Mkuu, yote hayo ya nini! Hebu fikiria endapo jamaa wakiamua kuonekana wapo kazini halafu hawafanyi kazi. Hao ffu watafanya nini? Pinda atafanya nini? Mimi naona mgomo baridi una impact kubwa kuliko kuliko kitu chochote. Wao si wataangalia daftari la mahudhurio tu.
Jana PM alisema watafutwe madaktari kutoka sehemu mbalimbali wakatibu, hivi anajua impact yake? Fikiria daktari aliyemaliza degree yake miaka kumi na zaidi iliyopita halafu hakufanya kazi hospitalini (aliwekwa pale wizarani), leo hii tuaminishwe kwamba akatibu watu, hili si bomu?! Tujiulize, kwa kipindi cha miaka kumi, tumebadili dawa za malaria mara ngapi? Au, kabla ya kuanza kutibu watapata fresher couse. Lakini pia, hivi tuna wanajeshi wangapi maMD jamani? Au labda mkuu alimanisha madaktari wa sampuli gani.
Kwa mtazamo wangu, naona kuna mabaya zaidi yanafuata.......