huu mtandao sina hamu nao kabisaTangu asubuhi naingiza vocha za tigo kwa *104* napata meseji isemayo "Connection problem or invalid MMI"
Baada ya several attempts nikafanikiwa, lakini tena kujiunga na vifurushi kupitia *148*00# imekuwa shida ileile, napata meseji "Connection problem or invalid MMI"
Swali langu kwao kama wanaingia humu ni kwamba, je!! mtatufidiaje kwa adha tunayoipata mkizingatia kuwa kuna wengine wamefanikiwa kujiunga na vifurushi lakini mpaka sasa hawawezi kupiga simu wala kutuma sms kutokana na "Connection problem or invalid MMI"
huu mtandao sina hamu nao kabisa
Ulivyoingiza hiyo vocha washakataa VAT?Tangu asubuhi naingiza vocha za tigo kwa *104* napata meseji isemayo "Connection problem or invalid MMI"
Baada ya several attempts nikafanikiwa, lakini tena kujiunga na vifurushi kupitia *148*00# imekuwa shida ileile, napata meseji "Connection problem or invalid MMI"
Swali langu kwao kama wanaingia humu ni kwamba, je!! mtatufidiaje kwa adha tunayoipata mkizingatia kuwa kuna wengine wamefanikiwa kujiunga na vifurushi lakini mpaka sasa hawawezi kupiga simu wala kutuma sms kutokana na "Connection problem or invalid MMI"
Mko mtandao gani?Poleni sana Wateja wa huo mtandao,wengine tulisha hamaga kitambo hukooo
mie yaani nilihama kitambo, nilichimba shimo nikaizika na kupanda mwarobaini ili ukikua nijue pale kuna line ya tigo, ukiweka vocha hujaweka data, hujapiga ukiuliza ndani ya dk 2 unakuta vocha ni less, ukipiga customer care kuwapata mpaka sijui ukadhikiri uchi, wamekuwa ka ile ndege yetu PW, hawa nao hawana tofauti na kampuni ya tigo, hata ulalamike vipi ni kama unajaza maji kwenye pakacha au tengaPoleni sana Wateja wa huo mtandao,wengine tulisha hamaga kitambo hukooo
Wacha bwana!!!? Kamnunua zanzbartel!!!?huo mtandao wa watoto wadogo sijawahi hata kufikiria kununua line ya tigo maisha yangu yote mpaka leo.Vituko vyake ukimpigia mtu wa tigo from voda/airtel utasikia simu haipatikani kwa sasa,utarudia mara 5 hivi then itapatikana,mbaya zaidi kainunua zantel na kuiambukiza magonjwa yote ya tigo.
Kwa kujibu SMS hii Kwa neno OKTigo inakuomba radhi kwa usumbufu uliojitokeza tunakupatia Dk 5 za kupiga tigo kwenda tigo na Mb 1.
Mjiandae na hyo msg kesho.
Jaribu kuweka kwenye Tigo Pesa kisha nunua muda wa maongezi via Tigo Pesa, mambo ya vocha za kukwangua nishaachana nayo miaka 5 iliyopita