TID amtembelea RC Makonda nyumbani kwake

TID amtembelea RC Makonda nyumbani kwake

476f00ac0e299660643243ba76f45e8e.jpg
Mapema leo Mwanamuziki Khalid Mohamed maarufu kama "Top In Dar" (TID) ambaye alikuwa miongoni mwa watu wa kwanza kuitwa polisi kwa mazungumzo ya tuhuma zake kuhusu anavyohusika na madawa ya kulevya, alifika nyumbani kwa Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam, Paul Makonda kwa ajili ya kumsalimia na mazungumzo ya kawaida
f47ba30c3a515c93d596169348cacac6.jpg
Kwa muda wote ambao wawili hao walipokuwa pamoja walionekana kufurahia mazungumzo yao, wakiwa wamekaa kama marafiki. Mkuu wa Mkoa akitumia muda wa mazungumzo hayo kumshauri TID kuhusu maisha kwa ujumla na umuhimu wa kumtegemea Mungu katika kila jambo analofanya

Kwa upande wake TID yeye alitumia muda huo kumweleza Paul Makonda kuhusu maisha ya kawaida na yale ya muziki, Aidha, mazungumzo ya wawili hayo yaligusa kuhusu namna wanavyoweza kuokoa vipaji vya wasanii

Aidha, TID amenukuliwa akisema "Muziki bila madawa ya kulevya inawezekana... This is the turning Point kwangu mimi na kizazi cha muziki huu wa kizazi kipya, nikiwa na Mhe. Makonda leo tukijadili jinsi ya kuokoa vipaji na sanaa kwa ujumla, Mungu ibariki bongo fleva, Mungu ibariki Tanzania".

Naye Makonda kupitia ukurasa wake wa Instagram ameandika "Mungu wetu hajalala na siku zote anampenda amtafutae, karibu tena nyumbani TID".
Mungu aibariki "Bongo Flava?"This is a joke!Hii ni sawa na kusema Mungu mbariki Shetani.Watu ni lazima wajue kwamba Bongo Flava ni ubunifu wa kuzimu and has got no relationship at all with God. Kwa hiyo kumhusisha Mungu na anything to do with Bongo Flava is an abomination.
 
Katika pitapita yangu nlipita kijiwe kimoja kupiga toli moja mbili tatu...nkaskiaa Jamaa wanasema Gari la tid limevunjwa kioo cha mbele....na hawakuchukua kitu ndani ya gari

Ova
 
Back
Top Bottom