kwanza nimpongeze super woman Dr.Gourgeousmimi kwa thread nzuri pamoja na yote ameleta kitu cha tofauti chenye hadhi ya kujadiliwa na watu wenye akili na busara na kwa utulivu mkubwa.
pili, asante kwa kuleta upande mwingine wa shilingi kuhusu wanaume. daima sitabadili maneno ya kitabu kitakatifu.
kwenye comment yangu niliweka wazi kabisa kuwa thread inahusu wajibu wa mwanamke kwa mwanaume kama Dr alivyoiweka. Sija over look chochote na sina sababu ya kufanya hivyo. Umeamua kuongeza pale nilipoacha kuweka ni sahihi kabisa...ndio maana tuko JF, ni sehemu ambayo watu wanatoa maoni,na thread inakuwa na comment hata mia tatu,siwezi kumaliza kila kitu mimi na sifahamu kila kitu mimi.
Tatu,Suala la kufunguliwa na Bwana sio langu kulijadili,kila kitu kina nafasi yake na wakati wake. Ikimpendeza Mungu kuniongezea na hilo la kufunguliwa katika baraka nyingi alizonipa nitazidi kumshukuru.
Kama mwanamke nimefundishwa kujua wajibu wangu na kuusimamia ipasavyo,kwa uanamke wangu napaswa kumuomba au kumshukuru Mungu kwa mwanaume ambaye anaufahamu wajibu wake, na pale naposhindwa au yeye kushindwa basi tuchukuliane,tuvumiliane na tusaidiane kufanya maisha mazuri.
Mithali 14:1"Kila mwanamke aliye na Hekima hujenga nyumba yake; Bali aliye mpumbavu hibomoa kwa mikono yake mwenyewe"
Mwisho: Naomba Gourgeous uwe unatuletea vitu vya aina hii....unajua ukijazwa ujinga ukajipa muda kuusoma unawezaa kubadili muelekeo. JF kama social forum yabidi iwaweke watu kwenye mstari kama hivi. JF ya aina hii najivunia sana kuwa sehemu yake.