TIMU Magufuli tukutane hapa

TIMU Magufuli tukutane hapa

Hao wapinzani wana nini zaidi ya kuwa na ilani mbovu inayobebwa na mgombea mgonjwa? Asanteni Watanzania kwa kuamua kumchagua Magufuli

Mkuu umezisoma ilani za vyama vyote? Au ni mahaba ya kisiasa tu yanakuendesha? Hebu tupe tofauti ya ilani za vyama hivi (CCM V/s Chadema/ Ukawa) ndipo tujue kama ni ilani mbovu ama la! Vinginevyo tutajua umeongea tu na hujui chochote kuhusu ilani za uchagzi za vyama hivi. Au unashabikia chama aidha kwa sababu ya maslahi ya siku moja (njaa ya siku moja) au unashabikia tu bila kuelewa chochote then unabaki kusota na kulalamika kwa miaka mitano.
 
magufuri anapita kwa kukosa mpinzani makini, ila sio kiongozi bora.
 
Mwaka huu wapinzani mwaka huu mna kazi nzito Mana huyu mgufuli anakimbiza ilee mbaya hapa kazi tu

Edit post yako mkuu:
Mwaka huu wapinzani mwaka huu, Mana, mgufuli, ilee------ndo nini?
Au ndo unazidi kuaminisha watu kwamba CCM haitoi kipaumbele katika elimu ili iendelee kutawala?
 
Ndugu yangu ni ishara tosha kwamba watu hawaitaki CCM Kabisa wanaotangazwa ni wasanii kwenye ujio wa magufuli na hii yote ni kwa sababu CCM imezoea mizaha na usanii,bila diamond,na wapuuzi wenzake hakuna mkutano.Sisi kwetu huku baada ya kuona hakuna mtu kwenye mkutano wakaanza maonyesho ya nyoka nikacheka sana kweli CCM wamekaangika vzr sana ambaye hajaanza kufungasha mizigo yake shauri yake gari litamuacha.
 
Wadau kama wewe unampenda kiongozi huyu shupavu ingia hapa tuungane kumuunga mkono huyu Jembe na mzalendo CCM imekufa lakini Magufuli bado ana heshima na si fisadi kama baadhi ya wajumbe waliopo hata upinzani Naamini kuchagua mtu na si chama ndiyo itakayoivusha Tanzania yetu salama kwenye mtihani huu mgumu wa uchaguzi mwaka huu.

Ungana nasi kutengeneza timu ya Ushindi ya ndugu yetu John Pombe Magufuli na tunaamini atayafanyia kazi yale yoote tuliyokubaliana nae kuhusu kuifufua Tanzania inayozama...

Wasalaaam


Sawa kiongozi ila habari njema ni hii Ndugu yangu ni ishara tosha kwamba watu hawaitaki CCM Kabisa wanaotangazwa ni wasanii kwenye ujio wa magufuli na hii yote ni kwa sababu CCM imezoea mizaha na usanii,bila diamond,na wapuuzi wenzake hakuna mkutano.Sisi kwetu huku baada ya kuona hakuna mtu kwenye mkutano wakaanza maonyesho ya nyoka nikacheka sana kweli CCM wamekaangika vzr sana ambaye hajaanza kufungasha mizigo yake shauri yake gari litamuacha.
 
Na biashara hiyo ya mbele kwa mbele inawafaa sana na ndio mkaweka muziki.
 
Nina imani na Magufuli ila sina Imani na timu yote ya CCM na mfumo wake, tatizo sn
 
Tunaruhusiwa kusema madhaifu yake hapa pia?
Jifunze kwa Team Lowasa ,hata siku moja hawatazungumzia madhaifu ya Lowasa,bali ni yale mazuri tu,na ndivyo tunataka kwa Team Magufuli,madhaifu yatazungumziwa na Team Lowasa ,na pia madhaifu ya Lowasa yatazungumziwa na Team Magufuli,huwezi kuzungumzia madhaifu kwa mtu wako,wewe utakuwa sio mwana mkakati,lengo kuu la hizi team,ni kuwajenga wagombea wao na sio kuwabomoa hiyo ndio siasa.Hapa tunaongelea mazuri tu ya Magufuli na madhaifu ya wapinzani wa Magufuli,ukitaka kujua huu ukweli nenda Team Lowasa halafu jaribu kuzungumzia madhaifu yake halafu uje utupe majibu.
 
Back
Top Bottom