Vina bado vijaisha, Hakika nakuambia,
Vina ni yao maisha, Hawa naokutajia.
Klorokwini anatisha, Kunaye na lizzy pia,
Vina havijatuisha, majukumu yamebana.
Tunaye Magalumangu, Vina mejaa kichwani,
Kipaji kampa Mungu, Kamleta kwenye fani,
Ukija na hapa kwangu, Vimejaa ubongoni,
Vina havijatuisha, Majukumu yamebana
Mwanajamii wani, Acid nakutajia,
Ni magwiji kwenye fani, muda umewabania,
Mwanakijiji kundini, Teamo anafwatia,
Vina havijatuisha, Majukumu yamebana.
Hehehheh
Hata usipokubali wote twajua umeishiwa..
Msamaha siwezi omba maana sijakosea..
Hata Magulu wangu mjomba anaweza kunitetea..
Babu kubali jamani fani na utuachie!
Uzee umeshakusonga macho yameisha kuona..
Wino wako umemaliza ila bado wangangana..
Ngazi hutaki achia wajukuu tupambane..
Babu kubali jamani ngazi na utuachie!
Sasa fani imenoga, manguli wajibizana
Ikulu Lizzy kagonga, Aspirin katafuna
Nyote nyinyi ni malenga, Hamuishiwi na vina
Sasa mbele tunasonga, lugha ni yetu hazina
Babu watu wakubipu, tuliza bana mzuka
Hata utamu wa supu, ni chumvi ukiiweka
Suruali bila zipu , ina tabu kufunguka
Sasa ni yako tripu, kujibu kakubalika
Wengi wanakutambua, hii fani iko kwako
Ila wanakudonoa, umwage makeke yako
Sasa ukumbi tumia, simpe Lizzy kicheko
Namimi nashuhudia, nani apewe upako?
hehehe Tozi wa mbagala na wewe umehuzuria. Acha tukupe kibao kinachomwaga CV yako.