TISS (Usalama Wa Taifa): The best National Intelligence Ever!

TISS (Usalama Wa Taifa): The best National Intelligence Ever!

Chifunanga

JF-Expert Member
Joined
Oct 17, 2010
Posts
290
Reaction score
102
Moja ya kazi za hizi National Intelligences ni kuweka siri. Lakini mambo ya CIA, MOSAD, KGB na wengineo yapo kila sehemu.

Ila hawa ndugu zetu wa TISS wamejitahidi katika hii section ya kuweka siri....yaani hawana WEBSITE, halawa TWITTER account, hawana FACEBOOK account, na wala hawa OFFICIAL EMAIL.

Hawana PR (public relation person), ingawa Nzoka sijui nani alijaribu kufanya kazi hiyo kile kipindi Dr Wa ukweli alivyokuwa anatafuta Wachakachuaji.

Yaani ukitaka kusikia chochote kuhusu hawa Jamaa, ni lazima uje JF, ambapo pia story nyingi ni story tu na hazina ukweli.

Hata kwenye hii BUDGET sijasikia kipengele kilichotengwa kwa TISS......hivi POSHO zao nao wanakatwa?.....hivi kuna KIKAO cha BUNGE cha kuwadiscuss hawa jamaa.....mwenyekiti wake nani?

Hongereni TISS kwa kuwa Secret Service ya Ukweli.....sio wenzenu CIA information zao zipo nje nje tu kila sehemu.

Wadau mnaonaje?
 
Pia kuna ule msemo usemao "Our failures are Known, but our successes are Not".......kwa hiyo kwa wale mtakao ponda badala ya kudiscuss hoja niliyoiweka ya Usiri, mjue kwamba kwa sababu ya usiri huo....mambo mazuri wanayofanya hamuwezi kuyasikia...mtasikia mabaya tu....kwa kuwa Secret Service ya ukweli inabidi iwe Secret!
 
Moja ya kazi za hizi National Intelligences ni kuweka siri. Lakini mambo ya CIA, MOSAD, KGB na wengineo yapo kila sehemu.

Ila hawa ndugu zetu wa TISS wamejitahidi katika hii section ya kuweka siri....yaani hawana WEBSITE, halawa TWITTER account, hawana FACEBOOK account, na wala hawa OFFICIAL EMAIL.

Hawana PR (public relation person), ingawa Nzoka sijui nani alijaribu kufanya kazi hiyo kile kipindi Dr Wa ukweli alivyokuwa anatafuta Wachakachuaji.

Yaani ukitaka kusikia chochote kuhusu hawa Jamaa, ni lazima uje JF, ambapo pia story nyingi ni story tu na hazina ukweli.

Hata kwenye hii BUDGET sijasikia kipengele kilichotengwa kwa TISS......hivi POSHO zao nao wanakatwa?.....hivi kuna KIKAO cha BUNGE cha kuwadiscuss hawa jamaa.....mwenyekiti wake nani?

Hongereni TISS kwa kuwa Secret Service ya Ukweli.....sio wenzenu CIA information zao zipo nje nje tu kila sehemu.

Wadau mnaonaje?

hasa za kuiba kura kwenye chaguzi za tz. kwanza me sioni hata faida yao kwa taifa letu... rushwa haiishi,ujambazi upo,madawa ya kulevya kila kona,mauaji ya wananchi kwenye uhalifu,mipakani kuna maaskari na wanajeshi sehemu nyingine na hivyo vyote hapo vina taasisi zake. sasa hawa jamaa wanafanya nini? usalama gani huo? eti utakuta wamemzunguka baba riz1,sasa nani ana shida na huyo mtu...wanakula hela tu..... masifa mengine bana!!!!!!!!!!!!!
 
..Hongereni TISS kwa kuwa Secret Service ya Ukweli.....sio wenzenu CIA information zao zipo nje nje tu kila sehemu.

Wadau mnaonaje?
Unadhani waliwezaje kumkamata/kumuua Usama?
 
Hivi kuna usalama wa taifa tanzania au kiini macho tu?
au kazi yao kumlinda JK pekee huku wakiacha makaburu na wazungu wengine wakisafirisha madini yetu usiku wa manane,
wakiacha wanyama wetu wanaibwa usiku.kazi yao nn sasa au tuseme polisi ndio kila kitu?
Nadhani hii sekta ingefungwa wanatumia garama na kodi zetu bure sioni cha maana kwao.
Tujiulize ile kashfa ya kutumika kuchakachua kura wamejisafisha??Mi nlidhani kazi yao ni kulinda sii usalama wa siasa tu pia kulinda uchumi wetu na vyanzo vyake kwa ujumla,kuzuia mikataba feki nk....KAMA YUPO HAPA AJITOKEZE AKANUSHE HAYA.
 
Moja ya kazi za hizi National Intelligences ni kuweka siri. Lakini mambo ya CIA, MOSAD, KGB na wengineo yapo kila sehemu.

TISS kazi yao ni kuweka siri ya jinsi nchi inavyotafunwa na wachache.....na pia kazi yao kubwa siku hizi ni kutafuta na kuwaharass wote wanaoisema vibaya serikali ya muheshimiwa au wanaomsema vibaya muheshimiwa na pia wanaoingilia anga za muheshimiwa.

Mataifa yaliondelea, vyombo vyao kama TISS wala haviko tena kwenye zama za usiri ebu cheki websites zao hapa (hadi kuna sections za ajira!!!)

https://www.cia.gov/
http://www.fsb.ru/ (hii ni ya Russia; KGB ilikua dissolved mwaka 1994 au 1995)
https://www.sis.gov.uk/ (hii ni ya UK; yaani hadi wameweka picha ya bosi wao!!!)
www.mossad.gov.il (hii ni ya Israel)

Hapa kwetu TISS ni kizungumkuti!! Kazi zenyewe za kupeana...baba, watoto, wajukuu, wajomba.................


 
... rushwa haiishi,ujambazi upo,madawa ya kulevya kila kona,mauaji ya wananchi kwenye uhalifu,mipakani kuna maaskari na wanajeshi sehemu nyingine na hivyo vyote hapo vina taasisi zake. sasa hawa jamaa wanafanya nini? !!!!

yaani TISS ni PCCB, polisi na Jeshi ? Great Sinker
 
hasa za kuiba kura kwenye chaguzi za tz. kwanza me sioni hata faida yao kwa taifa letu... rushwa haiishi,ujambazi upo,madawa ya kulevya kila kona,mauaji ya wananchi kwenye uhalifu,mipakani kuna maaskari na wanajeshi sehemu nyingine na hivyo vyote hapo vina taasisi zake. sasa hawa jamaa wanafanya nini? usalama gani huo? eti utakuta wamemzunguka baba riz1,sasa nani ana shida na huyo mtu...wanakula hela tu..... masifa mengine bana!!!!!!!!!!!!!

TISS hawana faida kwa maslahi ya taifa ni bora ingefutwa kuliko kumaliza bure hala za walipa kodi
 
hao TISS, WANAFANYA UJASUSI WA KIZAMANI, ni sawa na wachawi tu, wanahangaika na adui ambae hawezi kudhuru taifa, wamegeuka kua adui wa kwanza wa Watanzani........!
wanahangaika kufuatilia humu JF kujua siri ya mwizi gani inatoka ili waanze kuizima.
wanaficha wezi wa mali ya umma, wanawawinda wanaopambana na uhalifu wa Taifa.
 
yaani TISS ni PCCB, polisi na Jeshi ? Great Sinker


Mkuu kazi ya intelligence officer ni kuhakikisha kuwa maslahi ya taifa yanalindwa asilimai 100! Sasa katika ujambazi na matukio aliyosema mkuu pale awali, maslahi ya taifa yanachezewa na kuibiwa! Ndio maana mkuu akasema aliyosema!!

Ndio maana wakaitwa Tanzania Intelligence and Security Service (TISS); kwa maana nyingine hawa ni overseer wa mambo yote ya kiusalama katika nchi. Hao PCCB, polisi na jeshi wanapaswa kuitegemea TISS katika kupata taarifa za kiusalama (sasa sijui hawafanyi hivyo au TISS hawajui kazi yao au hawatoi taarifa!!! mimi sijui)
 
Mkuu kazi ya intelligence officer ni kuhakikisha kuwa maslahi ya taifa yanalindwa asilimai 100! Sasa katika ujambazi na matukio aliyosema mkuu pale awali, maslahi ya taifa yanachezewa na kuibiwa! Ndio maana mkuu akasema aliyosema!!

na kazi ya polisi ni nini?
 
Nafikiri ni utendaji wa kazi wa kizamani tu,hawataki kibadilika.
 
Moja ya kazi za hizi National Intelligences ni kuweka siri. Lakini mambo ya CIA, MOSAD, KGB na wengineo yapo kila sehemu.

Ila hawa ndugu zetu wa TISS wamejitahidi katika hii section ya kuweka siri....yaani hawana WEBSITE, halawa TWITTER account, hawana FACEBOOK account, na wala hawa OFFICIAL EMAIL.

Hawana PR (public relation person), ingawa Nzoka sijui nani alijaribu kufanya kazi hiyo kile kipindi Dr Wa ukweli alivyokuwa anatafuta Wachakachuaji.

Yaani ukitaka kusikia chochote kuhusu hawa Jamaa, ni lazima uje JF, ambapo pia story nyingi ni story tu na hazina ukweli.

Hata kwenye hii BUDGET sijasikia kipengele kilichotengwa kwa TISS......hivi POSHO zao nao wanakatwa?.....hivi kuna KIKAO cha BUNGE cha kuwadiscuss hawa jamaa.....mwenyekiti wake nani?

Hongereni TISS kwa kuwa Secret Service ya Ukweli.....sio wenzenu CIA information zao zipo nje nje tu kila sehemu.

Wadau mnaonaje?

Mkuu, information za CIA, Mossad na wengineo, ambao unafikiri zipo nje nje, Ni zile tu ambazo mashirika hayo yanataka wewe ufahamu kwa manufaa ya mashirika hayo. Ni habari ambazo zinatolewa na kudhibitiwa na vitengo vya "disinformation and misinformation". Kwa hiyo hapo ni kwamba TISS hawajafanikiwa kwenye hivyo vitengo kama ambavyo wanashindwa hata kufanya economic and technological espionage. Hamna haja ya kuwasifia.
 
hao TISS, WANAFANYA UJASUSI WA KIZAMANI, ni sawa na wachawi tu, wanahangaika na adui ambae hawezi kudhuru taifa, wamegeuka kua adui wa kwanza wa Watanzani........!
wanahangaika kufuatilia humu JF kujua siri ya mwizi gani inatoka ili waanze kuizima.
wanaficha wezi wa mali ya umma, wanawawinda wanaopambana na uhalifu wa Taifa.

Ni ajabu wakati hiyo siyo kazi yao kisheria....katika sheria ya TISS No. 15 ya 1996 Part II, section 5, subsection 2 kinasema; nanukuu:

It shall not be a function of the Service-
(a) to enforce measures for security; or(b) to institute surveillance of any person or category of persons by
reason only of his or their involvement in lawful protest, or dissent
in respect of any matter affecting the Constitution, the laws or
the Government of Tanzania.


Sasa siju ni lugha au?!?!? Hiyo ndiyo kazi yao kubwa sasa!!!


 
Back
Top Bottom