Timu ya matibabu ya China yapeleka huduma za afya bila malipo katika wilaya ya mpakani ya Uganda

Timu ya matibabu ya China yapeleka huduma za afya bila malipo katika wilaya ya mpakani ya Uganda

ldleo

JF-Expert Member
Joined
Jan 9, 2010
Posts
1,242
Reaction score
1,212
0e1b40de63cf4ebf99a60daf696ca883.png


Wakati jua lilipochomoza kwenye eneo la Bonde la Ufa katika wilaya ya mbali ya Magharibi ya Kikuube, Jennifer Nyangoma mwenye umri wa miaka 45 alienda kwenye kambi ya matibabu ya bure iliyokuwa ikisubiriwa na watu wengi.

Kwa wiki kadhaa, wanakijiji katika eneo hili linalopakana na mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo walikuwa wamesikia kuhusu huduma ya afya iliyoandaliwa na timu ya matibabu ya China kutoka Kampala, umbali wa zaidi ya kilomita 300.

Zaidi ya madaktari 20 wa Uganda walijiunga na timu hiyo, yenye madaktari wa magonjwa ya moyo, madaktari wa watoto, madaktari bingwa wa upasuaji wa jumla, wataalam wa akyupancha na wataalam wa afya ya umma kutoka timu ya 24 ya matibabu ya China. Walipoanzisha Kituo cha Afya cha Buhuka III, ambacho ni cha ngazi ya jamii kinachohudumia zaidi ya watu 10,000, Nyangoma alikuwa miongoni mwa watu wa kwanza kabisa kwenye foleni.

Baada ya kuchunguzwa, madaktari walipendekeza afanyiwe akyupancha, tiba ya jadi ya Kichina ya sindano.

"Madaktari wamenichunguza na kusema watanichomeka sindano kadhaa. Nilipata matibabu na natumai nitapata nafuu. Nimekwenda kwenye vituo kadhaa vya afya, lakini bado ninaendelea kusumbuliwa na viungo na mgongo," Nyangoma aliiambia Xinhua.

Kufikia adhuhuri, mamia ya watu walikuwa wamekusanyika katika eneo la kusubiri lenye ulinzi. Miongoni mwao alikuwepo Evelyn Atuhura mwenye umri wa miaka 30 na watoto wake watatu.

"Ilipofika saa moja asubuhi nilikuwa tayari nimeshaamka kuwaandaa watoto ili waje hapa, afya ya watoto wangu sio nzuri kabisa, Wachina wametupa matibabu, nawashukuru sana," alisema huku akipokea dawa.

Linard Kule, kaimu mfawidhi wa kituo hicho cha afya, alisema kambi hiyo sio tu inatoa huduma muhimu na vifaa tiba bali pia inakuza utoaji wa maarifa kati ya wataalamu wa afya wa China na Uganda.

Li Yun, mkuu wa timu ya madaktari wa China, alisema kambi hiyo inalenga kuhudumia takriban watu 1,000. "Pia tulijifunza mengi kutoka kwa wenzetu wa Uganda. Nimetiwa moyo na ujasiri wa wahudumu wa afya wa eneo hilo wanaotoa huduma katika eneo la mbali huku wakiwa na rasilimali chache tu," alisema daktari huyo wa China.

Kambi hiyo ya kila mwaka huandaliwa na Shirika la Kitaifa la Mafuta la China Offshore (CNOOC), ambalo linaendeleza mradi wa mafuta wa Kingfisher karibu na hapo.

Hu Weijie, kaimu rais wa CNOOC Uganda Limited, alisema mpango huo unaonesha kujitolea kwa muda mrefu kwa kampuni hiyo kwenye masuala ya afya na ustawi wa wakaazi wa eneo hilo.

"Tangu mpango huu uanze, maelfu ya watu wamepata huduma muhimu za kimatibabu," Hu alisema, akiongeza kuwa CNOOC inapoendeleza sekta ya mafuta na gesi ya Uganda, inazingatia na afya na usalama wa watu pia.

"Afya sio tu haki ya msingi ya binadamu, bali pia ni msingi wa familia imara, jamii zenye tija, na ukuaji endelevu wa taifa," alisema.

Ushirikiano wa afya ya umma ni sehemu muhimu ya hatua 10 za ushirikiano zilizotangazwa kwenye Mkutano wa Beijing wa 2024 wa Baraza la Ushirikiano kati ya China na Afrika (FOCAC), alisema Fan Xuecheng, mwambata mshauri wa Ubalozi wa China nchini Uganda.

"China iliahidi kusaidia kujenga hospitali nyingi zaidi barani Afrika, kuendelea kutuma timu za matibabu, kuimarisha kinga na udhibiti wa magonjwa kwa pamoja, na kuongeza upatikanaji wa dawa muhimu na mafunzo ya matibabu," Fan alisema. "Hii haiwakilishi tu dhamira ya China kwa sekta ya afya ya Afrika bali pia imani yetu katika kujenga mustakabali wa pamoja ambapo maendeleo na utu vinaenda sambamba."

Alisema timu za matibabu za China zimetoa ushauri wa kimatibabu kwa mamia na maelfu ya watu nchini Uganda tangu 1983, kusaidia hospitali za nchi hiyo, na kutoa mafunzo kwa watumishi wa afya.

"Katika vituo vyote vya mijini na vijijini, madaktari wa China wamefanya kazi bega kwa bega na wenzao wa Uganda kuboresha maisha. Timu iliyopo hapa leo inaendeleza utamaduni huu wa kujivunia, ikitoa sio tu vifaa na huduma, bali pia matumaini, uaminifu, na mshikamano," Fan alisema.
 
Polepole alikuwa anaota na hizi dili...
Bahati mbaya kama washabiki walivyo, alidhani Kyuba ni Ulaya...
Ikawa kila akijipange na timu za madaktari wa kyuba, anakuta kumbe wanahitaji makazi yao na mishahara yao kutoka kwa bajeti ya afya wakati wachina wanalipiwa na nchi yao....
 
Back
Top Bottom