kuandaa Ritani za VAT/SDL/PAYE nk
-Kuandaa hesabu (Financial statements)
-Driving license 🪪
-Leseni za Biashara.
-Tax payments receipt. nknk

Tulipe Kodi kwa Maendeleo ya Taifa letu.
 
Leo nitabase na walipakodi binafsi/ Individual taxpayers (Presumptive ). Kuna jambo ambalo nafikiri ni kilio kwa wengi ila wanakosa mahali pakusemea. Ukweli hili jambo TRA mliangalie ni namna gani mtaweza kulitatua.

Mlipakodi akifikisha mauzo ya milion 100 mnamsajili na VAT na pia mnamwambia afanye self assessment. Nashindwa kutambua ni sheria ipi ambayo inamlazimisha mlipakodi kufanya online self assessment (e-filling)?. Point yenu ni kwamba mteja

Tulipe Kodi kwa Maendeleo ya Taifa letu.

Shukrani mkuu, nimejifunza kumbe ili uingie kwenye VAT ni lazima mauzo yako yafike 100m na zaidi.
 
Leo nitabase na walipakodi binafsi/ Individual taxpayers (Presumptive ). Kuna jambo ambalo nafikiri ni kilio kwa wengi ila wanakosa mahali pakusemea. Ukweli hili jambo TRA mliangalie ni namna gani mtaweza kulitatua.

Mlipakodi akifikisha mauzo ya milion 100 mnamsajili na VAT na pia mnamwambia afanye self assessment. Nashindwa

Nimeanza kusoma vizuri ingawa bandiko lako lina makosa madogomadogo mwisho nikakutana na TANGAZO! TANGAZO! haya tutakuja.
 
Marketing stratergy nzuri kwa tax consultant. Mada nzuri pia. Wafanyabiashara msiwe wavivu kuwatumia washauri wa kodi.
Kama sheria za kodi ni mbovu hata huyo mshauri anafika dead end.
 
Leo nitabase na walipakodi binafsi/ Individual taxpayers (Presumptive ). Kuna jambo ambalo nafikiri ni kilio kwa wengi ila wanakosa mahali pakusemea. Ukweli hili jambo TRA mliangalie ni namna gani mtaweza kulitatua.

Mlipakodi akifikisha mauzo ya milion 100 mnamsajili na VAT na pia mnamwambia afanye self assessment. Nashindwa
Naunga mkono hoja,wanavyoshupaa na VAT utadhani biashara yako inakuwa ipo juu tu wakati hali imebadilika sana lakini bado wanatukamua,kuwekwa kwenye haraka inakuwa haraka sana na vitisho juu lakini, unapotaka kuondolewa kutokana na biashara kwenda halijojo basi hapo inakuwa ni danadana
 
Sheria nyingi za kodi hapa kwetu ni copy and paste kutoka huko first world, ndo maana unakuta vitu vingi Tra wana struggle kuvielezea .naamini hata hii vat huko first world ilimuja kuwa introduced baada ya uchumi wa wafanyabiashara kuwa imara huko kwao , siai huku vat inaanza kubana masikini
 
Hivi wenye maduka ya uwakala naona Kama wanna kondi nyingi maana wanakata kwenye miamala na bado unalipa hizi za leseni za biashara why tusiwe na Kodi moja tu
 
Ukweli TRA bado katika utendaji wako mifumo yao mingi bado haiko kufavor pande zote mbili. Wao wanajua kukamua tuu.

Mfano kwa wafanyabiashara ambao hawajisajili kama entity au kampuni wengi kodi zao zinapigwa kulingana na mauzo, hawaangali kama mtu huyu anatumia na cost zingine kama kodi, huduma za kufikisha mzigo kwa watej wake katika iyo biashara. Wao watataka kuona efd tuu imefanya kazi.

Wanaamini kila mwaka au kila baada ya mwaka wa fedha biashara yako imekua so wao ni kuongeza kiwango cha kodi kufikia target za kisiasa.

Mimi tangu tusumbuane nilipokosea kutoa risti ya million 10 nikatoa billion 1 ile risti wakashindwa kuclear baada ya claim zote. Nikapata dawa ni kila ndugu atafanya iyo biashara kodi ikiwa mlima tunaamia kwa mwingine
 
Kodi, hadi pale kura itakapopigwa kulingana na ulipaji kodi labda wanasiasa watakuwa siriazi

Maana watajua kuwa walipakodi ndio wenye mamlaka ya kuzitumia hizo kodi
 
Wengine wanalilia kuingia VAT, wengine huwa hawataki kuisikia.

Tanzania zaidi ya uijuavyo.

Kama mtu analilia kuingia VAT kuna mambo mawili
1. Anatenda au anafukuzia tenda za serikalini
2. Professional business yoyote lzima isajiliwe na VAT kisheria.
 
Naunga mkono hoja,wanavyoshupaa na VAT utadhani biashara yako inakuwa ipo juu tu wakati hali imebadilika sana lakini bado wanatukamua,kuwekwa kwenye haraka inakuwa haraka sana na vitisho juu lakini, unapotaka kuondolewa kutokana na biashara kwenda halijojo basi hapo inakuwa ni danadana

Ndo sheria za kodi hizo, zina mapungufu mengi sana.
 
Hivi wenye maduka ya uwakala naona Kama wanna kondi nyingi maana wanakata kwenye miamala na bado unalipa hizi za leseni za biashara why tusiwe na Kodi moja tu

Kodi ni laki 1 kwa wakala wa simu ila kama utakua na zile za bank kodi inaongezwa na pia ina depend na size ya business.
 
Ukweli TRA bado katika utendaji wako mifumo yao mingi bado haiko kufavor pande zote mbili. Wao wanajua kukamua tuu.

Mfano kwa wafanyabiashara ambao hawajisajili kama entity au kampuni wengi kodi zao zinapigwa kulingana na mauzo, hawaangali kama mtu huyu anatumia na cost zingine kama kodi, huduma za kufikisha mzigo kwa watej wake katika iyo biashara. Wao watataka kuona efd tuu imefanya kazi.

Wanaamini kila mwaka au kila baada ya mwaka wa fedha biashara yako imekua so wao ni kuongeza kiwango cha kodi kufikia target za kisiasa.

Mimi tangu tusumbuane nilipokosea kutoa risti ya million 10 nikatoa billion 1 ile risti wakashindwa kuclear baada ya claim zote. Nikapata dawa ni kila ndugu atafanya iyo biashara kodi ikiwa mlima tunaamia kwa mwingine

Presumptive anachajiwa kodi kutokana na mauzo yake kama unamauzo ya million 40 bhs hapo hapo kodi itakatwa hawaangalii kama ulipata hasara. Wao watakata kodi kutokana na mauzo ghafi yako.

Kwa kampuni ndo 30% ya profit.
 
Back
Top Bottom