Tozo vipi?Chadema wahini kukimbia kile kijengo chenu cha makao makuu msije kufa kwa joto
Tozo vipi?Chadema wahini kukimbia kile kijengo chenu cha makao makuu msije kufa kwa joto
We uko pande zipi? Mvua zinaanzaga kunyesha mwezi wa ngapi?Kwhiyo alizeti tunalima mwezi wangapi?
Nimekuwa nikifuatilia hizi taarifa za utabiri kwa miaka kadhaa ukweli zimenisaidia sana kujipanga na zina usahihi mkubwa, mwaka jana zimeniepusha na hasara kubwa shambani iwapo ningepanda mapema.Ukiona MTU ana beza taarifa za kitaalamu kama hizo jibu ni simple tuuu " shule hana"
Hizi habari huwa hazituhusu sisi wa Nyanda za Juu Kusini ,sijawahi shuhudia ukame landa mvua kuzidi ila mikoa ya Kaskazini na Kanda ya Ziwa daa nimeshuhudia mara kadhaa ila msijali kufa kufaana tutawalisha ila kwa bei juu.MAMLAKA ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) imesema kuna uwezekano mkubwa wa kutokea kwa ukame kutokana upungufu mvua unaotarajiwa kutokea katika kipindi cha mvua za vuli zinazotarajiwa kuanza kunyesha hivi karibuni.
Imebainishwa kuwa katika kipindi cha mvua za Oktoba hadi Desemba mikoa mingi itakuwa na upungufu mkubwa wa mvua ambazo zitakuwa chini ya wastani hadi wastani na pia kunatarajiwa kuwepo kwa vipindi vya joto kali lisilo la kawaida.
TMA imetoa tahadhari hiyo leo Septemba 2, 2021 wakati wa utabiri wa mvua za Vuli, ambazo ni mahsusi kwa maeneo ya nyanda za juu kaskazini zinazotarajiwa kuanza kwa kusuasua katika wiki ya tatu na ya nne ya mwezi Oktoba 2021 ikiwa na mtawanyiko na muendelezo usioridhisha katika maeneo mengi.
Akizungumza na waandishi wa habari, Mkurugenzi wa Huduma za Utabiri wa TMA, Dk. Hamza Kabelwa amesema mifumo ya hali ya hewa inaonyesha mvua za Vuli zinatarajiwa kuwa za chini ya wastani hadi wastani na zinatarajiwa kuambatana na vipindi virefu vya ukavu katika maeneo mengi yanayopata mvua za Vuli.
Amesema hali hii itapekeleka kutokea kwa athari mbali mbali zitakazotokana na hali ya ukavu kwa maeneo yatakayokosa mvua ikiwemo upungufu wa unyevunyevu katika udongo unatarajiwa kujitokeza katika maeneo mengi na kutokeza kwa magonjwa ya mlipuko, kutokana na upungufu wa maji safi na salama.
Athari zingine ni uwezekano wa kujitokeza upungufu wa malisho na maji hivyo kusababisha kujitokeza kwa migogoro kati ya wafugaji na watumiaji wengine wa ardhi.
Uwezekano wa kutokea matukio ya moto katika mapori na misitu, hivyo mamlaka husika zinashauriwa kupanga mikakati mahsusi ya kukabiliana na hali hiyo.
Amesema, msimu wa mvua za Vuli ni mahsusi kwa maeneo ya nyanda za juu kaskazini mashariki, mikoa ya Arusha, Manyara na Kilimanjaro na Pwani ya kaskazini, kaskazini mwa mkoa wa Morogoro, mikoa ya Pwani ikijumuisha visiwa vya Mafia, Dar es Salaam na Tanga, pamoja na visiwa vya Unguja na Pemba.
Katika ukanda wa Ziwa Victoria, Mikoa ya Kagera, Geita, Mwanza, Shinyanga, Simiyu na Mara pamoja na kaskazini mwa mkoa wa Kigoma wilaya za Kibondo na Kakonko.
"Kutokana na mifumo ya hali ya hewa ilivyo kwa sasa na inavyotarajiwa katika kipindi chote cha msimu kwa ujumla mvua za chini ya wastani hadi wastani zinatarajiwa katika maeneo mengi ya nchi yanayopata misimu miwili ya mvua kwa mwaka" amesema Kabelwa.
Amesema, baadhi ya maeneo ya ukanda wa Ziwa Victoria yanatarajiwa kupata mvua za wastani hadi chini ya wastani.
Aidha Mamlaka TMA, imetoa ushauri katika sekta mbalimbali ikiwemo Kilimo,usalama wa Chakula ,Mifugo na Uvuvi,Utalii na Wanyamapori,Usafiri na Usafirishaji,Nishati ,Maji na Madini,Mamlaka za Mji,Sekta ya Afya ,Sekta binafsi pamoja na Menejimenti za Maafa kuhakikisha zinachukua tahadhari za mapema ili kuweza kuepukana na majanga yoyote yanayoweza kujitokeza katika kipindi huu hicho cha mvua chache.
Pia wameshauriwa kuendelea kufuatilia utabiri unaotolewa na wataalamu mbalimbali kipindi chote cha Mvua za Vuli.
Michuzi Blog
Upo geita pande zipi? Unajiusisha na kulima mazao gani?Geita tunalimaga mwezi wa 9 au wa 10.
Sa sijui hapa vp
Itakuwa vizuri yakianzia hukohuko ofisini kwao!Hapo ni kujiandaa na mafuriko tu, hawa jamaa utabiri huaga vice versa.
Katoro mazao ni ya chakula...mahindi..marage karanga alzetUpo geita pande zipi? Unajiusisha na kulima mazao gani?
In the contrary, utakuwa mwaka mzuri kwa wakulima! Mazao yatapatikana ya kutosha na bei zitakuwa nzuri. Ukiweza, lima heka za kutosha...Mamlaka ya hali ya hewa imetoa utabiri wake kama unavyoonekana hapo ila huko mbeleni naona dhahama kubwa kwa sisi wakulima inakuja! View attachment 1922054
Panahitajika ufafanuzi binafsi sijapaelewaPwani ya kaskazini, kaskazini mwa mkoa wa Morogoro, mikoa ya Pwani ikijumuisha visiwa vya Mafia, Dar es Salaam na Tanga, pamoja na visiwa vya Unguja na Pemba.