Tizama maandalizi ya UKUTA

Tizama maandalizi ya UKUTA

habari ya kuhamia dodoma haipo tena sasa hivi wizara zote ajenda ni UKUTA alafu mnajisifu hapa kazi tu,vichwa vya wanaccm vianakazi moja tu kufugia nywele
 
1471870384379.jpg
 
hakuna nchi inayoweza kuendesha kwa nguvu ikawashinda wananchi. polisi ni wachache kuliko wananchi. nawashauri waatumie taaluma kwenye kuzuia fujo, la sivyo wanaweza kuongeza fujo. vilevile, nafikiri tuzuie matamshi ya kuhamasisha fujo au yale yatakayoibua fujo. ninyi viongozi wa nchi ongozeni nchi kwa busara mkijizuia na maneno ya kuudhi na kusababisha chuko mioyoni mwa raia, maneno ya kebehi yanayoonyesha kama nchi hii inaongozwa kwa nguvu na si democrasia.

ninyi raia pia, pimeni wenyewe kipi chenye faida kukifanya kwa sasa. jiulize ukifanya maandamano tarehe moja, ni kwa maslahi gani, kuna faida gani utapata, au kama utavuruga maendeleo ya nchi kwanini usinyaamaze? binafsi ata kama magufuli atakuwa aliongea lugha fulani ya kuudhi, tunatakiwa kumchukulia alivyo, tumsome na tuchukuliane naye, kiiujumla hana nia mbaya kwa chochote anachofanya. tuseme ukweli tu hata uccm ccm ule wa zamani siku hizi umepungua, siku hizi rais anawaza maendeleo, unamwona ana nia ya ndani kabisa, hivyo hata kama atakuwa ameteleza ulimi, jueni kwamba maadamu alikuwa na nia njema moyoni basi tunachukuliana naye kama alivyo. la sivyo tunarudisha maendeleo nyuma na haina faida kwetu. rudini majumbani kweli mkafanye kazi. hao wanasiasa mnaowaamini ni wasaliti na wanawazunguka kila siku lakini hamuelewi tu.
 


Wewe uliwahi kuona michezo ya halaiki? Unatishia mtu mzima na nyau? Hawa wanafanya entertainment!. Ukuta wala haiko huko!. Acha wafanye show!.

Ukiona hivyo ujui ni dalili za kuishiwa pumzi. Utashangaa wanapigana wao kwa wao wala ukuta hawatauweza kwa kuwa wanapishana nayo. Inakotoka wao ndiko wanatazama. Hizi ni sarakasi tu, wala hazina uhusiano wowote na operesheni UKUTA.
 
Hii ni vita ya kisaikolojia (psychological warfare). Ukitishika umeshindwa. Kwa nini maandalizi yake makubwa hiyo dhidi ya watu wasio na silaha?
 
Back
Top Bottom