Husninyo
JF-Expert Member
- Oct 24, 2010
- 23,723
- 9,189
PM=Panga Mapema. haya njoo tupange halaka kabla uporoto hajavamia jukwaa.
hebu usimtaje taje uporoto wangu. Ntakung'ata.
PM=Panga Mapema. haya njoo tupange halaka kabla uporoto hajavamia jukwaa.
Wapi???Ntakung'ata.
hauogopi marazi ya kuambukiza?hapo.
.
hauogopi marazi ya kuambukiza?
Ohooo!!! Kumbe uko na brazameni Kloronitaziba meno na plasta kabla sijakung'ata.
Ohooo!!! Kumbe uko na brazameni Kloro
dah! jamaa walisema umelazwa hospitali ya rufaa muhimbili? Dah JF kwa majungu bana, tena niliwaambia aisee jamaa ni mzima lakini walibishia ajabu.Ohooo!!! Kumbe uko na brazameni Kloro
Utaning'ata lini? hakyababu i cant wait.nitaziba meno na plasta kabla sijakung'ata.
Utaning'ata lini? hakyababu i cant wait.
Wee Mzee Small acha majungu banaaadah! jamaa walisema umelazwa hospitali ya rufaa muhimbili? Dah JF kwa majungu bana, tena niliwaambia aisee jamaa ni mzima lakini walibishia ajabu.
khaaa! ankal unachafua CV aisee, yaani mimi mzee small?, dah! afazali Keren Happuch hayupo online.Wee Mzee Small acha majungu banaaa
Mkuu umekubalika, katika hii hii fani
Mistari imetukuka, tukuite namba wani?
Mwenyewe nimetishika, Naogopa kusaini
Kwangu usiwe na shaka, najipa matumaini
Mapenzi ni usanii, babu aliniusia
Jifanye kuwa mtii, mapenzi kukumbatia
Lakini yakikuudhii, haraka mbele timua
Mapenzi ni ulaghai, Lugha tamu kutumia
Nikisema sili sinywi, hivi nitaishi vipi?
Ila kama hadanganywi, atakuthamini vipi?
Atakuona nyang'anywi, takataka za makapi
Lugha mapenzi haifinywi, Hata nepi yaitwa chupi.
Ukuu ninaukana, hilo si daraja langu
Ni sifa ya maulana, mjuzi wa toka tangu
Niepushie laana, wewe kimbilio langu
Mapenzi haya ya sasa, akili kichwani mwako
Mapenzi haya ya leo, yana mingi mitihani
watu wapenda vileo, nafsi zi mashakani
Tumekosa mwelekeo,bora yale yazamani
mapenzi haya ya sasa,akili kichwani mwako
Mimi sintodanganya, sababu eti ni penzi
sitaki kujichanganya, siwezi nunua benzi
mapesa sintotawanya, naogopa utelezi
mapenzi haya ya sasa, akili kichwani mwako
Klorokwini watisha
1. Klorokwini u bingwa, kwenye fani uko juu
Hakuna anayepinga, na tena huna makuu
Mistari waipanga, twapenda zako nukuu
Klorokwini watisha
2. Wachache mlo bakia, wataalamu wa fani
Twaomba usije kimbia, twazipenda zako ghani
Yalo mema simamia, uzidishe burudani
Klorokwini watisha
3. Ghani zako ni makini, tena zinapendeza
Siuoni ulakini, kweli zajitosheleza
Wang'ara humu kundini, wengi zawabembeleza
Klorokwini watisha
4. Hii si fani ya wote, wachache mna vipaji
Sisemi wajua yote, ila nakuvisha taji
Tuongoze sasa sote, mwenzetu una kipaji
Klorokwini watisha
5. wanikumbusha kandoro, gwiji yule wa zamani
Hutomtoa kasoro, alikuwa namba wani
Ongeza kasi kloro, usiwe na mpinzani
Kloro watisha
Mengi uliyoyasema , nami ninayathamini
Shukrani ewe mwema, ulonipa tumaini
Ni nyingi zako hekima, shairi limesheheni
Namuomba karima , akuweke furahani
Ubingwa ulionipa, nauvua hapa hapa
Taji lako ninakupa, kwako nimetoka kapa
Vina nimevipa chapa, "yakuonea" uko supa
Shairi hili ni kopa , burudani umetupa
Cheo chako kiko juu, siwezi kukufikia
Uwanja wako ni huu, wengine tunadandia
Twaiga zako nukuu, kwengine twazitumia
Bahari yako buluu, fani waiogelea.
hehehe senks Mzee Moskwito aisee. Halaf mbona unaonekana kimachale au zali limeclick?...aiseee!...braza you are multi talented bana!
Lyrics zako zimetulia kuliko za hawa Bongo fleva