Tigo leo mmeniharibia sana

Tigo leo mmeniharibia sana

Ijumaa usiku SAA sita nimenunua vocha ya buku kwenye duka la mangi mchelewaji kufunga ili nipate MB za kubrowse nikashangaa naweka naambiwa nadaiwa bado sh 500,nikijiuliza nilikopa SAA ngapi ilihali hata sijui huo mkopo wanabonyeza code zipi,yani wamekuwa wasanii sanii,na Leo ndio komesha nimerushiwa hela mpaka dk hii sijaitoa mtandao umekuja rudi saa saba kasoro usiku,bila kuomba msamaha wowote.
 
Mimi toka saa sita nimeganda tu Guest mtoto hupatikan hewani. Chumba nimeshalipia na mtoto mwenyewe nimemfukuzia mwaka wa tano huu, Jana ndio kanikubalia leo nikapige shoo kutwa nzima kwa kua kesho atasafiri kwenda nje kusoma.

Nilifikiria hata Nipige substitute kwa michepuko yangu mengine ili hela ya chumba isiende bure lakini wote bahati mbaya wako Tigo nao na muhudumu kagoma kurudisha hela. Leo kweli NIMEWEZWA

Ahahahaha unaendana na id yako, pole mkuu.
 
Toka asubuhi huku nilipo simu haziingii wala haziendi,sms pia, tgo pesa ndio kabisaa!.. Mbaya zaidi siku ya leo nilikuwa na mihadi na mtu kila nikimpigia Sim inakata, nimebadilisha line ni hivyo hivyo mpaka muda huu ninavyoandika hapa......

Cha ajabu hakuna notification yeyote mliyotupatia wateja wenu ili kuonyesha mnajari na mmegundua uwepo wa tatizo na mnaendelea kurekebisha,
Yaaani nyie mnaona ni kawaida tu hali kama hii,
Ila fresh tu najua nitakachowafanya mda si mrefu. .

Sie wengine Unguja hatuna hamu nao hao!
 
Wasamehe bule mkuu,kwa wasiofahamu,ni kuwa baada ya makampuni ya TIGO na VODACOM,kuuza(kubinafsisha vitengo vya power) minara yao kwa kampuni ya HELLIOS TOWERS,utendaji na ubora wa huduma umepungua sana,

HELLIOS TOWERS,inasimamia vitengo vyote vinavyohusu nishati ya umeme kwenye minara ya TIGO na VODA,kama mafuta(diesel),vipuri,majenereta,usalama wa mitambo,

Sasa tatizo kubwa sasa hv ni upatikanaji wa diesel,kutokana na umeme wa Tanesco kuwa na matatizo,herrios anaomba mafuta kutoka VODA na TIGO,harafu yeye anayagawa kwa makampuni mengine yanayo simamia minara,kwaiyo mafuta yakitoka kidogo,yeye mwenyewe HELLIOS,ili apate faida ya kuendesha shughuri zake,atanunua mafuta kidogo,kwaiyo hata minara itapata mafuta kidogo,na kama umeme wa GRID,haupo,mitambo itazima,na ndio maana network inapotea,

kwa ufupi ni usimamizi mbovu wa huyu dalali HELLIOS TOWERS,NI bora kipindi kile,makampuni yalikuwa yana deal na TIGO au VODA mojakwa moja,AIRTEL alishitukia usanii huu,akagoma kuuza minara yake,
Mbeya,mbozi mpaka Tunduma,leo hakuna mtandao wa tigo,kuanzia saa 12jioni,kwa sababu mnara mkubwa wa TIGO tunduma,umezima,mafuta yameisha,

Kwa uzembe wa aina hii ndin ttunakuja kuambiwa kwamba ''samahani wateja weju hali hii ilisababishwa na MATATIZO YAKIYO NJE YA UWEZO WETU'
 
Toka asubuhi huku nilipo simu haziingii wala haziendi,sms pia, tgo pesa ndio kabisaa!.. Mbaya zaidi siku ya leo nilikuwa na mihadi na mtu kila nikimpigia Sim inakata, nimebadilisha line ni hivyo hivyo mpaka muda huu ninavyoandika hapa......

Cha ajabu hakuna notification yeyote mliyotupatia wateja wenu ili kuonyesha mnajari na mmegundua uwepo wa tatizo na mnaendelea kurekebisha,
Yaaani nyie mnaona ni kawaida tu hali kama hii,
Ila fresh tu najua nitakachowafanya mda si mrefu. .
Mnaizungumzia Tigo ipi?
 
Shabash!..nilikuwa nadaiwa,jamaa nimemuendesha nimemtumia toka jana,mtandao unasumbua!
Kitachofata ni sound tu za kujifanya nafuatilia tigo wanirejeshee pesa yangu walioikata!!
Tigo wamenipa wiki nzima ya kulipa deni!.
Kama vp na leo wapotee tena!
 
Offer kutoka tigo, je inaendana na usumbufu waliopata wateja wao?
 

Attachments

  • 1447051712197.jpg
    1447051712197.jpg
    24.5 KB · Views: 141
He he hivi ni kweli usumbufu wa siku nzima mnaongwa dk 10..??tigo wanatutania
 
Hawa jamaa wametuharibia sana weekend hii. mi nilishatengeneza mazingira hom ili nikapige nje cup. mwisho wa siku nimejikuta nalala ugenini bila faida yoyote
Ha ha ha,
Dah kama mimi aisee. Unajua hizi nje cup kama ni wake za watu haitakiwi muwe mnaingia Guest hiyohiyo kila siku. Kila mkikutana mnapanga Guest mpya ili kua salama zaidi, na jina la guest unampa siku hiyohiyo asubuhi. Hapa ndipo tigo walipotuwezea aisee
 
Back
Top Bottom