Leseni yangu ya udereva iliisha hivyo nikaenda kuirenew karibu mwezi mmoja umeshapita. Pale TRA Samora kila nikienda wananiambia material hakuna lakini naona wengine wanavipata kama kawaida.
Nikamuuliza dogo mmoja akaniambia mpaka nitoe chochote nami nimegoma sababu sioni mantiki ya kutoa rushwa kabisa.
Naombeni ushauri nitumie njia gani nipate leseni yangu kwani nimechoka kutembea na risiti zao tu.
Unajua kama tunataka nchi iendelee inabidi tuwasaidie watu kufanya kazi. Kuwapa license bila mambo ya rushwa na mambo mengine ya kijingajinga.
Mtu kama wewe ndio mlipa kodi, ndio unaiwezesha serikali kutimiza malengo yake.
Kwahiyo Serikali iwe na mikakati makini kuwasaidia wananchi wake kama kupata leseni,kulipa kodi haraka bila usumbufu, kupunguza rushwa, kuwasaidia na kuwawezesha wanyonge, wasiwe wanyonge tena.
Tuwasaidie walalahoi wasilale hoi sana kila siku.
Walipa kodi waweze kulipa kodi haraka, ndugu zetu, watu wetu, Wantazania wenzentu waweze kusaidia familia zao, jamii zao, taifa lao.
Tutafakari, tuweke malengo, kanuni na sheria zitakaowasaidia wananchi wetu, wengi wetu.
Sheria, kanuni, masharti, vitu gani vinaweza kukomboa taifa zima, sio tu kunufaisha maslahi yetu binafsi, familia zetu, our narrow interests, siasa zetu.
Hamna nchi iliyoendelea inakubaliana na ujinga kama huu wa kuangalia maslahi yetu binafsi, madogo kama iongeefamilia, ukoo, kabila letu(narrow interests.)
TRA ikiwa makini, ikifanya kazi kama nchi ziliondelea, kusimamia haki ya wananchi wake, nchi itasimama haraka sana.
Tuache mambo ya kukomoana, rushwa, na ujinga ujinga, mambo ya kitoto.
We should grow up.