To You Hon Zitto Kabwe, MP

To You Hon Zitto Kabwe, MP

Hodi mlangoni wana JF naomba kuingia jamvini,
nafikiri mmeshanikaribisha naanza kwanza na Salaam kisha nasema Hon. Zitto ni mwana mapinduzi halisi asiyejua kuutumia uanamapinduzi wake is like un-guided missile. Mkiniomba kufafanua nitafafanua.

Mbona kwenye avatar yako kuna mtu kashika bunduki??

oka, karibu JF

Fafanua basi maneno yako! ila please fafanua bila ushabiki, ushabiki huwafanya watu kuwa vipofu!
karibu
 
Huyo ndiye Zitto mbaye Umar Ulyas anamfahamu vyema
 
Mbona kwenye avatar yako kuna mtu kashika bunduki??

oka, karibu JF

Waberoya
usihofu sana kwenye avatar yangu hiyo bunduki ni ishara ya amani tu hata UN wakienda kulinda amani Somalia lazima wawe nayo ingawa wengine huwa wanasema they are not going to keep peace but to spread violence.
 
naamini dhambi kuu ya zitto ni kukataa kufanya siasa kwa style mnayotaka ninyi ambayo mnadhani ndio suluhu la matatizo yenu ambayo ukweli ukiyaangalia sana hayana upeo mkubwa isipokuwa chuki zenu dhidi ya ccm tu.

Zitto anaangalia siasa zaidi ya kuiondoa ccm madarakani tu. Kwake yeye kitu cha kwanza na muhimu ni kujenga demokrasia makini ya vyama vingi ambayo itawezekana tu pale watanzania watakapoongozwa kuondoa ukiritimba wa ccm (single party dominance). Cha pili ni kujenga misingi ya watanzania wote kutambua, kuamini na kuthamini utamaduni wa kidemokrasia ambao unachukulia tofauti za kifikira na kimisimamo kama mbolea na sio sumu ya maendeleo. Cha tatu kujenga tanzania yenye nguvu kiuchumi na kijamii ambayo itawezesha kufanikisha umoja wa kiafrika ambao kwake anaamini kuwa ndio mkombozi mkuu wa madhila na changamoto tunazokutana nazo sasa kama taifa la dunia ya tatu.

Omarilyas

uwongo mtupu. Thubutu!!!!!!
Hizo ni ndoto za mchana kwa nchi kama tanzania labda huko ujerumani. Hapa kwetu bongo watu hawana hata elimu ya uraia ndio uwajaribishe siasa poa????
 
Back
Top Bottom