Kuna mambo ambayo ni magumu sana kwenye historia ya dunia.Mojawapo ya mambo hayo ni ajali ya iliyokua meli kubwa sana duniani iliyokua inaitwa Titanic.Meli hii ilipata ajali April 15,1912.Kuna jambo hapa nahisi haliko sawa,hebu na wewe jiulize,inakuaje tukio hili lifanane na hadithi?Kuna binadamu aliitwa Morgan Robertson,katika hadithi yake ya Futility aliyotunga mwaka 1898,inazungumzia meli ya kifahari iliyokua na jina Titan,iliyokua inafanya safari yake ya kwanza kutoka mji wenye jina la Newfoundland,England kuelekea New York,Marekani kugonga barafu kwenye bahari ya Atlantic na kuzama!Meli hiyo ya Titan haikua na majaketi ya kutosha ya kuogelea,pia ilikua na urefu wa futi 800,mwendo kasi wa Titan ulikua 25 kph.Ajali ya Titan ilitokea maili 400 kutokea ilipoanzi safari,ilipoteza maisha ya watu 2500!Hebu tuangalie Titanic,kwanza majina ni yaleyale,Titanic nayo ilipata ajali siku ya kwanza ya safari yake,nayo iligonga barafu kwenye bahari ile ile,na ilipata ajali hiyo umbali ule ule wa maili 400,ikitokea mji ule ule,ajali hii nayo ilitokea usiku wa kwanza na hakukua na majaketi ya kutosha kujiokoa,Titanic iliua watu 2200,ilikua na urefu wa futi 882.9,mwendo kasi wake ulikua 22.5!Tangu hadithi ya Futility itoke mpaka ajali ya meli ya Titanic ni miaka 14,kwanini matukio haya yafanane?Yalipangwa?