Faida ya Halotel ni kupatikana maeneo mengi kwa spidi ya kawaida.
Kwa mfano ukiwa unatoka Moro kuja Dar, hata ukiwa porini kama mtandao wa halotel upo basi ni 3G, wakati hawa wengine 3G unaiacha Moro mjini.
Pia mitandao mingine inachagua sana maeneo, yaani katika mji mdogo tu, ukiwa mtaa huu 2G na huwezi kufungua hata web page ukiwa mtaa mwingine 3G na spidi imepanda kidogo, wakati kwa Halotel haiko hivyo, ingawa si kwa 100% ila inaizidi mitandao mingine.
Kwenye suala la spidi tigo 4G iko juu, ingawa sijawahi kupima ila nimetumia router za tigo (Huawei) 4G na halotel natumia pia. Ila udhaifu ndio huo nilioueleza hapo juu.
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.