Kasomi
JF-Expert Member
- Sep 3, 2014
- 11,036
- 20,337
TMA yatoa taarifa ya kimbunga Batsirai
Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) imetoa taarifa ya uwepo wa Kimbunga Batsirai katika maeneo ya kusini Magharibi mwa bahari ya Hindi.
TMA imesema Kimbunga hicho tangu kilipojitokeza katika bahari ya Hindi Januari 27, 2022 na kwa sasa kimesogea katika maeneo ya kisiwa cha Madagascar.
Kwa taarifa iliyotolewa leo na Mamlaka hiyo imesema uchambuzi wa mifumo ya hali ya hewa unaonyesha kutokuwepo kwa uwezekano wa Kimbunga hicho cha Batsirai kufika katika Pwani ya Tanzania.
Imeeleza kuwa uwepo wa kimbunga hicho baharini unatarajiwa kuathiri mifumo ya hali ya hewa kwa baadhi ya maeneo hapa nchini ikiwa ni pamoja na kusababisha ongezeko la mvua, vipindi vya upepo mkali unaofika na kuzidi kilometa 40 kwa saa na mawimbi makubwa baharini yanayozidi mita 2 hasa kwa maeneo ya ukanda wa pwani.
Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) imetoa taarifa ya uwepo wa Kimbunga Batsirai katika maeneo ya kusini Magharibi mwa bahari ya Hindi.
TMA imesema Kimbunga hicho tangu kilipojitokeza katika bahari ya Hindi Januari 27, 2022 na kwa sasa kimesogea katika maeneo ya kisiwa cha Madagascar.
Kwa taarifa iliyotolewa leo na Mamlaka hiyo imesema uchambuzi wa mifumo ya hali ya hewa unaonyesha kutokuwepo kwa uwezekano wa Kimbunga hicho cha Batsirai kufika katika Pwani ya Tanzania.
Imeeleza kuwa uwepo wa kimbunga hicho baharini unatarajiwa kuathiri mifumo ya hali ya hewa kwa baadhi ya maeneo hapa nchini ikiwa ni pamoja na kusababisha ongezeko la mvua, vipindi vya upepo mkali unaofika na kuzidi kilometa 40 kwa saa na mawimbi makubwa baharini yanayozidi mita 2 hasa kwa maeneo ya ukanda wa pwani.