TRA: Kufuta Usajili wa Vyombo vya Moto

TRA: Kufuta Usajili wa Vyombo vya Moto

Kufuta Usajili wa Vyombo vya Moto​


Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) inapenda kuwajulisha watu wote wanao miliki vyombo vya moto (magari, matrekta, pikipiki na matela) ambavyo havipo tena barabarani au haviwezi tena kurudi barabarani kwa sababu ya uchakavu, kuwasilisha maombi yao TRA ya kuvifuta kwenye usajili.

Kwa mujibu wa Kanuni Namba 177 ya mwaka 2001 ya Sheria ya Usalama Barabarani ya Mwaka 1973 kinamtaka mwenye chombo cha moto ambacho hakifai kuwa barabarani kuomba kufutwa kwenye usajili wa magari

Mwongozo:

1. Mmiliki atatakiwa kwenda Ofisi ya Usalama Barabarani (Polisi) kwa ukaguzi wa chombo cha moto na kupata cheti cha ruhusa ya kufuta usajili

2. Mmiliki atatakiwa kuwasilisha barua ya maombi ya kufuta usajili ofisi ya TRA iliyokaribu ikiambatanishwa na kadi halisi ya gari na cheti kutoka ofisi ya usalama barabarani

3. Baada ya TRA kuridhika na taarifa zilizowasilishwa maombi yatakubaliwa na chombo husika kitafutwa kwenye usajili na mmiliki atapewa cheti kuthibitisha kufutwa kwa chombo husika

Lengo:
Lengo la tangazo hili ni kuwahimiza wenye vyombo vya moto ambavyo haviko barabarani kuwasilisha maombi ya kufuta usajili haraka ili Serikali iwe na kumbukumbu sahihi ya idadi ya vyombo vya moto vinavyotembea barabarani kwa ajili ya kurahisisha mipango yake ya maendeleo ya taif
Load License inarudi
 
Na je kama niliuza kama screpa hapo inakuwaje
 
Serikali ya Ccm ni SAwa na mpika chapati leo atakuja na hili kesho watatugeuza vile
 

Kufuta Usajili wa Vyombo vya Moto​


Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) inapenda kuwajulisha watu wote wanao miliki vyombo vya moto (magari, matrekta, pikipiki na matela) ambavyo havipo tena barabarani au haviwezi tena kurudi barabarani kwa sababu ya uchakavu, kuwasilisha maombi yao TRA ya kuvifuta kwenye usajili.

Kwa mujibu wa Kanuni Namba 177 ya mwaka 2001 ya Sheria ya Usalama Barabarani ya Mwaka 1973 kinamtaka mwenye chombo cha moto ambacho hakifai kuwa barabarani kuomba kufutwa kwenye usajili wa magari

Mwongozo:

1. Mmiliki atatakiwa kwenda Ofisi ya Usalama Barabarani (Polisi) kwa ukaguzi wa chombo cha moto na kupata cheti cha ruhusa ya kufuta usajili

2. Mmiliki atatakiwa kuwasilisha barua ya maombi ya kufuta usajili ofisi ya TRA iliyokaribu ikiambatanishwa na kadi halisi ya gari na cheti kutoka ofisi ya usalama barabarani

3. Baada ya TRA kuridhika na taarifa zilizowasilishwa maombi yatakubaliwa na chombo husika kitafutwa kwenye usajili na mmiliki atapewa cheti kuthibitisha kufutwa kwa chombo husika

Lengo:
Lengo la tangazo hili ni kuwahimiza wenye vyombo vya moto ambavyo haviko barabarani kuwasilisha maombi ya kufuta usajili haraka ili Serikali iwe na kumbukumbu sahihi ya idadi ya vyombo vya moto vinavyotembea barabarani kwa ajili ya kurahisisha mipango yake ya maendeleo ya taifa
Kwa hiyo tuseme tu kuwa hiyo ni sensa ya magari au siyo???.
 
Naskia Japan kuna ukomo wa kilomita za vyombo vya moto. Zikiisha hizo kilomita basi chombo cha moto hakiruhusiwi barabarani. Lengo la kufanya hivyo ni kuhifadhi mazingira.

Ukija huku kwetu (TZ), mambo ni tofauti. Unakuta gari au pikipiki ya miaka mingi na kilomita kibao ila ipo barabarani.

Sasa, je, kuna ubaya gani kwa hapa Tanzania magari namba A yakaondolewa barabarani?

Sent from my TECNO F1 using JamiiForums mobile app

Wanafanya hivyo kwa kuwa wana viwanda vingi,wasiendelee kuchafua hewa na sisi hatuna viwanda vingi so hatuchafui hewa’wastan’
 

Kufuta Usajili wa Vyombo vya Moto​




Mwongozo:

1. Mmiliki atatakiwa kwenda Ofisi ya Usalama Barabarani (Polisi) kwa ukaguzi wa chombo cha moto na kupata cheti cha ruhusa ya kufuta usajili
Gari litapelekwaje kukaguliwa wakati halitembei na halifai tena, au litapebwa na fuso kwenda kukaguliwa...
 
Ukiona hivyo ukifika tu unalipia ada ya kuondoa gari yako kwenye usajili.

Bado utawalipa polisi kuja kwenye karakana yako kukagua gari.

Ahahha hii nchi ni ngumu sana, hela inasakwa. Dunia ya leo kwa nini wasije na teknolojia kila kitu kikafanyika kwa njia ya internet.

Taasisi za serikali zinapenda kujaza sana watu ofisini kwao
 
Basi tuangalie hata km. Magari yenye kilomita nyingi yaondolewe barabarani.

Mbona Japan magari ni mazima ila yanaondolewa barabarani kwa sababu ya km nyinhi?

Unajua sisi TZ hatujali kabisa afya. Unakuta gari linatoa moshi mweusi na lipo barabarani tu!

Nimejaribu kufanya utafiti. Magari mengi namba "AAA" ni ya zamani sana, na tena yana kilomita nyingi sana, hivyo yaondolewe kwani yanazalisha kiwango kikubwa cha hewa chafu!

Wachache sana wenye magari kumi mchanganyiko yaani namba "AAA" na namba "D". Wengi wenye namba "AAA" wanalo moja wanajikongoja nalo!

Sent from my TECNO F1 using JamiiForums mobile app
Japan vs Tanzania
Two different things
 
Ukiona hivyo ukifika tu unalipia ada ya kuondoa gari yako kwenye usajili.

Bado utawalipa polisi kuja kwenye karakana yako kukagua gari.

Ahahha hii nchi ni ngumu sana, hela inasakwa. Dunia ya leo kwa nini wasije na teknolojia kila kitu kikafanyika kwa njia ya internet.

Taasisi za serikali zinapenda kujaza sana watu ofisini kwao
Wavivu wa kutumia Teknolojia,
 
Back
Top Bottom