Abdul Said Naumanga
JF-Expert Member
- Jan 28, 2024
- 745
- 1,470
Wanajamvi kwema?
Nadhani wote tunakumbuka tarehe 15/09/2025, taifa lilishuhudia kadhia ya aibu katika Mahakama Kuu DSM. Wanachama wa CHADEMA walipigwa na kudhalilishwa na jeshi la polisi ila mbali na hayo pia Wakili Deogratius Mahinyila (ambaye pia ni mwenyekiti wa CHADEMA Vijana), akiwa kazini kama Afisa wa Mahakama, alivamiwa na askari polisi, akakabwa, akapigwa vibao, ngumi, mateke na virungu mbele ya umma na kamera za vyombo vya habari. Cha kusikitisha zaidi, baada ya kipigo hicho, Mahinyila aliyetupwa rumande akituhumiwa kwa kosa la kufanya fujo Mahakamani.
View: https://youtu.be/3IONoqSHnMk?si=oNZ9NjwtP5Tb25tG
Tukio hili limeibua hasira na taharuki kubwa miongoni mwa wanasheria. Tanganyika Law Society (TLS) imetafsiri tukio hili si kama shambulio dhidi ya wakili mmoja, bali kama tishio kwa heshima ya taaluma nzima ya uwakili, hadhi ya Mahakama, na msingi wa Utawala wa Sheria nchini.
Kupitia vikao vyake vya dharura, TLS imetangaza hatua kadhaa za haraka ikiwemo
Nadhani wote tunakumbuka tarehe 15/09/2025, taifa lilishuhudia kadhia ya aibu katika Mahakama Kuu DSM. Wanachama wa CHADEMA walipigwa na kudhalilishwa na jeshi la polisi ila mbali na hayo pia Wakili Deogratius Mahinyila (ambaye pia ni mwenyekiti wa CHADEMA Vijana), akiwa kazini kama Afisa wa Mahakama, alivamiwa na askari polisi, akakabwa, akapigwa vibao, ngumi, mateke na virungu mbele ya umma na kamera za vyombo vya habari. Cha kusikitisha zaidi, baada ya kipigo hicho, Mahinyila aliyetupwa rumande akituhumiwa kwa kosa la kufanya fujo Mahakamani.
View: https://youtu.be/3IONoqSHnMk?si=oNZ9NjwtP5Tb25tG
Tukio hili limeibua hasira na taharuki kubwa miongoni mwa wanasheria. Tanganyika Law Society (TLS) imetafsiri tukio hili si kama shambulio dhidi ya wakili mmoja, bali kama tishio kwa heshima ya taaluma nzima ya uwakili, hadhi ya Mahakama, na msingi wa Utawala wa Sheria nchini.
Kupitia vikao vyake vya dharura, TLS imetangaza hatua kadhaa za haraka ikiwemo
- kusitisha ushiriki wa mawakili katika kesi za msaada wa kisheria (hasa za jinai) pamoja na Samia Legal Aid,
- kuandika barua rasmi kwa Jaji Mkuu na Waziri wa Katiba na Sheria kutaka tamko la wazi,
- kufungua mashauri dhidi ya askari waliohusika,
- kuandaa maandamano ya kitaifa ya amani kwa mawakili wote.
- Pia TLS imetangaza kuwa itakutana na viongozi wa juu wa Mahakama, Polisi na Serikali ili kudai suluhisho la kudumu.
Lakini hoja kubwa hapa haipo kwa Mahinyila peke yake. Tukio hili linaashiria hatari kwa kila raia. Ikiwa wakili ambae ni Afisa wa Mahakama na anayelindwa kisheria anashambuliwa ndani ya viunga vya Mahakama, mwananchi wa kawaida atawezaje kusimama mbele ya mfumo wa sheria bila hofu ya kudhalilishwa?
Hili ni zaidi ya tukio la udhalilishaji wa mtu binafsi; ni jaribio la kubomoa nguzo za haki na amani. Kukaa kimya ni kuruhusu mabavu yaingie Mahakamani na kuyavua nguvu mamlaka ya sheria. TLS imesimama imara, na ni wajibu wa kila mdau wa haki nchini kushirikiana kuhakikisha kuwa utu na heshima ya kila mwananchi inalindwa.
Hili ni zaidi ya tukio la udhalilishaji wa mtu binafsi; ni jaribio la kubomoa nguzo za haki na amani. Kukaa kimya ni kuruhusu mabavu yaingie Mahakamani na kuyavua nguvu mamlaka ya sheria. TLS imesimama imara, na ni wajibu wa kila mdau wa haki nchini kushirikiana kuhakikisha kuwa utu na heshima ya kila mwananchi inalindwa.