Return Of Undertaker
JF-Expert Member
- Jun 12, 2012
- 4,572
- 26,868
Hebu tuache hii tabia ya kijinga ya kuumauma maneno na kujipendekeza. Call a spade a spade, not a big spoon. Wazee wa kujipendekeza wameanza kupayuka "ooh Nyalandu yupo TAKUKURU, Chadema mmezusha kuwa amekamatwa na watu wasiojulikana"
Iko hivi. Nyalandu alikua kwenye kikao cha ndani pale Itaja. Wamekuja watu wakiwa na silaha za moto, AK47 na Sub Machine Gun. Kufika wakasema wanamtaka Nyalandu, David Jumbe na Mwenyekiti wa Chadema kwenye kata hiyo. Walipoulizwa wao ni nani wakakataa kujitambulisha. Hata vitambulisho wamegoma kutoa. Wakawashurutisha watu hao watatu hadi kwenye gari na kuondoka nao.
Sasa mlitarajia Chadema waote kuwa hao ni maafisa wa Takukuru? Hivi kama wamekataa kujitambulisha wangejulikanaje kuwa ni Takukuru? Kwahiyo taarifa kwamba ni watu wasiojulikana ni sahihi as long as walikataa kujitambulisha.
Pili; hivi ni kuanzia lini maafisa wa Takukuru wameanza kutembea na silaha za kivita kama AK47 au SMG? Sheria ya kuzuia na kupambana na rushwa Na.11 ya mwaka 2007 inazuia afisa wa Takukuru kubeba silaha yoyote (hata rungu). Leo watu wanaenda na AK47 halafu tunaambiwa ni maafisa wa Takukuru na tunakubali kirahisi kabisa. Shame on u. JPM aliwahi kusema watanzania sio wajinga kama mnavyodhani.
Halafu Takukuru kama walikua wanamhitaji Nyalandu wangeweza kumpa tu 'notice' akaripoti ofisini kwao. Hakukua na haja ya kutuma watu wenye silaha za kivita kwenda kumfanyia ambush kama jambazi. Nguvu zote hizo kwa faida ya nani?
Tatu, ni mara ngapi ndugu zetu wamechukuliwa na watu ambao walikataa kujitambulisha na hawajaonekana hadi leo? Azory Gwanda alichukuliwa na watu waliokataa kujitambulisha na hadi leo hajaonekana hata mfupa wake. Erick Msyaliha the same. Sasa leo wanakuja watu kumchukua Nyalandu wanakataa kujitambulisha mlitaka tueleweje.
Kule Musoma it was the same scenario. Watu waliokataa kujitambulisha walitaka kumchukua Zacharia. Alipowazidi nguvu na kuwatandika risasi ndio tukaambiwa ni maafisa usalama. Kama wangefanikiwa kumchukua, sina hakika kama wangekaa wajulikane kuwa ni watu wa usalama. Pengine tungeendelea kuambiwa ni watu wasiojulikana.
Mwisho ni kwa wafuasi na wanachama wa Chadema pale Itaja. Mmezingua sana. Yani watu wanachukuliwaje kwa nguvu wakiwa kwenye kikao na nyie mnakaa kimya? Nyie ndo mnafanya tuonekane 'maboya' wa kutekwa tu wakati wowote hawa 'maharamia' wanapojisikia kufanya hivyo.
Kitendo cha hao jamaa kukataa kujitambilisha ilitakiwa muwazuie kuwachukua kina Nyalandu. Jukumu la wanachama ni pamoja na kuwalinda viongozi wao kwa gharama yoyote. Sasa nyie mmeona mitutu mkanywea? Mkaacha jamaa wakachukuliwa kama kuku? Mmezingua sana. Kama na nyie mnajiita 'makamanda' basi tuna safari ndefu sana ya kufikia ukombozi.
Credit to G malisa
Iko hivi. Nyalandu alikua kwenye kikao cha ndani pale Itaja. Wamekuja watu wakiwa na silaha za moto, AK47 na Sub Machine Gun. Kufika wakasema wanamtaka Nyalandu, David Jumbe na Mwenyekiti wa Chadema kwenye kata hiyo. Walipoulizwa wao ni nani wakakataa kujitambulisha. Hata vitambulisho wamegoma kutoa. Wakawashurutisha watu hao watatu hadi kwenye gari na kuondoka nao.
Sasa mlitarajia Chadema waote kuwa hao ni maafisa wa Takukuru? Hivi kama wamekataa kujitambulisha wangejulikanaje kuwa ni Takukuru? Kwahiyo taarifa kwamba ni watu wasiojulikana ni sahihi as long as walikataa kujitambulisha.
Pili; hivi ni kuanzia lini maafisa wa Takukuru wameanza kutembea na silaha za kivita kama AK47 au SMG? Sheria ya kuzuia na kupambana na rushwa Na.11 ya mwaka 2007 inazuia afisa wa Takukuru kubeba silaha yoyote (hata rungu). Leo watu wanaenda na AK47 halafu tunaambiwa ni maafisa wa Takukuru na tunakubali kirahisi kabisa. Shame on u. JPM aliwahi kusema watanzania sio wajinga kama mnavyodhani.
Halafu Takukuru kama walikua wanamhitaji Nyalandu wangeweza kumpa tu 'notice' akaripoti ofisini kwao. Hakukua na haja ya kutuma watu wenye silaha za kivita kwenda kumfanyia ambush kama jambazi. Nguvu zote hizo kwa faida ya nani?
Tatu, ni mara ngapi ndugu zetu wamechukuliwa na watu ambao walikataa kujitambulisha na hawajaonekana hadi leo? Azory Gwanda alichukuliwa na watu waliokataa kujitambulisha na hadi leo hajaonekana hata mfupa wake. Erick Msyaliha the same. Sasa leo wanakuja watu kumchukua Nyalandu wanakataa kujitambulisha mlitaka tueleweje.
Kule Musoma it was the same scenario. Watu waliokataa kujitambulisha walitaka kumchukua Zacharia. Alipowazidi nguvu na kuwatandika risasi ndio tukaambiwa ni maafisa usalama. Kama wangefanikiwa kumchukua, sina hakika kama wangekaa wajulikane kuwa ni watu wa usalama. Pengine tungeendelea kuambiwa ni watu wasiojulikana.
Mwisho ni kwa wafuasi na wanachama wa Chadema pale Itaja. Mmezingua sana. Yani watu wanachukuliwaje kwa nguvu wakiwa kwenye kikao na nyie mnakaa kimya? Nyie ndo mnafanya tuonekane 'maboya' wa kutekwa tu wakati wowote hawa 'maharamia' wanapojisikia kufanya hivyo.
Kitendo cha hao jamaa kukataa kujitambilisha ilitakiwa muwazuie kuwachukua kina Nyalandu. Jukumu la wanachama ni pamoja na kuwalinda viongozi wao kwa gharama yoyote. Sasa nyie mmeona mitutu mkanywea? Mkaacha jamaa wakachukuliwa kama kuku? Mmezingua sana. Kama na nyie mnajiita 'makamanda' basi tuna safari ndefu sana ya kufikia ukombozi.
Credit to G malisa