Michelle
JF-Expert Member
- Nov 16, 2010
- 7,631
- 3,543
Thread nzuri sana sana Gourgeous.
Kwakuwa leo umeongelea wajibu wetu kwa wanaume zetu basi na mimi nisistize tu kuwa Biblia takatifu imetoa muongozo wa namna ambavyo mwanamke/mke mwema anapaswa kuwa. Mithali 31:10-31.
Hilo ndilo neno wanawake wa kikristo hutumia kuwafundisha watoto wao kabla ya kuwaruhusu sasa mwanangu nenda ukaolewe..... na katika hilo neno kwenye ishu ya kujiamini,nakubaliana na wewe kuwa wanawake kwa namna moja au nyingine tumekuwa sababu ya wanaume kutokujiamini.
Kwanza: Kuwabagua,kuwa nataka mwanaume mwenye hiki na kile,unakuta mwanaume ana miaka 27 lakini anatakiwa kuwa na mali ambazo mwanaume wa miaka 45-50 kiuhalisia ndio anaweza kuwa nazo. Wanachanganyikiwa kwa hili,manake kiukweli wote wanataka vilivyo vizuri machoni pao kuona kwamba anakosa kwa kitu ambacho baada ya muda akiwajibika atakuwa nacho inaumiza na kukatisha tamaa na mwishowe anakosa kujiamini.
Pili: maneno ya karaha pale ambapo mwanaume anashindwa kufikia malengo aliyotarajiwa,hili husababisha kutokujiamini sana kwa wanaume. waliofikia kusema kuwa nyuma ya mwanaume mwenye mafanikio kuna mwanamke walielewa wajibu wetu kwenye kujenga au kubomoa. Kuna siku nilimtizama mke wa Rais mteule wa Nigeria, mama Buhari,pamoja na tofauti kubwa aliyonayo ya kiumri na mumewe lakini unaona heshima,imani na kunia pamoja kati yake na mumewe. ndivyo wanawake tunavyopaswa kuwa.
Mwisho nanukuu maneno yaliyotafsiriwa ya Mithali 31: 10-......!
Kitabu cha mithali 31 kuanzia msitari wa 10 hadi 31 kimeelezea sifa mbalimbali za mke mwema, tuangalie kwa uchache sifa hizo kwa kuzichambua katika maeneo tofauti.
1. Imani
Mithali 31:26, 29, 30
Mke mwema anayashika na kuyafanyia kazi maneno ya Mungu na ni mtu ambaye anamtumikia Mungu kwa moyo wake wote na akili yake yote. Anatafuta makusudi ya Mungu katika maisha yake na kuyafuata. Zaburi 119;15
2. Ndoa
Mithali 31:11-12, 23, 28
Mke mwema humuheshimu mume wake na anahakikisha anamtendea mambo mema siku zote za maisha yake. Ni wa kuaminika na msaidizi kwa mume wake. Efeso 5:22-24, 1Petro 3
3. Malezi
Mithali 31: 26, 28
Mke mwema anawafundisha watoto wake njia za Mungu na pia anawatunza kwa upendo. Huwafundisha kwa hekima na kuwaelekeza njia iwapasayo kuiendea. Mithali 22:6
4. Huduma
Mithali 31:12-15, 17, 20
Mke mwema anamhudumia mume wake na familia yake yote kwa ukarimu na upendo. Anahakikisha wanapata chakula kilicho bora na chenye afya. Ni mtu mwenye huruma na ukarimu.
5. Mali
Mithali 31:14, 16, 18
Mke mwema anatafuta kwanza ushauri wa mumewe kabla ya kutumia fedha na pia anafanya manunuzi kwa hekima. Ni muangalifu kununua bidhaa zenye ubora kulingana na mahitaji ya familia yake.Efeso 5:23
6. Nyumba
Mithali 31:15, 20-22, 27
Mke mwema ni mtu anayeifanya nyumba iwe mahali pa kuishi. Anatengeneza mazingira ya kuvutia kwa familia yake na wageni wote na anawahudumia watu wake wote kwa ukarimu. 1pet 4:9, Ebrania 13:2
7. Muda
Mithali 31:13, 19, 27
Hutumia muda wake vizuri na kuhakikisha anakamilisha kazi zake za kila siku. Kamwe hapotezi muda katika kufanya mambo ambayo hayampendezi Mungu na yasiyo na faida.
8. Uzuri / Urembo
Mithali 31:10, 21-22, 24
Ni mrembo na mwenye thamani, ana uzuri wa ndani unatoka kwa Yesu Kristo. Anatumia ubunifu wake na utanashati wake kuleta uzuri katika maisha yake na ya watu wake.
Mungu atusaidie ili maisha yetu yaonyeshe kweli tunamjua na kumwamini yeye.
Kwakuwa leo umeongelea wajibu wetu kwa wanaume zetu basi na mimi nisistize tu kuwa Biblia takatifu imetoa muongozo wa namna ambavyo mwanamke/mke mwema anapaswa kuwa. Mithali 31:10-31.
Hilo ndilo neno wanawake wa kikristo hutumia kuwafundisha watoto wao kabla ya kuwaruhusu sasa mwanangu nenda ukaolewe..... na katika hilo neno kwenye ishu ya kujiamini,nakubaliana na wewe kuwa wanawake kwa namna moja au nyingine tumekuwa sababu ya wanaume kutokujiamini.
Kwanza: Kuwabagua,kuwa nataka mwanaume mwenye hiki na kile,unakuta mwanaume ana miaka 27 lakini anatakiwa kuwa na mali ambazo mwanaume wa miaka 45-50 kiuhalisia ndio anaweza kuwa nazo. Wanachanganyikiwa kwa hili,manake kiukweli wote wanataka vilivyo vizuri machoni pao kuona kwamba anakosa kwa kitu ambacho baada ya muda akiwajibika atakuwa nacho inaumiza na kukatisha tamaa na mwishowe anakosa kujiamini.
Pili: maneno ya karaha pale ambapo mwanaume anashindwa kufikia malengo aliyotarajiwa,hili husababisha kutokujiamini sana kwa wanaume. waliofikia kusema kuwa nyuma ya mwanaume mwenye mafanikio kuna mwanamke walielewa wajibu wetu kwenye kujenga au kubomoa. Kuna siku nilimtizama mke wa Rais mteule wa Nigeria, mama Buhari,pamoja na tofauti kubwa aliyonayo ya kiumri na mumewe lakini unaona heshima,imani na kunia pamoja kati yake na mumewe. ndivyo wanawake tunavyopaswa kuwa.
Mwisho nanukuu maneno yaliyotafsiriwa ya Mithali 31: 10-......!
Kitabu cha mithali 31 kuanzia msitari wa 10 hadi 31 kimeelezea sifa mbalimbali za mke mwema, tuangalie kwa uchache sifa hizo kwa kuzichambua katika maeneo tofauti.
1. Imani
Mithali 31:26, 29, 30
Mke mwema anayashika na kuyafanyia kazi maneno ya Mungu na ni mtu ambaye anamtumikia Mungu kwa moyo wake wote na akili yake yote. Anatafuta makusudi ya Mungu katika maisha yake na kuyafuata. Zaburi 119;15
2. Ndoa
Mithali 31:11-12, 23, 28
Mke mwema humuheshimu mume wake na anahakikisha anamtendea mambo mema siku zote za maisha yake. Ni wa kuaminika na msaidizi kwa mume wake. Efeso 5:22-24, 1Petro 3
3. Malezi
Mithali 31: 26, 28
Mke mwema anawafundisha watoto wake njia za Mungu na pia anawatunza kwa upendo. Huwafundisha kwa hekima na kuwaelekeza njia iwapasayo kuiendea. Mithali 22:6
4. Huduma
Mithali 31:12-15, 17, 20
Mke mwema anamhudumia mume wake na familia yake yote kwa ukarimu na upendo. Anahakikisha wanapata chakula kilicho bora na chenye afya. Ni mtu mwenye huruma na ukarimu.
5. Mali
Mithali 31:14, 16, 18
Mke mwema anatafuta kwanza ushauri wa mumewe kabla ya kutumia fedha na pia anafanya manunuzi kwa hekima. Ni muangalifu kununua bidhaa zenye ubora kulingana na mahitaji ya familia yake.Efeso 5:23
6. Nyumba
Mithali 31:15, 20-22, 27
Mke mwema ni mtu anayeifanya nyumba iwe mahali pa kuishi. Anatengeneza mazingira ya kuvutia kwa familia yake na wageni wote na anawahudumia watu wake wote kwa ukarimu. 1pet 4:9, Ebrania 13:2
7. Muda
Mithali 31:13, 19, 27
Hutumia muda wake vizuri na kuhakikisha anakamilisha kazi zake za kila siku. Kamwe hapotezi muda katika kufanya mambo ambayo hayampendezi Mungu na yasiyo na faida.
8. Uzuri / Urembo
Mithali 31:10, 21-22, 24
Ni mrembo na mwenye thamani, ana uzuri wa ndani unatoka kwa Yesu Kristo. Anatumia ubunifu wake na utanashati wake kuleta uzuri katika maisha yake na ya watu wake.
Mungu atusaidie ili maisha yetu yaonyeshe kweli tunamjua na kumwamini yeye.