Tigo tutakutana mahakamani

Abdull Kazi

JF-Expert Member
Dec 29, 2012
322
255
Kampuni ya simu ya tigo imekuwa ikinikata kiasi cha fedha mara kwa mara huku wakinitumia ujumbe kuwa nimesikiliza hadithi wanazozijua wao,binafsi sikuwahi kujiunga na huduma yoyote zaidi ya ile ya kupiga mitandao tofauti,awali nilipokuwa ninapata ujumbe wMao unaonieleza kuwa nimekatwa kiasi cha sh.320 kwa kusikiliza hadithi hizo nilijibu kwa kuandika neno ondoa na kutuma katika namba iliyoniletea ujumbe na zoezi lilikuwa linasitishwa kwa muda sasa wameanza tena.Nimedhamiria kuwashitaki kwa kuwa suala hili limepigiwa kelele bungeni na kwenye vyombo vya habari bila mafanikio nafanya hivi kwa ajili ya kutetea haki yangu na wengine dhidi ya wizi wa aina hii ninazo mesegi zote kama ushahidi na ninawaomba na wengine waliokutwa na madhila kama yangu tuungane ktk hili
 
sawa mimi wa pili, nakatwa sh 1500 kila mwez eti sijui bima pona nimeenda kila branch wanasema wamenitoa ikifika siku 30 wanakata yani sijui nifanyaje, najiunga nawe ni pm nipo serious
 
Poleni sana kwa shida inayowakumba. Ukienda mahakamani mkuu,kwenye systeam wewe utaonekana umejiunga mwenyewe. Me nawashauri wote mnaopatwa na hiyo adha. Kwenye hizo sms mnazopata huwa kuna neno linaanza kwa herufi kubwa. Zingatia hilo neno na andika neno'ondoa acha nafasi,kisha andika hilo neno lenye herufi kubwa na tuma kwa number inayokutumia ujumbe. Mfano km unapata hadithi neno HADITHI litaanza then hadithi yenyewe. Kwa hiyo andika "ONDOA HADITHI" Kisha tuma kwa number inayokutumia ujumbe.
 
Pekela mahakamwni hao waizi sana mi wameniibia kununua salio kwa tigo pesa na s8japata mw3zi sasa napiga simu wananambia watarudisha
 
Poleni sana kwa shida inayowakumba. Ukienda mahakamani mkuu,kwenye systeam wewe utaonekana umejiunga mwenyewe. Me nawashauri wote mnaopatwa na hiyo adha. Kwenye hizo sms mnazopata huwa kuna neno linaanza kwa herufi kubwa. Zingatia hilo neno na andika neno'ondoa acha nafasi,kisha andika hilo neno lenye herufi kubwa na tuma kwa number inayokutumia ujumbe. Mfano km unapata hadithi neno HADITHI litaanza then hadithi yenyewe. Kwa hiyo andika "ONDOA HADITHI" Kisha tuma kwa number inayokutumia ujumbe.
 
Hata voda wanatabia kama hizo .Mimi walinikata hela eti nilikopa mwezi ambao nilikuwa sijanunua hiyo line.nimewapigia wanachoogea hakieleweki.Saizi hawapokei nikiwapigia Mitandao ya cm wanatuibia sana hawa
 
Tigo wapuuzi sana. Wanakukata pesa yako ukiuluza wanasema ulikopa wakati sio kweli.
 
Mimi baaada ya kugundua upuuzi wa Tigo nimegoma kuweka salio Mwezi wa tatu sasa naitumia kupokea cm basi watejawote tukiweka msimamo watatia adabu

Hata mimi nimechukua uamuzi kama wako!!! , kwa zaidi ya miaka kumi nimekua mteja wa Tigo, wizi unaofanyika sasa hauvumiliki , idea yangu ni kutoweka salio kwa mwaka mzima huku nikiwahamishia wanaonipigia kwenye Tigo ,namba mpya nilikohamia .baada ya hapo simu tigo itapoteza fursa ya kipekee kukaa mfukoni mwangu ,nitaacha nyumbani ikisubiri miss calls za wale wanaopiga baada ya miezi!!
 
Kuwashtaki inawezekana ila evidence ndio tatizo so inabidi pale unapopata tatizo unaweka kumbukumbu yako binafsi kuwa siku flani tarehe flani nilikatwa kiasi fulani ukiwapigia simu unajirekodi mana wana empty promices sana wale wahudumu watakuambia piga baada ya saa 24 itakua tayari so ww warekodi 2 mwisho wa cku unatinga mahakamani una pa kuanzia
 
Hata mimi nimechukua uamuzi kama wako!!! , kwa zaidi ya miaka kumi nimekua mteja wa Tigo, wizi unaofanyika sasa hauvumiliki , idea yangu ni kutoweka salio kwa mwaka mzima huku nikiwahamishia wanaonipigia kwenye Tigo ,namba mpya nilikohamia .baada ya hapo simu tigo itapoteza fursa ya kipekee kukaa mfukoni mwangu ,nitaacha nyumbani ikisubiri miss calls za wale wanaopiga baada ya miezi!!
mimi zoezi hilo nilishalianza mwezi wa pili...iko kama landline,kila jioni nikitoka kazini naangalia missed calls tu.
 
Poleni sana kwa shida inayowakumba. Ukienda mahakamani mkuu,kwenye systeam wewe utaonekana umejiunga mwenyewe. Me nawashauri wote mnaopatwa na hiyo adha. Kwenye hizo sms mnazopata huwa kuna neno linaanza kwa herufi kubwa. Zingatia hilo neno na andika neno'ondoa acha nafasi,kisha andika hilo neno lenye herufi kubwa na tuma kwa number inayokutumia ujumbe. Mfano km unapata hadithi neno HADITHI litaanza then hadithi yenyewe. Kwa hiyo andika "ONDOA HADITHI" Kisha tuma kwa number inayokutumia ujumbe.
Mkuu haya makampuni ni ya wezi. Mimi Vodacom walinitumia ujumbe juzi kuwa namba yako imeshinda zawadi, tuma neno "NDIYO" kupata zawadi yako. Nilipojibu ujumbe huo nikaambiwa nina pointi 50 za kushinda bodaboda, na wakakata hela kwenye account yangu. Huo sio wizi kweli? Wajuzi wa sheria tusaidieni.
 
Back
Top Bottom