Tigo imekuwaje?

Faana

JF-Expert Member
Dec 12, 2011
31,922
33,364
Tangu asubuhi naingiza vocha za tigo kwa *104* napata meseji isemayo "Connection problem or invalid MMI"

Baada ya several attempts nikafanikiwa, lakini tena kujiunga na vifurushi kupitia *148*00# imekuwa shida ileile, napata meseji "Connection problem or invalid MMI"

Swali langu kwao kama wanaingia humu ni kwamba, je!! mtatufidiaje kwa adha tunayoipata mkizingatia kuwa kuna wengine wamefanikiwa kujiunga na vifurushi lakini mpaka sasa hawawezi kupiga simu wala kutuma sms kutokana na "Connection problem or invalid MMI"
 
huu mtandao sina hamu nao kabisa
 
Ulivyoingiza hiyo vocha washakataa VAT?
 
huo mtandao wa watoto wadogo sijawahi hata kufikiria kununua line ya tigo maisha yangu yote mpaka leo.Vituko vyake ukimpigia mtu wa tigo from voda/airtel utasikia simu haipatikani kwa sasa,utarudia mara 5 hivi then itapatikana,mbaya zaidi kainunua zantel na kuiambukiza magonjwa yote ya tigo.
 
Tigo ni WEZI, I mean ni wezi na nikitakiw akutoa ushahidi hapa nitatoa, Tigo ni weziiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiii
 
Poleni sana Wateja wa huo mtandao,wengine tulisha hamaga kitambo hukooo
mie yaani nilihama kitambo, nilichimba shimo nikaizika na kupanda mwarobaini ili ukikua nijue pale kuna line ya tigo, ukiweka vocha hujaweka data, hujapiga ukiuliza ndani ya dk 2 unakuta vocha ni less, ukipiga customer care kuwapata mpaka sijui ukadhikiri uchi, wamekuwa ka ile ndege yetu PW, hawa nao hawana tofauti na kampuni ya tigo, hata ulalamike vipi ni kama unajaza maji kwenye pakacha au tenga
 
Tigo inakuomba radhi kwa usumbufu uliojitokeza tunakupatia Dk 5 za kupiga tigo kwenda tigo na Mb 1.

Mjiandae na hyo msg kesho.
 
Wacha bwana!!!? Kamnunua zanzbartel!!!?
 
Jaribu kuweka kwenye Tigo Pesa kisha nunua muda wa maongezi via Tigo Pesa, mambo ya vocha za kukwangua nishaachana nayo miaka 5 iliyopita


Hata kama, shida ni network yao mchosho, nimekwenda nimefanya kila niwezalo nikiwa chini ya mnara wao sijafanikiwa
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…