Timu ya kampeni ya Dr. Magufuli yasambaratika

Timu ya kampeni ya Dr. Magufuli yasambaratika

VUTA-NKUVUTE

JF-Expert Member
Joined
Nov 25, 2010
Posts
6,140
Reaction score
18,004
Nimeambiwa kuwa ile ya kampeni ya CCM iliyoundwa kwa kumsaidia Dr. Magufuli na Mama Samia imesambaratika jana usiku baada ya kikao cha kimkakati. Nimearifiwa na mmoja wa wajumbe wa timu hiyo kuwa kusambaratika kwa timu hiyo kunatokana na sababu mbalimbali. Wapo wajumbe waliosusa baada ya kuona wananchi hawaelewi somo la CCM na kuielewa Ilani. Wananchi wamekuwa hawaelewi wanachoambiwa na sasa wajumbe wanaishiwa cha kusema.

Wapo wajumbe waliosusa kwakuwa wanatuhumiana, na hata na Dr. Magufuli mwenyewe, kuwa ni popo wa kisiasa. Wanaunga mkono harakati za wapinzani kwa kificho na kumharibia Dr. Magufuli majukwaani kwa kutamka maneno ya kukwaza na kukera yanayochochea hasira za wananchi dhidi ya wagombea wa CCM wa ngazi za Urais, Ubunge na Udiwani.

Wapo wajumbe waliosusa kutokana na kutotimiziwa matakwa yao hasa ya malipo kwa kila siku wanayoifanyia kazi. Wajumbe hao wamesema kuwa hawana muda wa kusubiri kulipwa baadaye kwakuwa uchaguzi ni bahati nasibu na lolote laweza kutokea. Wanasisitiza kulipwa marupurupu yao sasa kwa mujibu wa makubaliano ya kichama na kutoahidiwa kulipwa baada ya uchaguzi.

Wapo wajumbe waliosusa kwakuwa hawapewi uzito na umaarufu kama ilivyotarajiwa. Wanamlaumu Dr. Magufuli na viongozi waandamizi chamani, kwa mfano, kumuamini sana Abdallah Bulembo ambaye hana hadhi kichama, kisera na kihela kupewa nafasi ya kutawala majukwaa kama afanyavyo sasa. Wanalalama kuwa watu maarufu wamewekwa kando na sasa wanaanza kuota utando.

Sasa timu imesambaratika. Dr. Magufuli yuko njiapanda kikampeni. Itambidi kupambana kiume ili kuendelea kujieleza mbele ya wananchi. Apambane kivyake sasa na watakaobaki naye!

Mzee Tupatupa wa Lumumba, Dar es Salaam
 
VUTA-NKUVUTE

Kauli mbiu yenu Hapa ni kazi tu, kweli mwaka huu kazi mnayo.
Ndio sababu kutwa kucha CCM inajaribu kufanya kampeni kwa kutumia lugha chafu, na hata kupika matokeo kwa kutumia TWAWEZA na REDET.
Ukweli ni kwamba Magufuli na CCM haiuziki, watu tumewachoka, na siyo siri.
Na hizo njama zinazotumiwa kutaka kulazimisha kukubalika ndizo zinazokwenda kuwamaliza!
 
Last edited by a moderator:
Mbona hilo liko wazi. Kampeni za magufuri ni tofauti na utamaduni wa ccm, yeye anailalamikia serikali iliyopo madarakani kwa kutotimiza wajibu wake na kuahidi wananchi 'mahakama ya mafisadi'. wanaoambatana naye wanajiuliza hao mafisadi ni nani kama si wao na rais wao, swali gumu zaidi ni hiyo ahadi ya mahakama anaitoa kifungu kipi cha ilani yao na katiba.

Zaidi msemo wa Tanzania ya magufuri unawachanganya sana...hawamwelewi....na mbaya zaidi kushindwa kumnadi Chenge ni mojapo ya tatizo la kampeni hizo.....ukweli hawafiki mbali....

Mkanganyiko huo ulishatabiliwa na lazime utimie.......
 
VUTA-NKUVUTE

Mtoa mada una bahati sana kwamba habari yako itakuwa ni ya kuwafurahisha wengi hapa jamvini hasa wale wanaopenda

kutukana. Kwa mfano ungeandika Lowassa njiapanda timu ya kampeni imesambaratika ungetukanwa ungeitwa mnafiki,

Magamba, msaliti, Yuda yaani kila jina. Ila angalau ubunifu wako mzuri hapa utapewa hongera na kuonekana mpenda

mabadiliko.
 
Last edited by a moderator:
TWANUNULIWA zamani TWAWEZA; hilo wamelisikia na kulizingatia katika tafiti zao zijazo au Mwigulu Nchemba na Hamis Kigwangala wamewashauri vipi?!
 
Mtoa mada una bahati sana kwamba habari yako itakuwa ni ya kuwafurahisha wengi hapa jamvini hasa wale wanaopenda

kutukana. Kwa mfano ungeandika Lowassa njiapanda timu ya kampeni imesambaratika ungetukanwa ungeitwa mnafiki,

Magamba, msaliti, Yuda yaani kila jina. Ila angalau ubunifu wako mzuri hapa utapewa hongera na kuonekana mpenda

mabadiliko.

Sasa ataandikaje Lowassa njiapanda wakati siyo kweli?

Kwani ni uongo kwamba hata Bro. Mako amelikimbia jukwaa? Yuko wapi Mwigulu? Kwani ni uongo kwamba Magufuli aliwalalamikia wenzake kwamba mchana wanajidai ccm lakini usiku wanahamia UKAWA?

VUTA-NKUVUTE, Mzee Tupa tupa mimi huwa namkubali!!
 
Nimeambiwa kuwa ile ya kampeni ya CCM iliyoundwa kwa kumsaidia Dr. Magufuli na Mama Samia imesambaratika jana usiku baada ya kikao cha kimkakati. Nimearifiwa na mmoja wa wajumbe wa timu hiyo kuwa kusambaratika kwa timu hiyo kunatokana na sababu mbalimbali. Wapo wajumbe waliosusa baada ya kuona wananchi hawaelewi somo la CCM na kuielewa Ilani. Wananchi wamekuwa hawaelewi wanachoambiwa na sasa wajumbe wanaishiwa cha kusema.

Wapo wajumbe waliosusa kwakuwa wanatuhumiana, na hata na Dr. Magufuli mwenyewe, kuwa ni popo wa kisiasa. Wanaunga mkono harakati za wapinzani kwa kificho na kumharibia Dr. Magufuli majukwaani kwa kutamka maneno ya kukwaza na kukera yanayochochea hasira za wananchi dhidi ya wagombea wa CCM wa ngazi za Urais, Ubunge na Udiwani.

Wapo wajumbe waliosusa kutokana na kutotimiziwa matakwa yao hasa ya malipo kwa kila siku wanayoifanyia kazi. Wajumbe hao wamesema kuwa hawana muda wa kusubiri kulipwa baadaye kwakuwa uchaguzi ni bahati nasibu na lolote laweza kutokea. Wanasisitiza kulipwa marupurupu yao sasa kwa mujibu wa makubaliano ya kichama na kutoahidiwa kulipwa baada ya uchaguzi.

Wapo wajumbe waliosusa kwakuwa hawapewi uzito na umaarufu kama ilivyotarajiwa. Wanamlaumu Dr. Magufuli na viongozi waandamizi chamani, kwa mfano, kumuamini sana Abdallah Bulembo ambaye hana hadhi kichama, kisera na kihela kupewa nafasi ya kutawala majukwaa kama afanyavyo sasa. Wanalalama kuwa watu maarufu wamewekwa kando na sasa wanaanza kuota utando.

Sasa timu imesambaratika. Dr. Magufuli yuko njiapanda kikampeni. Itambidi kupambana kiume ili kuendelea kujieleza mbele ya wananchi. Apambane kivyake sasa na watakaobaki naye!

Mzee Tupatupa wa Lumumba, Dar es Salaam

''mzee tupatupa saa kumi nanusu saizi bado ujaamka usingizini tu???''
 
Nimeambiwa kuwa ile ya kampeni ya CCM iliyoundwa kwa kumsaidia Dr. Magufuli na Mama Samia imesambaratika jana usiku baada ya kikao cha kimkakati. Nimearifiwa na mmoja wa wajumbe wa timu hiyo kuwa kusambaratika kwa timu hiyo kunatokana na sababu mbalimbali. Wapo wajumbe waliosusa baada ya kuona wananchi hawaelewi somo la CCM na kuielewa Ilani. Wananchi wamekuwa hawaelewi wanachoambiwa na sasa wajumbe wanaishiwa cha kusema.

Wapo wajumbe waliosusa kwakuwa wanatuhumiana, na hata na Dr. Magufuli mwenyewe, kuwa ni popo wa kisiasa. Wanaunga mkono harakati za wapinzani kwa kificho na kumharibia Dr. Magufuli majukwaani kwa kutamka maneno ya kukwaza na kukera yanayochochea hasira za wananchi dhidi ya wagombea wa CCM wa ngazi za Urais, Ubunge na Udiwani.

Wapo wajumbe waliosusa kutokana na kutotimiziwa matakwa yao hasa ya malipo kwa kila siku wanayoifanyia kazi. Wajumbe hao wamesema kuwa hawana muda wa kusubiri kulipwa baadaye kwakuwa uchaguzi ni bahati nasibu na lolote laweza kutokea. Wanasisitiza kulipwa marupurupu yao sasa kwa mujibu wa makubaliano ya kichama na kutoahidiwa kulipwa baada ya uchaguzi.

Wapo wajumbe waliosusa kwakuwa hawapewi uzito na umaarufu kama ilivyotarajiwa. Wanamlaumu Dr. Magufuli na viongozi waandamizi chamani, kwa mfano, kumuamini sana Abdallah Bulembo ambaye hana hadhi kichama, kisera na kihela kupewa nafasi ya kutawala majukwaa kama afanyavyo sasa. Wanalalama kuwa watu maarufu wamewekwa kando na sasa wanaanza kuota utando.

Sasa timu imesambaratika. Dr. Magufuli yuko njiapanda kikampeni. Itambidi kupambana kiume ili kuendelea kujieleza mbele ya wananchi. Apambane kivyake sasa na watakaobaki naye!

Mzee Tupatupa wa Lumumba, Dar es Salaam

Labda aongeze na team ya wanamazoezi ili wawe wanapiga pushup pamoja. Naona kama watavutia pia!!!!!!!!!!!!!!!

Halafu, ushauri wangu wa pili, wapite kila nyumba wakigawa kila mpiga kura zile billion 13 walizowagawia wale waliofika bei ili kuhakikisha Watanzania wote wahanga wa ccm wanafika bei.

Kinyume cha pale, wahakikishe wanayo mataulo ya kutosha kujifutia machozi!
 
Back
Top Bottom