Tofauti kati ya CHADEMA na CCM na Vyama vingine

mabadilikosasa

JF-Expert Member
Dec 23, 2010
379
85
naomba niwape tofauti kati ya chama maarufu, chadema, na chama tawala, ccm- ambacho kitakufa hata kama wakibadilishana nafasi.
chadema:
1. wasema ukweli daima na hali halisi ilivyo, na wausimamia na kujengea ukweli huo hoja, inakubaliwa na wananchi
2. viongozi wao wote ni wazalendo wa kweli na thamira yao ni kuwakomboa wananchi, maslahi ya nchi kwanza, ubinafsi hakuna.
3. inakerwa na umaskini uliokidhiri tanzania
4. inapinga rushwa, na wizi wa mali ya umma kwa nguvu zote, e.g pima hoja zao hata wakiwa bungeni
5. watu wengi ndani ya chadema wana sifa na uwezo wa kuongoza, na dhamira ya kweli ya kumkomboa mtanzania
6. sera yao ya wananchi kwanza, viongozi baadae ni nzuri

CCM
1. wazuri wa kutunga owongo tofauti na hali halisi ilivyo, na wanajengea uwongo huo hoja, e.g swala ya muswada wa katiba, Dowans, richmond, EPA, na mengine mengi, uchaguzi wa meya wa arusha
2. viongozi wake wengi sii wazalendo, wengi wapo kwa maslahi binafsi, either kwa njia ya madaraka, au kukwepa kodi, au kufaidika kibiashara,e.g rostam, lowasa, sophia simba, na wengine wengi
3. wanachukulia umaskini wa watanzania kama kawaida, na hawana nia ya kweli kuupunguza, au kuutokomeza
4. Rushwa ni mchezo ulio halalishwa katika siasa zao ndani ya chama, na hawana uchungu na raslimali za tanzania
5. watu wengi ndani ya serikali, na chama hawachaguliwi kwa sifa za elimu na uadilifu e.g. makamba, sophia simba, na wengine wengi
6. Sera yao ni CCM (viongozi) kwanza, wananchi baadae.
7. Ubabe, udikteta, na kulazimisha mambo ndo sera yako, hawataki democrasia ya kweli, eg. walichakachua kura ktk majimbo mengi ya uchaguzi, pamoja na kura za urais

Hoja za uongo hazitaweza kuisaidia CCM. Zungumzeni ukweli juu ya mambo yote kufuatana na hali halisi, watanzania sii wote wajinga.wapo wanaojua duniani inakwendaje.

Watanzania sasa wanataka chama kinachosema ukweli na kuzungumza mambo kisayansi, siyo porojo. Kuwa mwanasiasa sii kuwa bingwa wa uongo na ubabe
 
Back
Top Bottom