TRA Bukoba na wengine huu nao ufisadi

TRA Bukoba na wengine huu nao ufisadi

Joined
Apr 8, 2014
Posts
60
Reaction score
18
Kama umewahi kufika katika mji wa BUKOBA Manispaa utakuwa shahidi kuwa hakuna daladala ambazo zinafanya safari za ndani ya mji na badala yake utaina no Pikipiki tu alimaarufu "sekido" na madereva wakiitwa "asekido"

Nauli zetuni 500 tsh tu kwa routes za karibu na mbali kidogo ni 1000 na kuendelea.

Kutokana na hali hiyo wauzaji wa Pikipiki wamekuwa wakipata faida nyingi kwa kuuza sana Pikipiki na kwa bei wanayotaka kwakuwa
1. Bukoba ni mbali na maeneo mengine
2. Pikipiki ni usafiri wetu mkuu
3. Wauzaji wote wana connection na TRA mkoa


Ninachoshangaa, TRA siku zote wana kagua vitabu vya wauzaji na kuchukua chao , lakini Pikipiki sasa inauzwa 2.4 millions na kitabu kinaandikwa 2.0 hadi 2.1

Hamuwaulizi mbona bei ni ndogo kuliko inayouzwa?

Sisemi mengi .... Kabla hatujawataja madalali Wa leseni za udereva, na wanaotetea hawa wenye maduka.... Simamieni uhalali Wa bei na kodi inayokwenda serikalini ....

Mtatuambia hiyo laki 3 ambayo haiandikwi mnagawanaje??? Tunaijua mienendo yenu ....

Chukueni tahadhari na waandishi Wa habari lifanyieni kazi suala hilo
 
Watajeni ili iwasaidie nyie raia vinginevyo watazidi kuwanyonga
 
Dalali wa TRA hapo Bukoba anaitwa LUGANUZA ni majanga mnk ana connect na watu wa TRA ili kuumiza hao vijana wa hizo sekido.
 
Hii sekta ya serikali ya ccm ni majanga tuh..!
 
hapo ofisi za TRA kuna ukilitimba wa ajabu sana. Kuna jamaa angu alienda kupatiwa TIN number alipewa process hadi akakimbia.

Eti unataka kufanya biashara gani, utatumia mtaji wa sh ngapi, yani kabla ya kufikia kupewa TIN number ili ukapate leseni halmashauri wanakukadiria kwanza halafu unalipa kodi hio ya mwaka mmoja ndio wanakupatia TIN.

TRA wanawaona wana Bukoba hamnazo kabisa.
 
Back
Top Bottom